Wanaume naomba ushauri wenu make mume wangu simuelewi

Wanaume naomba ushauri wenu make mume wangu simuelewi

miaka yote sita mliyoishi pamoja amekuwa na tabia hiyo?
 
Kuna watu wakiwa na stress hawapendagi kuulizwa kulikoni.

Na wewe kwa vile unampenda inakuuma ukimuona vile ndio maana unamuuliza.

Next time just try to keep your distance, uone kama hali itabadilika.
asante kwa ushauri
 
nimegundua mumeo yuko hivyo kwakuwa wewe si mwaminifu.unawaza kuchepuka?
hapana usipende kuhukumu. sijawai toka nje ya ndoa yangu takatifu hata siku moja. ningekuwa na wa kuniliwaza nisingeleta uzi huu kwenu ningekuwa biz na mchepuko wqngu
 
asante sana kwa ushauri wako mpendwa... japo nimeshajaribu njia hiyoila khali inaendelea kujitokeza we fikilia miaka yote khali hiyo inakuwa inamtokea.... mpaka nami akiwa amenuna siangaiki nae naumia tu..

Kwenye hali kama hii hali huwa haibadiliki haraka kwasababu anahisi unamtega tu,jambo la msingi sio kujaribu bali ni kufanya na usifanye hivyo kwa muda bali fanya hivyo maisha yako yote kwasababu huyo ni mumeo na kumfanyia hayo sio hisani bali ni jukumu lako

Unapofanya na kuja kuacha inamfanya ajue kuwa ulikuwa unamtega tu

Ukifanya hivyo bila kuweka time frame atakuja kuona kuwa umebadilika jumla na ataanza taratibu kujisogeza kwako na hatimae mambo yatakuwa mazuri tu

Just be patient !!!!!!
 
habari zenu wapendwa
mimi ni mama wa mtoto mmoja wa miaka 5 na nina mume wangu wa ndoa zaidi ya miaka sita. ila mume wangu simwelewi kitu kimoja inafika kipindi akaninunia na asikwambie sababu na ukimuuliza nini mbaya unaweeza ukalamba
hata vibao. si mara moja ili swala kujitokeza ndo mana nimeona nilete jamvini. na anakuwa na majibu ya mkato na hasira endapo nitamuuliza kitu. yani nakuwa sina thamani kwake. na naweza nikawa nyumbani na apigi kwa simu yangu anapiga ya dada na anaweza sa nyingine akarudi usiku wa manane na yupo chakali. sasa na jiuliza uu ni ugonjwa ama pepo. akiwa ajaninunia yupp sawa na ni mume mwema. ila haiwezi pita miezi 3 ajaninunia.

je mnahisi ana tatizo gani? mi nampenda sana mume wangu. ila kama binadamu akiwaga na khali hiyo nami uwa naumia mpaka sa nyingine nawaza yasiyo wazika.

Labda anakuwaga mwezini
 
Jibu unalo mwenyewe dada.Kwanza mumeo anafanyakazi gani.Pili umesema inatokea takribani kila baada ya meizi mitatu na wakati mwingine anakuja nyumbani akiwa amelewa sana.
Kama walivyosema watu wengi,mume wako anakitu kinachomkera lakini hataki kukushirikisha na bado hajakipatia ufumbuzi.

Je mumeo ni mtu ambitious lakini kipato chake ni kidogo?
Je mumeo ni mtu wa kujichanganya na watu?
Je mumeo ana marafiki wa karibu kabisa na familia yenu?
Kama wapo wewe una rafiki mmoja wa mumeo ambaye karibu ali uweze kumuuliza hata kwa ujanja janja kuweza kupata inside story ya mumeo?
Je ndugu na jana wa mumeo wanajua hali ya mwenzako?wamechukuwa uamuzi gani? Wazazi wa mumeo umeshawaeleza juu ya tabia ya mumeo ? Wanasemaje?
Hayo maswali yote yakishajibiwa kikamilfu utakuwa umetatua au umeshapata jibu juu ya kinachomsibu mumeo.
Natoa hoja.
 
Atakuwa na mahali anapopata furaha.mwombee sana atabadilika siku moja
 
Dada sikiliza mume wako anatatizo moja tu ambalo ukiweza kulimudu atabadilika ,anasykology ya kuongoza hapendi kuongozwa wala kupingwa. Kwa hiyo wazo lolote akilitoa sema ok,likiharibika then its is your right chance to argue then fanya marekebisho. Usipofanya hivi atadhani dharau. Kumbuka mwanaume always ni mtoto kwa mwanamke ktk maswala ya mapenzi,jaribu kurudisha Yale matendo ambayo ulikuwa Unafanya wakati wa uchumba mfano ,dear Leo nikutayalishie nini,kuna juice unapenda nini? Vitu vidogo tu basi atachenji. Always kuwa smart in dressing,manukato,aproching face etc.Mimi nikirudi nyumbani lzm ninywe juice nimeweka wazi kwa wife nisipokuta lzm anipe sababu. Mume wako si muwazi kwa maswala haya jalibu kurivew maisha ya awali utajua tu. Mfano mwingine mke wng nikimuudhi naenda kununua nyama choma nikirudi anatafuna yameisha, unajua ni Kwanini enzi za uchumba kila out anapenda kwenda nyamachoma. Jitahidi dada akiwa juu wewe usipande Ndio sheria
 
Watu wenye tabia ya kununanuna as their way of solving problems wana shida (Yani ni kazi kuishi nao)! Halafu mwingine eti ni mwanaume na unanuna!
a) Saa nyingine akinuna ujue msimu wa kununa umefika...akiwa na ugumu kwenye eneo lolote la maisha basi hukimbilia huko. Sasa wewe siku akiwa amelewa mbembeleze vizuri kisha muulize kuhusu maendeleo yake ukitaja eneo moja hadi jengine(Atakusumbua lakini atakupa the most honest answers). Ukishayachambua majibu kashauriane naye solution akiwa mzima sasa.
b) Saa nyingine pia akinuna kuna kitu umemuudhi na either hawezi kukuambia kwa sababu labda alishakuambia na hukurekebika ama anaogopa kukuumiza akikuambia (Fanya hivyohivyo-wakati mzuri wa maswali ni wakati kalewa then solution wakati akiwa sober).
c) He is guilty. Kuna mambo anafanya ambayo ni shida yakitambulika either kwako ama kwa jamii. Labda akiwaza kuungama anaona itakuwa shida so hajui afanyeje na ukizidi kumfanyia wema anakasirika kwa sababu anajua hastahili. Kwa hiyo anataka akuudhi ili muende sawa.

Kwa vyovyote jaribu kumtreat vizuri siku moja akiwa amelewa piga naye stori usimkasirikie utajua tu kitu ambacho huwa kinamsumbua.
Watu wa aina hii sio problem solvers kwenye mahusiano kabisa! Utasikia "I need space!". Sasa kama ulijua utahitaji space ssi ungefunga ndoa ya mkataba?
 
Defence mechanism hiyo,Huyo jamaa kuna vitu batili anavyovifanya sasa ili wewe usipate wa saa wa kuuliza anakuja amekununia utafikili ameng'ata jiwe.cha msingi komaa nae tu kuna siku utajua tu.
 
Atabadilika kadri umri unavyoenda. Kuna mtu alikuwaga hivyo hivyo huku kwetu. Sasahivi hali ni shwari kabisa. Ila umuombee.
 
Sababu ni moja tu. Kuna wakati huwa anataka mfanye ule mchezo wa kikubwa halafu unazusha vijisababu vya kukataa kugegedwa. Hata mimi huwa nina hiyo tabiw
 
Alikuoa bik.ra? Samahani, usione nimeenda off point, nna maana yangu.
 
We nawe mpe nafasi kununa kukiisha endelea naye! Unadhani kuna binadamu atakuwa anacheka muda wote?
Zingine ni sababu za kukosa hela, zingine ni kumwagwa na michepuko au kuifumania! Zingine ni stress za kazi na ups & downs za maisha!
Haha hapo pa michepuko ndo napapa asilimia mia tisa tisini na tisa bila senti
 
Muombe Mungu sana tena kwa imani atabadilika,lakn jitahidi kuampuuzia pale anapojinunisha maana hyo nitabîa yake utaumia mara ngap?
 
akinuna na wewe endelea na shughuli zako kama huoni vile, wanaume dizaini hii hiyo ndo dawa yao. mie alikuwa akinuna napotea siku nzima na-catch up na shughuli zangu za hapa na pale. kama kuna shosti sijamwona siku nyingi naenda kumtembelea tunapuyanga weee! mbona kashika adabu mwenyewe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom