Wiyelelee
JF-Expert Member
- Nov 9, 2012
- 1,071
- 348
Napata shida sana na hili. Wote tunafahamu kwamba jiji la Salidalama lina tatizo la usafiri na pengine kumsaidia mtu ni kitu cha kawaida kama anakwenda kazini. Lakini cha ajabu, kuna baadhi ya wanaume ambao wanafanya kazi. Kila siku unamkuta mtu amesimama mbali na kituo cha daladala utafikiri anasubiri gari la ofsini kwao kumbe sio. Kila akipita mtu unakuta kazi ni kuchungulia kwenye vioo vya gari na kupiga mkono kama trafik. Ukiwa job anapiga unatoka saa ngapi ili apande tena wakati wa kurudi home.
Jamani kwa nini wanaume tunajifedhehesha hivi? Mtu anakupa lift maramoja na pale ambapo kweli kuna shida ya usafiri na wewe, jaribu kukaa hapo kwenye kituo cha mabasi na wenzako. Wanaume tusipende sana kudandia lift maana ni fedheha. Mambo haya yalikuwa kwa wanawake zamani lakini siku hizi yamehamia kwa wanaume!
Najua wengi wataponda lakini ukweli ndo huo! Mi na mke wangu hatukuwahi kudandia lift ya mtu, tulikwa sisi na daladala kila siku! Hata kama gari imeleta tatizo tulikuwa tunawahi kupanda daladala. Iweje wasio na magari wapende sana lift utafikiri shida hawana?
Jamani kwa nini wanaume tunajifedhehesha hivi? Mtu anakupa lift maramoja na pale ambapo kweli kuna shida ya usafiri na wewe, jaribu kukaa hapo kwenye kituo cha mabasi na wenzako. Wanaume tusipende sana kudandia lift maana ni fedheha. Mambo haya yalikuwa kwa wanawake zamani lakini siku hizi yamehamia kwa wanaume!
Najua wengi wataponda lakini ukweli ndo huo! Mi na mke wangu hatukuwahi kudandia lift ya mtu, tulikwa sisi na daladala kila siku! Hata kama gari imeleta tatizo tulikuwa tunawahi kupanda daladala. Iweje wasio na magari wapende sana lift utafikiri shida hawana?