Wiyelele kama wanaokusumbua ni jamaa zako- waambie ukweli tu.
Binafsi napenda sana kutoa lift hasa asubuhi , ni jambo jema kushiriki ulichonancho na wengine. Ila iwe unplanned, kama unatoka na unaona jirani wanaelekea kituoni si vibaya ukiwapa tafu kwenda nao job au town.
But the other side of the coin ni binadamu tuna tabia ya kujisahau sana kama incidents zifuatazo:
1)Kuna jamaa nilikuwa nampa lifti nikiwa naenda job, basi akawa amezoea ile mida- baada ya siku kadhaa kila nikitoka getini namkuta hapo nje ya geti ananisubiri nitoke. Basi baada ya siku kadhaa tena , akawa anagonga kabisa geti kama saa kumi na mbili , ili aingie asubirie kwa ndani. Ikatokea siku moja siendi kazini basi kama kawaida kagonga na kwa kuwa ni jirani dada wa kazi kamfungulia , akakaa barazani - muda umepita mi nimejilalia zangu. Mara nasikia mtoto anagonga chumbani, ooh kuna mgeni, kutoka ndio yule jamaa wa lifti. Basi nikamwambia leo siendi job, duh jamaa bila aibu akaniuliza "mbona hujanipigia simu kuwa huendi?". Basi nikamwambia mimi huwa sina ratiba maalumu wewe uwe unaenda kituoni nikikukuta sawa, else consider am not around.
2) Niliwahi kuwapa watu fulani lifti mara mbili tatu: kila wakipanda mi nina CD yangu ya old music napenda kusikiliza, basi wakiingia tu- wanasema aaah weka BBC bwana tusikie habari. Sasa wewe ulikuwa unatembea tena kimya kimya, kupanda tu kamkweche kangu unadai BBC?
3) Kuna baadhi ya jamaa fulani ikifika mda ya kutoka kazini, text message na simu ooh unatoka sangapi. Na mi bila hiyana nasema. Sasa ikawa wakipanda wanaanza ooh naomba tusimame pale kontena ninunue LUKU , ooh kuna mtu ana bahasha yangu kituoni simama kidogo, mwingine anakuja na rafiki yake. Sasa kweli hapa utasema ustaarabu upo?
4) Siku moja niliwaambia watu walioniomba lifti jioni kuwa leo napitia maduka fulani ya ujenzi: bila aibu wakasema aah haina shida kwani utachukua muda. Basi kufika lile duka wakawa hawana stock inabidi niende kwenye godown yake ingine. Ikawa embarassment maana ilibidi niwaambie safari imebadilika na siendi home.
5) Huyu mmoja namsamehe maana hata mimi yanaweza nikuta, nimempa lifti na mtoto akawa amesahau kadi ya hospital, so akaomba turudi all the way apick kadi. Kurudi kafoleni kakawa kameanza, baada ya kama dakika 20 hivi mtoto wa around 3 yrs akadai kujisaidia basi ikabidi tupaki ashuke na ajisaidie.
Wito wangu mimi ni: kama jamii kusaidiana ni muhimu. Si vyema kwa mwenye gari kuwa mchoyo. We werent born with anything. Kuna vitu vidogo unaweza mezea (no one is perfect). Ila na kwa wapewa lift , chonde chonde usizoee kiasi cha kuwa dikteta sana. Kwenye kila jambo kuwe na mipaka.