Wanaume, unaweza kufunga kizazi (vasectomy) kama njia ya uzazi wa mpango?

wa zion

JF-Expert Member
Mar 23, 2013
222
476
Jamii tunayoishi kwa asilimia kubwa inaamini uzazi wa mpango ni kwa ajili ya wanawake tu, kumekua na changamoto nyingi sana pale wanaume wanapoambiwa wao pia wanaweza tumia njia ya uzazi wa mpango ambazo hasa ni tatu tu ikiwa ni kutumia Kondomu(njia hii hutumika kwa wengi kwenye kujikinga na magonjwa hasa hasa na si mimba zisizo tarajiwa), kufunga uzazi, na kutumia kalenda.

Je wewe kama mwanaume unaweza funga kizazi kama njia ya uzazi wa mpango baada ya mke wako/ mchumba? Je kuna wanaume ambao tayari mmeshafanya hivyo?

Wanawake mngependa wanaume wenu watumie uzazi wa mpango au mtaendelea tu wenyewe?
 
Jamii tunayoishi kwa asilimia kubwa inaamini uzazi wa mpango ni kwa ajili ya wanawake tu, kumekua na changamoto nyingi sana pale wanaume wanapoambiwa wao pia wanaweza tumia njia ya uzazi wa mpango ambazo hasa ni tatu tu ikiwa ni kutumia Kondomu(njia hii hutumika kwa wengi kwenye kujikinga na magonjwa hasa hasa na si mimba zisizo tarajiwa), kufunga uzazi, na kutumia kalenda.

Je wewe kama mwanaume unaweza funga kizazi kama njia ya uzazi wa mpango baada ya mke wako/ mchumba? Je kuna wanaume ambao tayari mmeshafanya hivyo?

Wanawake mngependa wanaume wenu watumie uzazi wa mpango au mtaendelea tu wenyewe?
Inawezekana...Ila kama njia zote za uzazi wa Mpango zanamsumbua mke wangu kiafya
 
Unafunga kizazi aafu unakorofishana na mke ndio anakuambia kwanza watoto sio wako.!!
Huu uzungu ulimkost Mengi akaanza kwenda kupandikiza mimba ulaya.
Sema yeye bahati alizihifadhi huko.

Mwanaume huwa Hana mwisho wa kuzaa.
Watoto wenyewe wawili aafu mnaanza kutafuta kufunga kizazi!!
Hili somo wazungu wamelikazania Sana mpaka watakapohakikisha wametuweza.
Wanawachukia Sana wanaijeria kwa kuwa na uwezo wa kuzaa watoto wengi.

Kila unaposoma kuhusu family planning lazima waongelee kuwa disappointed na Nigerians!!
 
Jamii tunayoishi kwa asilimia kubwa inaamini uzazi wa mpango ni kwa ajili ya wanawake tu, kumekua na changamoto nyingi sana pale wanaume wanapoambiwa wao pia wanaweza tumia njia ya uzazi wa mpango ambazo hasa ni tatu tu ikiwa ni kutumia Kondomu(njia hii hutumika kwa wengi kwenye kujikinga na magonjwa hasa hasa na si mimba zisizo tarajiwa), kufunga uzazi, na kutumia kalenda.
Je wewe kama mwanaume unaweza funga kizazi kama njia ya uzazi wa mpango baada ya mke wako/ mchumba? Je kuna wanaume ambao tayari mmeshafanya hivyo?
Wanawake mngependa wanaume wenu watumie uzazi wa mpango au mtaendelea tu wenyewe?
Watoke na ujinga wao huko. Nafunga iliiwe nni kwani vifo vya mpango wameviweka?
 
Kwani nikishafunga kizazi kwasasa, huko mbele yasafari siwezi kukifungua?
 
Unaanzaje mwanaume kufunga kizazi? Vyakufunga vinakua vimeisha mpaka ifunge kizazi??
 
Ili iweje sasa wakati kutia tia mimba ndio fahari yeti,pengine wewe ndio wa kwanza kufungwa kizazi
 
Kuna mjadala niliuona mahali feminists wanataka hii ishu ya family planning ianze kusisitizwa na kwa wanaume pia.

Wanasema imefika muda wanawake wapunzike kutumia haya mavidonge yanayozuia mimba kwanini zimekuwa zikiwaletea madhara makubwa na ya muda mrefu, na badala yake wanaume ndio waanze kufanya vesctomy sababu iko salama zaidi na ni reversible.

Wanadia kwamba Mwanaume kama hauko tayari kuwa na mtoto kuliko kumwambia mwanamke wako achome sindano ya uzazi, wewe ndio uende ukakate mirija inayopitisha manii(vesctomy) halafu siku ukihitaji mtoto unaenda hospital wanairejesha(reverse) inaendelea kupitisha manii kama kawaida.

Kiukweli hakuna mwanaume mwenye akili timamu atafanya hiki kitu.
 
Kwani nikishafunga kizazi kwasasa, huko mbele yasafari siwezi kukifungua?
unaweza na ni salama zaidi kuliko mwanamke kutumia haya masindano, vidonge au vipandikizi, kwa mwanaume kufunga mirija ya kutoa manii ni non hormonal haina vichochezi vyovyote vinavyoweza kukupa madhara kama wanawake ambazo njia nyingi ni hormonal zinaweza sababisha madhara kama kunenepa, kutoka damu sana na mengineyo muda mwingine hata kushindwa kuzaa kwa muda mrefu
 
Mimi hata mke wangu siwezi kumruhusu afunge kizazi labda kama kuna sababu ya kiafya/kitabibu. Hata njia za uzazi wa mpango labda moja ile ya kutumia kalenda yake, hiyo sawa ila nyingine zote simruhusu mke wangu kuzitumia.

Kufunga kizazi au kutumia madawa ya uzazi wa mpango kwangu ni kama kukufuru lakini pia kuna madhara mengi sana kiafya.
 
Kuna mjadala niliuona mahali feminists wanataka hii ishu ya family planning ianze kusisitizwa na kwa wanaume pia.

Wanasema imefika muda wanawake wapunzike kutumia haya mavidonge yanayozuia mimba kwanini zimekuwa zikiwaletea madhara makubwa na ya muda mrefu, na badala yake wanaume ndio waanze kufanya vesctomy sababu iko salama zaidi na ni reversible.

Wanadia kwamba Mwanaume kama hauko tayari kuwa na mtoto kuliko kumwambia mwanamke wako achome sindano ya uzazi, wewe ndio uende ukakate mirija inayopitisha manii(vesctomy) halafu siku ukihitaji mtoto unaenda hospital wanairejesha(reverse) inaendelea kupitisha manii kama kawaida.

Kiukweli hakuna mwanaume mwenye akili timamu atafanya hiki kitu.
Kukishakuwa na fibrosis(kovu) kwenye kale kamrija kanaziba Tena tu.
 
Back
Top Bottom