Mie King'asti umenielewa vizuri sana. Nami nimekusoma kabisaaa comments zakoKwa hiyo mkeo akikuletea chai kitandani unamuona kama roboti? (Najiulizisha tu manake kwa mtazamo wako sidhani kama hata tei tei unafuliwa wewe ). Nimesema toka mwanzo, shida ni malezi. Mie niliyedekezwa na babangu Mtambuzi, nikitoka shule nasimulia hadi peni ilipogoma kuandika ananiambia pole chukua hii yangu. Ungenipa shida tu wewe.
Mkeo nae anagangamala. Kwani ukimuambia pole mpenzi utapungukiwa sh ngapi? By the way, mwanaume unatakiwa kudekea mkeo tu. Mwenza wangu akiwa na stress na asiniambie, ugomvi wake sijui Mungu asimamie kwa mlangoni?
Muache si anajidai kamanda? Mapenzi yamehamishiwa instagram yeye hajui anapambana na wahindi alete hela nyumbani? Hehehe kweli dunia hadaa. Take what you give.
Teh sista, kabega tu pole mara sita?
Kudeka sawa lakini nyie bhana mmezidi kwa kweli, wajua ukideka sana mtu hawezi jua kama kweli waumwa au ndio kama kawaida yako..
Afu kwa nini wanawake hupenda sana kutumia dawa?.
Lol huna mkojo au huna usingizi...? Stress za mitandaoni hizi lol ebu nipishe mie
Koma mwenyewe kama topic inakuboa kakojoe ukalale mfyuuuuuu
Kasema komaa na si koma??? povu la nini sasa?
bora Huyo asiyejali ugonjwa kuliko asiyejali genye....
Lol sasa kama unamjua mtu wako si mara moja moja umpulize basi yaishe, atafurahi atalala. Sio kila siku mpera mpera tuUnakuta mtu akijikata kiwembe tu basi anataka siku nzima watu wasimamishe shughuli za kulijenga taifa kwa ajili yake yeye...anataka kuona watu wamemzunguka kitandani huku wakikipuliza kidole alichojikata.....hahahaaaa..
Hivi inawezekana akawa anajali genye halafu kwenye ugonjwa akawa hajali???
Mtumishi mambo. Sasa mtumishi kudeka sawa kuna watu wanatabia ya kudeka lakini kama mtu sio kawaida yake u cant assume akiumwa ni kudeka. Sio kuumwa tu hata stress zingine za kimaisha. Kwanza mpenzio asipokudekea wewe akamdekee nani? Ndo utakuta shamba boy yeye ana care zaidi ya mpenzi wako. Maana ukiamka asubuhi utasikia shkamoo mama, mbona leo unaonekana hauko sawa? Mpenzi wako mwenyewe hata kuku notice haja notice! Hata office mate sometimes utakuta akikuona tu anakuuliza upo sawa leo? Mpenzi ndo kwanzaaaa hana habareee...
Lol sasa kama unamjua mtu wako si mara moja moja umpulize basi yaishe, atafurahi atalala. Sio kila siku mpera mpera tu
Baadhi ya wanaume wabinafsi saaaana
Tena hawa wenzetu wakiugua utafikiri roho inakaribia kutoka . Lkn wanaume wasiojali ni vizuri wajifunze sio kusingizia sijui mtu akipendwa anadeka haifai.Unaona sasa, mtoa mada analalama kuwa akisema anaumwa haulizwi unaumwa nini. Hapa communication skills ndio issue. Hata sie uko kazini unapigiwa simu na dada anakuambia mtoto analia sana. Unauliza umempa chakula saa ngapi? Ulibadilisha diaper saa ngapi? Hebu iangalie tena. Ulimpa maji ya kunywa? Ana homa? Ametapika? Mwisho wa siku unagundua ana usingizi. Unamuambia lala nae kitandani. Baada ya nusu saa ukipiga simu unaambiwa amelala.
Sasa wewe unaambiwa kuna shida home unakurupuka unaenda. Huulizi una shida gani? Nini kimetokea? Damu imemwagika hadi sakafuni? Unaskia kizunguzungu? Ukionyesha upendo maisha yanakuwa marahisi kuliko unavyodhani. Upendo unarahisisha maisha kaka, jiachie ufurahi.
Hivi watu hatuwezi kuongelea relationship matters mpaka iwe ni mume wako au mpenzi wako?hivi umeshindwa kuongea nae hadi unapost udhaifu wa mume wako humu!:what:π nakushauri uachane nae hakujali.....hakufai....uje kwangu uone ntakavyokujaliππ