Wanaume wa Dar buana...!

Wanaume wa Dar buana...!

Khantwe

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2012
Posts
59,468
Reaction score
119,622
Habari ya weekend wakuu,

Leo bwana kwenye daladala ya huku kwetu gomz kimetokea kisa kimoja.

Aliingia kwenye daladala mama mwenye mtoto na siti ya mbele kabisa karibu na mlangoni alikaa m'baba kwa kumuangalia anaweza kuwa yupo mid/late 40s.

Kando yake alisimama mwanaume mwingine wa makamo yaleyale, basi yule aliyekaa akasimama kumpisha yule mama akae.

Aliposimama akaanza kumwaga povu (kumbe alikuwa ameambiwa na yule aliyesimama kuwa amsaidie mtoto ).

Wacha ateme povu eti ooh wanawake hampendani, mwenzenu anaingia mnashindwa kumpisha kwa sababu gani? Mwenzie akawa anamtuliza, walikuwa hawajamuona si unaona gari imejaa?

Ye kakomaa hamna walikuwa wamemuona wanawake wana roho mbaya sana, yaani hawapendani kabisa.

Kusema kweli yule mama aliyeingia na mtoto mimi sikumuona maana nilikuwa nimejilalia zangu usingizi, na hata ningemuona nisingempisha bali ningempokea mtoto.

Ila yule baba mimi kanishangaza sana, ni kwa nini anadhani sisi wanawake ndio tunatakiwa kupisha?

Kwanza yeye alikuwa jirani kabisa pale kwa hiyo badala ya yeye kupisha alitaka atokee mwanamke aliyekaa nyumba ndio apishe?

Niwaulize ninyi wanaume, hivi akiingia mama mwenye mtoto au mjamzito anayetakiwa kuwa wa kwanza kunyanyuka kwenye siti ni ninyi au sisi?

Yaani sisi tunabeba mimba miezi tisa, tunalea hadi watoto wanafikia umri wa kujitegemea eti inapotokea tupo huru yaani hatuna mimba wala mtoto wa kunyonyesha bado tuna wajibu wa kuwapisha wenzetu walio katika hali hizo?

Kweli leo nimejua kuwa ni shughuli pevu kuzaliwa mwanamke Afrika, nadhani wanawake wa Afrika tuna mbingu yetu spesho maana sio kwa kazi hii tuliyonayo.

Nilitaka nimtolee uvivu yule mwanaume ila nikaamua nikae kimya maana nilikuwa na my uncle mmoja naheshimiana nae na anajua mimi siongeagi kabisa nikaamua kuilinda image yangu
Hebu tuoneeni huruma

NB: Hapa nazungumza na wale ambao huwa wanapisha sio wale makauzu
 
Ni kweli wanawake mna roho mbaya sana hasa nyie kwa nyie hata aibu hamna kabisa

Anakuja mwanamke mwenzenu anamimba hata kiti hampishi mnamtizama kama picha hadi atokee mwanaume amuonee huruma ampishe

Mwanamke ni kiumbe katiri sana
 
Sasa dada unalalamika hyo jamaa kuwaponda wanawake hampendani na hamuwapishi wenzenu viti na wakati wewe mwenyew sshv unawaponda wanaume wa dar! Hapo mnatofauti gani labda? Wote mi naona ndo wale wale tu, mmegeneralize watu wote kwenye kundi moja
 
Kama umeitaja Gomz. Nina uhakika story hii ina asilimia nyingi za ukweli.
 
Sasa dada unalalamika hyo jamaa kuwaponda wanawake hampendani na hamuwapishi wenzao viti na wakati wewe mwenyew sshv unawaponda wanaume wa dar! Hapo mnatofauti gani labda? Wote mi naona ndo wale wale tu, mmegeneralize watu wote kwenye kundi moja
Sijakataa kwenye kupendana au kutopendana, shida ni hapo kwenye kuachiana siti
 
Ni kweli wanawake mna roho mbaya sana hasa nyie kwa nyie hata aibu hamna kabisa

Anakuja mwanamke mwenzenu anamimba hata kiti hampishi mnamtizama kama picha hadi atokee mwanaume amuonee huruma ampishe

Mwanamke ni kiumbe katiri sana
"Katiri" ndio nini?
 
Ni kweli wanawake mna roho mbaya sana hasa nyie kwa nyie hata aibu hamna kabisa

Anakuja mwanamke mwenzenu anamimba hata kiti hampishi mnamtizama kama picha hadi atokee mwanaume amuonee huruma ampishe

Mwanamke ni kiumbe katiri sana
Kwa nini unadhani mwanamke ndio anatakiwa kupisha? Yaani hadi itokee hakuna mwanamke wa kupisha ndio mnasimama? Kwa nini isiwe ninyi ndio wapishaji akikosekana mwanaume ndio tusimame sisi?
 
Nilitaka nimtolee uvivu yule mwanaume ila nikaamua nikae kimya maana nilikuwa na my uncle mmoja naheshimiana nae na anajua mimi siongeagi kabisa
emoji4.png
emoji4.png
nikaamua kuilinda image yangu
Ha haa!
Utaratibu wa kupisha watu kiti kwenye dala dala nilishauacha tangu mwaka 2006! Huyo unayempisha kiti, yeye pesa ambayo angenunulia gari ya kutembelea kajengea nyumba na anakulipisha kodi kila mwezi bila kupunguza hata senti moja! Why nimpishie. Kumpisha kiti mtu, labda awe mlemavu. Mzee, sijui mama mwenye mtoto, simpishi. Kama unajua una mtoto, panda boda boda ukapandie dala dala inapoanzia upate siti au geuza na dala dala upate siti. Mie nipande boda boda hadi stendi ili nipate siti afu nije kukupisha kirahisi? Huo moyo sina kwa kweli!
Mambo ya kupakatia mitoto ya watu, wengine hawajavalishwa pampas aje kukunyea au kukukojolea afu akuharibie siku bure! Kila mtu apambane na hali yake kwenye hili...
 
Kumpisha mtu kwenye kiti mara nyingi inategemea na mood ya hyo sku
Nikiamka vzur, katika ubora wangu ata raia awe anavuja damu huwa sipishi ila ntampa pole
Mimi pia
 
Kwa sababu unampisha mwanamke mwenzako
Kwa nini unadhani mwanamke ndio anatakiwa kupisha? Yaani hadi itokee hakuna mwanamke wa kupisha ndio mnasimama? Kwa nini isiwe ninyi ndio wapishaji akikosekana mwanaume ndio tusimame sisi?
 
Back
Top Bottom