Wanawake na Magari!

Wanawake na Magari!

Kwangu mimi, the most best cars are:

1) Lexus LS 460
2)Cadillac CT6
3)Audi S8
4)Jaguar XJ
5)BMW Alpina B7
6)Maserati Quattroporte
7)Aston Martin Rapide S
8)Mercedes-Benz AMG S65
We binti unaonekana unajua sana magari
 
Ni ulimbukeni tu kwa wachache , hasa wale ambao hawakuzaliwa na kuyakuta magari kwenye familia zao kabla ya kuolewa. Wale waliozaliwa na kukulia kwenye familia bora wala hawababaishwi nayo. Huyachukulia kawaida tu kama vile pasi ya kunyooshea nguo! Ni sawa na pesa tu. Inabidi uzoee kuzishika mapema tangu utotoni kwa kiasi kidogo kidogo (pocket money) ili Mungu akikujalia nyingi za kutosha ujanani na uzeeni uwe umezizoea na usiwe limbukeni. Naamini wote humu mnatambua jinsi malimbukeni waliopata pesa ukubwani bila ya kuzizoea mapema zinavyowasumbua. Wengine mpaka kusababisha vifo vyao kabla ya muda waliopangiwa na mola wao. Ulimbukeni hauna jinsia.
 
Habari wana jamii! Kwanza poleni kwa msiba wa Mzee Kingunge. Niingie kwenye maada. Katika pita pita kwenye familia nyingi nimegundua kama familia (mke, mme) wakiwa na gari moja basi hilo gari mara nyingi litakuwa linatumiwa na mke. Wanaume wengi hawajali hivyo yeye ataamua kupata daladala. Shida nyingine inayoonekana kwenye jamii wanawake wengi wakiwa wanamiliki magari wanakuwa jeuri na viburi hawana heshima kwa waume zao. Mfano mzuri nilishuhudia jamaa yangu ndoa yao ilivunjika baada ya mkewe kununua gari tu. Ijapokuwa jamaa nae ana gari lake lakini mwanamke alianza jeuri. Je mchawi wa wanawake ni magari? Karibuni tujadili.
d42bbb7d2ff5a438ab21f1fce084b7d4.jpg
 
Chezea wanawake wewe, kuna mke wa jamaa yangu alinunua kisuzuki kidogo (nimekisahau jina) ila alivyokuwa anamletea mme wake nyodo ni hatari
Mkuu hujanijibu sasa wakati anamletea mme wake nyodo...huyo Mme wake alikuwa anausafiri au hana kabisa?
Kama alikuwa nao ni wa aina gani?usikute alikuwa hana usafiri...
 
Back
Top Bottom