Wanatuvumilia hivo hivo, watafanyaje sasa? Afu tunakuaga watamu wanawake wa hivyo, yani hatuboi.
Mfano Baba K akirudi Ile nimempokea mizigo tu naanza kumpa umbea WA majirani, nikiwa namtengea chakula nampa ubuyu wa Jf nani katumbuliwa nani kaachwa...
Ukifika muda wa mpira naangalia nae sebuleni huku tunamsimanga Feisal...!
Ukifika muda wa chakula cha usiku pia mdomo haupoi, mechi nzima ni full kumropokea Baba K unajuaa...[emoji1787]
Tukimaliza hapo naanza kumsaidia kumsengenya bosi wake na majirani wawili watatu halafu tunalala.
Yani nikisafiri siku moja tu nyumba inapoaa, ananambia mke wangu Rudi! we unataka mwanamke kapoa, haongei Ka kakatwa ulimi[emoji1787]