Wanawake jitahidini kutoweka wazi shida zenu mapema mnapoingia kwenye penzi jipya

Daydream

Member
Oct 26, 2023
58
328
Nakumbuka niliwahi kuingia kwenye mahusiano na binti mmoja wa ki Arusha ambae tulijuana kupitia social media, yeye alikua Arusha na mimi nilikuwa Dar es Salaam.

Huyu binti kwanza alikuwa ananikera kitu kimoja, anapenda sana video call sasa sijui alikuwa anataka kugundua nini.

Ingawa nilikuwa sipendi lakini nikaona anyway kwakuwa ndo tumeanza mahusiano wacha nimridhishe

Hali hiyo haikunisumbua sana maana nikajua kadri tutakavyozoeana nitamueleza ukweli kwamba mimi sio mpenzi sana wa video call.

Tulipanga kuonana na nilimuahidi kwamba ningeenda Arusha kuonana nae.

Huyu binti alinivunja moyo kitu kimoja, kabla hata sijaenda kuonana nae kwa mara ya kwanza akanipiga mzinga wa 80k akidai kioo cha simu yake kimepasuka hivyo anataka akakibadilishe.

Alivyonambia hivyo tu nikaona hapa hamna mtu, yaani hata kuonana physically kwa mara ya kwanza bado hatujaonana lakini nishapewa invoice ya 80k wakati yeye mwenyewe anafanya kazi na ana kipato.

Nilikuwa na uwezo wa kumpa ile hela lakini niliona mbona mapema sana kashaanza kuleta matatizo yake it means yupo after something.

Huyu binti nilimkatia mawasiliano 100% maana niliona hana tofauti na Golddigger na safari yenyewe nilii cancel.

Ni kweli wanawake mnahitaji kuhudumiwa na wanaume ila jitahidini kuficha shida zenu mwanzoni tu mwa mahusiano maana mtajikuta watu wanapiga kisha wanatembea yaani ni kama vile kununua malaya Riverside kisha kila mtu anachukua hamsini zake.
 
Mimi katika kumuwimba kimasihara mpangaji mwenzangu akaanza kunipa virungu vidogo kabla hata ya kuwekana sawa. Nilikuwa naweza kumpa hata mara kumi yake ila nikaona nitaingia mkataba wa kibandari....zoezi nililifuta.
 
Sasa we mwenyewe hujishangai maelezo yako, unaoneka wazi umekurupuka kujibu.

Familia na uchumba ni vitu viwili tofauti, kama angekua ni mke nisingelalamika mana tayari ni mke sasa sasa nahudumiaje mchumba ambae hata penzi lake sijalionja.

Tumia akili boya wewe
 
Aliona bora akuombe mapema kabla ya wewe kumuomba😂😂 yani ni full kuombana uzuri yeye mjanja kakuwahi😅
Sasa ulitaka uende ukamnanii bure bure tu ukizingatia hamkai karibu😂😂😂
Sio kwamba nisingemuachia pocket money, pesa kdg lazima ningemuachia ila alipaswa baada ya kuonana ndo aanze at least kusema shida yake.Binafsi siwezi kukutana na mwanamke halafu nisimpe chochote sema alianza kunililia shida kabla hata ya kuonana napata mashaka mana najua litakua penzi la invoice daily.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…