Sumba-Wanga
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 5,349
- 1,224
Wana JF, hebu nisaidieni. Kwa nini wanawake wengi huwa tunakawaida ya kuwanunia/kuwasusia wanaume/marafiki zetu? au ndio dalili ya mapenzi? Hii hata kwenye cinema utaiona sana, mwanamke anajifanya kununa/kususa na kuja na mkiwara mingi kama anataka kitu kwa mwanaume! Akikipata, basi utaona anacheka, anaona raha kubembelezwa kama mtoto!
Mbaya zaidi kwenye ndoa, hasa wa wale wenzangu wasiopenda kuambiwa ukweli, wale wanaojiona kuwa kila wakati wako sawa, basi wakirekebishwa/au kushauriwa na waume zao utawakuta wamevuta midomo hao! Kisa mwanaume hamsikilizi na kwa wanawake wengine, ni kama vile hawapendwi! mmh jamani hapo huwa nakwama, kwani mwanaume kukupenda ni yeye kukubakli kila unalosema wewe na akiwa tofauti basi umenuna? Mmh .....
Mbaya zaidi kwenye ndoa, hasa wa wale wenzangu wasiopenda kuambiwa ukweli, wale wanaojiona kuwa kila wakati wako sawa, basi wakirekebishwa/au kushauriwa na waume zao utawakuta wamevuta midomo hao! Kisa mwanaume hamsikilizi na kwa wanawake wengine, ni kama vile hawapendwi! mmh jamani hapo huwa nakwama, kwani mwanaume kukupenda ni yeye kukubakli kila unalosema wewe na akiwa tofauti basi umenuna? Mmh .....