Wanawake muwe na huruma jamani

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,150
KATIKA hali isiyo ya kawaida mtandao huu ulishuhudia mwanamke mmoja akilia kwa machungu baada ya kushuhudia mwanandoa wake akibebwa na moja ya mashangingi ya mtaa huo.
Dada huyo alikadiria kuwa na umri kati ya miaka 25 hadi 26 aliangua kilio cha nguvu na kushindwa kujizuia baada ya kushuhudia mume wake kipenzi akiondoka na shangingi hilo.

Tukio hilo la aina yake lilkitokea jana majira ya saa 11:45 jioni, katika maeneo ya Kinondoni Manyanya baada ya shangingi hilo kufika nyumbani kwa dada huyo na kuondoka na mume wake.

Mtandao huu ulishuhudia tukio hilo na kukuta dada huyo akilia na watu kujaa mtaani baada ya kuangua kilio cha nguvu ambapo kilivutia watu wengi na kujaa eneo hilo.

Mtandao huu ulijaribu kuwahoji watu wawili watatu ambao ni majirani na mwanamke huyo walidai kuwa alikuwa akilia kwa kuwa ameshuhudia mume wake akiondoka na shangingi moja maarufu mtaani hapo jambo ambalo amefanya aamini alilokuwa akiambiwa na majirani zake.

“Ujue dada, huyu analia kwa machungu kwa kuwa mume wake ametekwa na shangingi moja la hapa mtaani ambalo kazi yake ni kuchukua waume za watu, na tulikuwa tunamueleza alikuwa hatuamini sasa leo kashuhuda mwenyewe’ ndio mana analia hivyo” walisema

Ilidaiwa kuwa mume wa dada huyo ni kijana naye anayekadiriwa kuwa na miaka 28 hadi 30 alitekwa kimapenzi na mama huyo ambapo ilidaiwa alikuwa akimsaidia katika mambo mengi ya kimaisha na kumpa pesa na kijana huyo kunogewa na huyo mama anayekadiriwa kuwa na miaka 40 hadi 45.

Ilidaiwa kuwa kijana huyo kabla ya kutekwa na jimama hilo alikuwa akijishughulisha na biashara ndogondogo akiuza viatu vya mitumba kupitisha mitaani.

Alipoona amepiga hatua moja alikwenda kijijini kwao Iringa na kwenda kuoa na kurudi na mke wake huyo ambaye alishakuwa amezaa nae mtoto mmoja wa kiume ambaye ana umri wa miezi 11 sasa.

Majirani hao walidai kuwa kijana huyo alianza kubadilika tabia na pia akibadilisha biashara na kufungua mabanda ya biashara sehemu mbalimbali ikiwemo kariakoo na kinondoni.

Majirani waliposhtukia kuwa shangingi hilo maarufu ndilo linalomtunza kijana huyo walimtonya mkewe ambaye hakuamini na hakutaka kusikia stori hizo.

Siku ya tukio jimama hilo alifika nyumbani kwa kijana huyo na gari yake aina ya Toyota RAV 4 na kupiga mlio ulioashiria yuko nje ya nyumba hiyo na kijana huyo alitoka nje na kupanda garini na kuondoka naye.
 
wanawake wengi sana hasa wasomi hapa bongo hawana wanaume, tujiulize, wanakaa hivihivi? kule mbezi beach africana kuna jimama moja mwanasheria, ana jumba la kufa mtu, lakini jumba lote anakaa peke yake, huwezi amini. mama mwenyewe si kwamba ni mzee sana, miaka kama hamsini tu. cha kujiuliza, nyumba yoote hii anakaa peke yake? kumbe ndo tabia zao, kuchukua damu za motomoto ndo wanavyoita, na ukimwi wa motomoto, na laana za motomoto. mwogopeni Mungu wajameni.
 
Trend ya Maisha inabadirika sasa hivi, tulizoea kuona wanaume ndo wanaowalea wanawake tu, sasa hivi si one way traffic tena, wanawake nao wapo kwenye kulea wanaume.Juzi jpili kaja dada mmoja hivi ni meneja sijui kwenye shirika flani la wakimbizi wana ofisi hapa Dar, ana takriban 38yrs maka 40. Sijajua bado background yake lkn alikuwa na mchumba wake, huyu mchumba ni kijana wa miaka kama 26-28, alikuwa anaishi Mwanza, lkn wote ni watu wa MOSHI (CHagga). Huyu kijana background yake si nzuri sana ingawa mzazi wake ni mtu aliyekwenda shule lkn alioa mwanamke ambaye hakwenda shule na malezi ya watoto hayakuwa mazuri sana. Huyu kijana alikuwa anaishi Mwanza na kaka yake, shughuli aliyokuwa akiifanya si nzuri sana, alikuwa mtu wa kupuliza sana Dope (bangi) kupora watu nk. Ikafika kipindi akaokoka akawa anajifunza uchungaji pale Moshi, Ndipo alipokutana na huyu dada ambaye na yeye ni mwokovu(KAMA KWELI). Huyu dada yupo desparate kuolewa na huyo kijana, kamleta Dar anamhudumia kila kitu. Kijana kamwambia yule dada hana pesa za kufanyia harusi dada kapenyeza rupia kampa jamaa millioni 5, ili asionekane hana kitu na sasa kampangishia chumba cha elfu arobaini kwa mwezi pale sinza. Dada kwa kweli amependa kila kijana anachotaka kitafanywa, wasi wasi wangu ni kwamba huenda huyu dada atakuja lia sababu kijana anaonekana kishaona mwanya wa kupata pesa, jana walinipigia simu dada anatafuta nyumba ya kununua kwa 50M, kampa kazi kijana ya kutafuta nyumba, dogo anasema yeye si mzoefu hapa dar, akaniuliza mie wapi house zinapatikana, nikamwambia atulie lkn hakuridhika akasema kwa nini nisimshawishi huyo dada hiyo 50M aiweke kwenye account ya jamaa ili iwe rahisi kununua nyumba pindi ipatikanapo? nikaona mmmh segerea inanukia hapa, nikamwambia awe mpole haya mambo hayahitaji haraka kiasi hicho. Dogo aliacha pombe kwa muda wakati anajifunza uchungaji, sasa hivi yupo town namuona kaanza kulamba Konyagi upyaaaaa na anajificha mchumba wake asigundue. Kule alikokuwa anajifunza uchungaji tayari kanisa limemtenga coz yule dada anataka ndoa iwe mwezi wa saba mwaka huu yaani miezi mitano tu toka wamekutana, wakati Mchungaji alimwambia amchunguze vizuri yule dada na si kuparamia tu, atakuja juta, lkn dogo jeuri ya pesa ya dada imemtia kiwewe, na yeye hasikii wala haambiwi. Nadhani mwanamke na yeye ana preferance zake ni uchumi tu ndo unawabana lkn wangekuwa na uwezo wa kutosha nadhani wangeweza jichagulia mume wnanayemtaka na muda vile vile wa kuolewa au wengine wasingependa kabisa hizi ndoa NDOANO za siku hizi, na wengine wange zaa tu na wanaume ili mradi awe na watoto basi, saa hivi ndicho kinachotokea, wanaanza kuwa na uwezo kwa hiyo wanachagua kipenda roho hata kama kijana ni mdogo ili mradi kampenda na kwenye malovee ana mkuna sawa sawa!!!!!!!!!!!! basi huyo ndo chaguo lake
 
Back
Top Bottom