Michelle
JF-Expert Member
- Nov 16, 2010
- 7,621
- 3,514
Siku hizi naona kupewa gari na wanaume imekuwa issue kubwa.......kiasi kwamba kuna wakati hoja inajadiliwa mtu labda ana tatizo...mtu anaweka comment za ajabu kwamba wasichana wa siku hizi mnafuata hela na mnadanganywa na magari sijui nyumba na vitu kama hivyo.........ndo maana mnateseka............Au mtu umepata mwanaume mwenye uwezo watu wanakukatisha tamaa,mara hawajatulia,atakudharau mara sijui nini.......
Na wasichana tumekuwa tukijaribu kubisha hilo au kusema si wote.........
Nafikiri wote tunapenda maisha mazuri,hayaletwi na hela bali hela ni sehemu tu ya kuwa na maisha bora na yenye furaha.....
Nikiangalia dunia ya sasa,na hasa jamii inayonizunguka siioni tofauti ya kimatendo na kimaadili ya mwanaume mwenye hela na maskini......wanaume asilimia kubwa ni waongo na wanatoka nje ya ndoa na wengine wanashindwa hata kutimiza wajibu wao kama baba na kama mume.........mimi siamini kwamba ukiwa na hela kiasi au usipokuwa nazo inakufanya wewe uwe mwema sana au mwenye upendo wa kweli....
Nafikiri maisha ni kuchagua na bahati, mwanamke ukipata mwanaume mwenye hela nyingi manake hata mwenye mia mbili atasema anazo.... kama UNAMPENDA, mchunguze, chukua muda tafuta ufahamu wa kile anachokifanya kumpatia kipato...... ukimuona anakufaa nenda,ishi maisha yako,Sali,lea watoto wako na kuwa mvumilivu,zaidi jitahidi kuwa wa manufaa kwa jamii yako na wenye shida.
Ukiwezeshwa nawe kaza buti,jijenge,fanya kazi usiwe tegemezi.......na zaidi kuwa msaada kwa mumeo na furaha yake ili aendelee kufanikiwa zaidi na zaidi mkumbushe kuwasaidia wasio na uwezo.
Na wasichana tumekuwa tukijaribu kubisha hilo au kusema si wote.........
Nafikiri wote tunapenda maisha mazuri,hayaletwi na hela bali hela ni sehemu tu ya kuwa na maisha bora na yenye furaha.....
Nikiangalia dunia ya sasa,na hasa jamii inayonizunguka siioni tofauti ya kimatendo na kimaadili ya mwanaume mwenye hela na maskini......wanaume asilimia kubwa ni waongo na wanatoka nje ya ndoa na wengine wanashindwa hata kutimiza wajibu wao kama baba na kama mume.........mimi siamini kwamba ukiwa na hela kiasi au usipokuwa nazo inakufanya wewe uwe mwema sana au mwenye upendo wa kweli....
Nafikiri maisha ni kuchagua na bahati, mwanamke ukipata mwanaume mwenye hela nyingi manake hata mwenye mia mbili atasema anazo.... kama UNAMPENDA, mchunguze, chukua muda tafuta ufahamu wa kile anachokifanya kumpatia kipato...... ukimuona anakufaa nenda,ishi maisha yako,Sali,lea watoto wako na kuwa mvumilivu,zaidi jitahidi kuwa wa manufaa kwa jamii yako na wenye shida.
Ukiwezeshwa nawe kaza buti,jijenge,fanya kazi usiwe tegemezi.......na zaidi kuwa msaada kwa mumeo na furaha yake ili aendelee kufanikiwa zaidi na zaidi mkumbushe kuwasaidia wasio na uwezo.