Wanaume mamwinyi

Wanaume mamwinyi

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
58,636
Reaction score
220,349
Kuna wanaume wanapenda u-mwinyi bwana, yaani anaamka anaenda kuoga wakati anaoga unatandika kitanda na kuweka mazingira ya chumba vizuri. Unakwenda jikoni kuandaa chai, anatoka bafuni na taulo kiunoni anatafuta atavaa boxer na kama atakumbuka mafuta basi itakuwa kwenye viganja vya mikono. Taulo atakuachia juu ya kitanda si tatizo lake tena.

Mezani umeandaa chai na vitafunio hata kama chumvi haisikiki mfano kwenye mayai atakuita ukamchukulie jikoni hapo ni baada ya kukuita umletee maji ya kunawa na tissue ya kujikaushia.

Yaani ameshindwa kabisa kwenda kunawa jikoni au bafuni au kwenda jikoni kuchukua chumvi. Na akimaliza kula hataondoa hata kijiko mezani anaacha kila kitu pale anakwenda kukaa kwenye sofa anaangalia mpira, kusoma gazeti au anachat kwenye simu. Hiyo ni weekend.
 
Ok

Sent from My GooglePixel using JamiiForums mobile app
 
Utakuwa umekutana na shetani,siyo mwanaume.

Habeeb Marhan
 
Inategemea mahusiano yenu yakoje. Kuna nyumba nyingine mke na mme wanalala vyumba tofauti kwenye nyumba moja hiyohiyo! Kwa wapenzi, wanahujua ni kupenda na kupendwa yaani kupendana. Mwanamme akiwa na nafasi mbona hata kupika anapika na mkewe!
 
Kwanza tujue je umeolewa?? Ni ngumu sana kulisema jambo hilo kwa ujumla wake...ndoa ni katiba/mkataba wa watu wawili me na ke jinsi watakavyoendesha mambo yao, kama ndo wamekubaliana hivyo nani wa kuingilia?? Wakati wewe unataka mwanaume afanya hayo wapo ambao mwanaume akifanya humkatalia na kumsihi aache atafanya yeye (ke) kwani ni majukumu yake.
 
Hayo mambo tushazoea kwenye ndoa we r Tanzanian hata usomeje mwanamke lazima mumeo umhudumie kila kitu wengi tunafundishwa hvyoo
Ni jambo la kawaida pia kwetu ukiona ananuna mke hajafundwa au uzungu mwingi

My own brand!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom