Wanawake mlioolewa piteni hapa

Wanawake mlioolewa piteni hapa

Murete

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2016
Posts
246
Reaction score
102
Salaam mama zangu, dada zangu, wenzangu na wadogo zangu!
Tumshukuru Mungu kwa kuiona tena siku hii.

Nimerudi na uzii huu nia yangu ni kupata uzoefu (experience) kutoka kwenu kuhusiana na maswala ya ndoa baada ya kuolewa. Kwanza nianze kwa kuwapongeza wote mlio kwenye ndoa zenu. Wale ambao ndoa zimeisha kwa uwazi au kificho niwape pole. Naamini JF MMU ni kisima cha mawazo mapana na ya hekima. Hapa naomba mnipe hekima zenu ambazo zinaweza kuelemisha pia wadada wenzangu wanaotarajia kuolewa. Ni dhahiri ya kwamba mwanamke anaweza kuolewa akiamua tu.

Sasa natatizwa na mambo muhimu na ningependa kusikia kutoka kwenu. Je, maisha yanakuwaje ukiolewa na:-

1. Mwanaume uliyempenda kwa dhati
2. Mwanaume usiyempenda ila yeye alikupenda
3. Mwanaume mliyependana toka urafiki na uchumba
4. Mwanaume asiyekupenda ila akakuoa kwa sababu ya mimba, familia n.k
5. Mwanaume kwa sababu ya mali.

Kwenye jamii yetu haya yanatokea sana na kuna madhara na faida zake baada ya ndoa. Tafadhali hebu tupeni uzoefu wa mahusiano huko ndani ya ndoa yanakuwaje kutokana na aina ya ndoa. Wengine mtauliza kwanini nauliza kuolewa na mwanaume ila siku hizi kuna ndoa za jinsia moja.

Wanaume mnaweza kuchangia pia, tungependa kusikia toka kwenu. Ili uzi huu uwaelimishe wadada wanaotegemea kuingia kwenye ndoa sitegemei kejeli, dharau na matusi. Hapa kila mtu yuko nyuma ya computer, hakuna anayejua nani anaandika kwa hio maoni yako halisi ni muhimu kwa kujifunza. Tafadhali tupeane maoni ya kweli (genuine) kwenye swala hili.

Karibuni tuchangie. Asanteni
 
Mwanaume uliyempenda kwa kwa dhati, posibillity ya kukuumiza ni kubwa, nature yetu binadamu anaekupenda unaishia kumtesa tu

Mwanaume usie mpenda afu ye anakupenda atleast, hapo upendo guaranteed ukiamua kumpenda pia you will enjoy

Mliependana tangu urafiki hapo ndo penyewe

Mwanaume aliekuoa kwa sababu ya mimba au familia tegemea kuishi kwenye ndoa hewa

Nb: ndoa haina formula
 
Asante kwa mchango wako bibie Evelyn Salt
 
Yeyote tuu poa mtajuana mbele kwa mbele. Ni wangapi wanakuja kama malaika ila mkishaingia hapo ndani wanageuka kuwa Nyegere!!
 
Ni bora nikupende mimi basi,wew sina sababu ya kutaka unipende hapo ndio ntakuoa.
 
Asante Lavanda. Na je, maisha yanakuwaje ukiwa na mwanake asiyekupenda? Je, una uhakika gani kwamba atakupenda baada ya kuoa?
 
kumbuka hakuna mwanadamu mwenye tabia ya kudumu, hivyo ndoa haina formular, kuna mambo mengi yanaathiri ndoa ikiwemo mazingira uwezo wa kipato tamaa za aina ya maisha, matarajio ya baada ya ndoa vyote hivyo husababisha ndoa zikawa na mafanikioa ama kinyume chake.
 
Jamani jamani uzi unawakaribisha wanawake waliyo olewa wanaume wanatafuta nini? Na msio olewa hapa pita hivi...
 
Mwanaume kunipenda mm ni criteria ya kwanza, na mm nikimpenda basi ni wonderful. Lakini hata kama sina mapenzi nae but i should atleast be attracted with him, with time i'm sure i can learn to love him. Lakini kama hanipendi hata kama mm nampenda siwezi olewa nae na kikubwa zaidi siwezi olewa na mtu just because i'm pregnant! So he has to love be in love with me period, i won't have it any other way.
 
Mwanaume anaekupenda kwa dhati ndo mzuri wa kuolewa nae hata Kama mwanzoni hujampenda mbeleni utampenda tu maana sisi wanawake ni rahisi kufundishwa kupenda ila mwanaume huwezi kumfundisha Kama hakupendi ni hakupendi huna utakalo fanya kubwa umfanye akupende.

Mwanaume uliyempenda sana kuna uwezekano mkubwa asiwe amekupenda huyu kaa nae mbali atakutesa tu.
Kuolewa kwa sababu ya ujauzito au mali sio kitu kizuri kabisa mtu awe ameweka nia ya kukuoa mwenyewe.

Ila hili lalamiko la kuwa tunabadilika tukishaolewa naona linakuwa kwa kasi tunatakiwa tuwe halisi kipindi chote cha mahusiano mpaka ndoa ili mwanaume ajue yupo na mwanamke wa aina gani maana tunaharibu ndoa zetu wenyewe.
 
Mwanaume kunipenda mm ni criteria ya kwanza, na mm nikimpenda basi ni wonderful. Lakini hata kama sina mapenzi nae but i should atleast be attracted with him, with time i'm sure i can learn to love him. Lakini kama hanipendi hata kama mm nampenda siwezi olewa nae na kikubwa zaidi siwezi olewa na mtu just because i'm pregnant! So he has to love be in love with me period, i won't have it any other way.
Very good my dear we are standing on the same ground
 
Mwanamme aliumbiwa kupenda ndo maana hata maandiko Matakatifu yanasema " mwanamme ampende mkewe kama aipendavyo nafc yake" soo kuolewa na mwanamme asiyekupenda ni sawa na kusubiria ndege bandarini..!! Something that is very impossible
 
Uzur mwanamke akupende bhana hiyo ndoa tam sana hamna kuzunguana hapo,mi wanawake mungine akijua unampenda atakutesa sana,mungu ni mwema wanawake mpo wengi sana ukipata wa kukupenda shukuru sana ukichangia na haka ka hali hatareee
 
Maoni mazuri. Nakaribisha pia michango kutoka kwa wanaume. Swala la ndoa ni la me na ke. Karibuni mtoe mawazo
 
Tatizo lipo kwenye familia kila ufanyalo utaonekana unamnyanyasa, hata ukichelewa kurudi tuu watasema umeenza.
 
Tatizo ni pale anapogundua unampenda zaidi daaah! utateseka sana, bora tu niwe sieleweki.
 
Kumbe umeshaolewa nilijua upo single.
Hahahaha.......mkuu nitake radhi kwanza naona umeamua kunizalilisha kwa kiwango kikubwa sana.

Mimi ni dume bana, mwenye mada ameturuhusu madume pia tuchangie au umesoma kichwa cha habari tu
 
Back
Top Bottom