EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Yaani alimwonyesha mdada mapenzi hasa kumbe hayakuwa mapenzi bali utapeli, alimpa mdada milioni moja ya kufanya shopping. Baada ya muda ndo yeye akaja na gia ya kusema mzigo umekwama na hahui afanye nini? Eti dada tu ndo mtu wake anamhesabu kama mama wa watoto wake, halafu anavyoongeaga kwa upole kaka yule, hata sisi marafiki hatukutegemea. Kweli tumepata somo.
Hapo kwa mwanamke wenye akili angemshtukia. Mmekutana miezi mitatu. Ndani ya miezi mitatu anakupa milioni moja ya shopping. Ndani ya miezi mitatu hiyo hiyo anakuomba mkopo wa milioni sita. Halafu hapo mtu unakopesha tuu bila hata kufikiria mara mbili. Ina maana hata kabla ya kumkopesha hakuomba ushari kwenu nyie mashosti wake? Au aliomba ushauri na nyie mkaushari amkopeshe? Role ya mashosti iko wapi hapa? Mwanamke yoyote anayesoma hii post ajiweke kwenye mazingira ya huyo mwanamke. Je Ungekopesha?