Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Matatizo ya kuamini mtu haraka....jamani miezi mitatu ya mapenzi unamkubalia ombi kubwa kiasi hicho? Na umefunguka mapema sana yaelekea binti alitoa siri \zake zote kuwa ana uwezo wa kupata huo mtaji au mkaka alikuwa anamlia timing..................................duh kweli kuna haja ya kumshirikisha MUNGU katika kuchagua wenzi wetu!!
wangechukua hamsini ingekuwa vizuri,millioni sita?? Wanaume wengine jamani!!! kweli wanatisha....nafurahi haya maneno yanapotoka kwa mwanaume....Bwana Yesu Rudi tu!!!
wow....u aint ma bitch nigger.....dah
walahi apo utataman uwe mchawi um....
Mkuu sio viherehere, kushikwa na penzi ndo kunasababisha haya. Iko siku deni litaisha, na huyo mhuni hatafika popote na udhulumaji wake.
mkome na nyie..ndo maana hata JK anawaambia mna viherehere...
OMG................6 milllion,mwanaume wa miezi mitatu???? tena unamchukulia mkopo kazini?? ni mume au baba wa watoto wake???
Kweli maisha ni shule ngumu sana....naomba umpe pole,kupitia yeye na sisi tunazidi kujifunza kuhusu viumbe wazito hawa....hakuna haja ya kulipiza ubaya,manake huyu mwanaume ni jambazi,ana roho isiyoshindwa ubaya wowote.....atulie,avumilie,milioni sita inalipika...akumbatie tu kazi yake sasa.....zaidi,Mwenyenzi Mungu namuomba ampe nguvu,hekima na akili katika kukabiliana na haya yaliyomkuta.....!!!God Forbid!!
Hapo Kaka mpendwa umenena(Nowadys mabinti/wasichana/wanawake hawajali utu wao.Utu, thamani ya mwanamke iko katikati ya miguu yetu jamani,kabla ya kutenda tufikiri kwa kutumia vichwa na sio hisia).Hata mimi sioni haja ya kulaumu wanaume wakati wote,au kulaumu wanaume kila wakati.Kwani wanatubaka?Na kama umeamua kutenda la ndoa kabla ya ndoa kama ambavyo wengi wanafanya then kuwa makini kabla ya kufanya maamuzi yoyote yale yanayohusiana na sekta hiyo.Bado sijaona Logic ya hilo tukio hadi kupelekea kuhusisha wanaume wote.. Huyo jamaa amepewa nafasi na yeye ameitumia kulingana na roho yake mbaya, na ujambazi wake..
Hii ni sawa sawa na kusema wanaume wote ni vibaka au majambazi kwa sababu tu, siku zote wanaofanya na kukamatwa kwenye hayo matukio ni wanaume.
Wakati mwingine ninamu-admire Miss Judith kwa kauli zake za kuwavulia nguo wanaume kabla ya ndoa..Kama umefikia nafasi ya kumpa mwili wako auchezee, sio vigumu kukopa na kumtafutia pesa. (kwani pesa ina thamani gani kama mwili wako)..Aende tu kwenye vituo vya polisi watamsaidia kumtafuta huyo jamaa
Kipenda roho Michelle!!.......Si unasikia jamaa alionyesha mapenzi moto moto "jamaa kuonyesha mapenzi mazito haswa mpaka wenzake wakawa wanaona mamsapu kapata bwana wa ukweli" akadhani amepata kumbe amepatikana! Hakuna mapenzi yoyoye ni TAPELI TU!
Hapo Kaka mpendwa umenena(Nowadys mabinti/wasichana/wanawake hawajali utu wao.Utu, thamani ya mwanamke iko katikati ya miguu yetu jamani,kabla ya kutenda tufikiri kwa kutumia vichwa na sio hisia).Hata mimi sioni haja ya kulaumu wanaume wakati wote,au kulaumu wanaume kila wakati.Kwani wanatubaka?Na kama umeamua kutenda la ndoa kabla ya ndoa kama ambavyo wengi wanafanya then kuwa makini kabla ya kufanya maamuzi yoyote yale yanayohusiana na sekta hiyo.
Habari za mchana wana jamvi.
Hebu sikilizeni kisa hiki, huwa nina ki-grocery changu, sasa hapa huwa nina mashoga zangu kibao, kila mtu anakuja na la kwakwe kuhusu kutendwa, mengine naona ya kawaida lakini hili jamani!!!!! Limenichosha nimeona niwashirikishe.
Huyu shoga yangu kaja hapa mchana huu analia. Kuna jamaa alijifanya anampenda kwa dhati ya moyo wake, katika kukaa, kaa kwenye hilo penzi lao kwa takribani miezi mitatu kwa jamaa kuonyesha mapenzi mazito haswa mpaka wenzake wakawa wanaona mamsapu kapata bwana wa ukweli. Kumbe jamaa alikuwa na yake kichwani, kamdanganya dada wa watu, eti kuna biashara huwa anafanya lakini amekwama, hivyo anamwomba mdada amkopeshe shilingi 6m. Mdada hakuwa nazo, jamaa akamwambia kwa sababu umeajiriwa naomba unikopee ofisini kwako nitakuwa nikirudisha kidogo, kidogo, mdada wa watu kakopa kampa jamaa. Jamaa baada ya kushika kitita mkononi, kidogo kidogo mapenzi yakaanza kupungua na mwisho yakaisha kabisa, kwani hivi sasa dada akimpigia simu hapokei, akipokea akiulizwa mbona siku hizi hauonekani anasema yuko bize. Mdada si akaamua kujitoa fahamu kumfuata huko nyumbani kwake, akakuta jamaa full shangwe na mwanamke mwingine na deni yeye anaendelea kukatwa kwenye mshahara wake kila mwisho wa mwezi. Mwanaume hajajali kuwa kafumaniwa wala nini? Sana sana alimuuliza unashida gani, binti akamwambia inakuwaje leo hii unaniuliza nimefuata nini wakati mimi ni mpenzi wako jamaa akamwambia una kichaa na maneno mengine mengi ambayo siwezi hata kuendelea kuyaandika. Wanaume jamani, jamani mbona mnatutenda vibaya, vibaya hivi why? Kwanini?
Duh! inasikitisha sana kusema kweli...Ya nini kwenda kumuingiza mwenzio deni kubwa namna hiyo!? Kama ana ushahidi wa kumpa pesa hizo basi afikirie kumpandisha kizimbani. Wanaume wengine jamani Mhhhhh! Wanatisha! Kama penzi hakuna si bora uchukue hamsini zako tu kuliko kumtia hasara kubwa mdada wa watu!!!