Wanaume kuogopa wanawake

Wanaume kuogopa wanawake

Habari zenu sana jf

Kuna jambo linanitatiza hapa na sijajua if lina ukweli ndani yake au la. Siku ya X-mas nilikua na rafiki yangu mmoja tukawa tunapiga story, akaniambia kuwa ukiwa msichana, unafanya kazi, unajiweza, una gari inabidi uolewe.

Mimi nikamjibu kwamba ndoa sio jambo la kukurupuka, mpaka sasa sijaona atayenifaa na ambaye nitaendana nae. Sasa nilipomwambia kuolewa is not my priority nina plans zangu za maendeleo zaidi like kujenga nyumba etc alihamaki akaniambia,"Shosti wanaume watakuogopa na hutaolewa kamwe".

Hii statement imenishangaza. Kwahiyo eti nisifanye maendeleo yoyote eti sababu wanaume wataniogopa? Mbona wanawake tumekua watumwa wa ndoa hivi? Kwanini nisifanye kitu roho inapenda kwa kuhofia hiyo kitu?

Swali langu ni je ni kweli wanaume huogopa wanawake waliowazidi kipato? Kama ni kweli ni kwanini? Kwani mwanaume akinioa anashindwa kuja kuishi kwenye nyumba yangu?
Hakuna mwanaume anaemuogopa mwanamke,labda awe ni punguani wa akili,au awe ni mtu anaetumia mbinu fulani kumlinda huyo huyo mwanamke asiende wrong ktk maisha.ukitamka neno MWANAUME hata MUNGU hustuka usingizini na kuja kuangalia kuna nini
 
Habari zenu sana jf

Kuna jambo linanitatiza hapa na sijajua if lina ukweli ndani yake au la. Siku ya X-mas nilikua na rafiki yangu mmoja tukawa tunapiga story, akaniambia kuwa ukiwa msichana, unafanya kazi, unajiweza, una gari inabidi uolewe.

Mimi nikamjibu kwamba ndoa sio jambo la kukurupuka, mpaka sasa sijaona atayenifaa na ambaye nitaendana nae. Sasa nilipomwambia kuolewa is not my priority nina plans zangu za maendeleo zaidi like kujenga nyumba etc alihamaki akaniambia,"Shosti wanaume watakuogopa na hutaolewa kamwe".

Hii statement imenishangaza. Kwahiyo eti nisifanye maendeleo yoyote eti sababu wanaume wataniogopa? Mbona wanawake tumekua watumwa wa ndoa hivi? Kwanini nisifanye kitu roho inapenda kwa kuhofia hiyo kitu?

Swali langu ni je ni kweli wanaume huogopa wanawake waliowazidi kipato? Kama ni kweli ni kwanini? Kwani mwanaume akinioa anashindwa kuja kuishi kwenye nyumba yangu?
Ww hutoolewa bali jiandae kuoa
 
Ndoa ni muungano baina ya watu wawili kuwa pamoja katika mahusiano ya kimapenzi na kuitwa mke na mume, na waliotayari kuanzisha familia.

Ikitokea mwanamke akimiliki pesa zaidi ya mwanaume sio kwamba atamdharau na kumuona mwanaume hana kitu la hasha hii inatokana na maelewano yenu katika mahusiano, kwani kuna wanawake wangapi wana pesa, kwani kuna wanawake wangapi wana elimu nzuri, kwani kuna wanawake wangapi wamepiga hatua kubwa kimaendeleo kuzidi wanaume zao lakini bado mahusiano yao yapo imara na wanaelewana vizuri, ingawa ni wachache lakini wapo wanawake wa namna hiyo.

Katika jamii nyingi tumezoea kuona wanaume ndiye anaweza kumiliki vitu vyote hivi ikiwemo pesa, elimu, mali, n.k na kuweza kuishi katika mahusiano na mwanamke yeyote yule,
Hii ni mitazamo ya watu mbali mbali na fikra zao
Kila kitu huwa na utaratibu wake aghalabu inakuwa hivyo kwamba mwanaume hawezi kuishi na mwanamke akiwa amemzidi kiuchumi, kielimu n.k..........
 
Wengi hua wanawaogopa,ila mimi niko tofauti,kama upo tayari ni pm tuyajenge mamaa
 
Kwa asilimia kubwa wanaume huogopa kuoa wanawake waliowazidi kiuchumi. Sababu kubwa ni wanaogopa kuwa wanawake watawadharau waume zao
Tatizo wanaume wamezoea ubabe, ASA unadhani Mimi na hela Yangu Mani anizingue? Sasa hapo ndio wanaanza kusema ni dharau ila sidhani
 
hatuogopi wanawake wenye kipato.. tunachoogopa ni kudharauliwa .asimia kubwa ya wanawake wanapokuwa na kipato hukosa heshima kwa wenza wao..sasa hakuna mwanaume mwenye akili timamu anapenda kudharauliwa..kumbuka kuwa we are super before God.
 
Muda mwingi mwanamke huwa sio mtu wa kujizuia maneno mdomoni,kila kukicha huja na jipya na kabla halijakuchwa humalizia na kingine,una gari,nyumba,kazi nzuri labda umpate mwenye uwezo zaidi yako ili siku utakapo mletea maneno na madharau akuone kama kinyago vile! lakini kupata mwanaume asie na kitu akupende hiyo ipo ila kukuamini au yeye kujiamini atakua kwenye amani hapo nyumbani kwako hilo halipo,utashangaa wamepita na wameondoka hata watano mpaka utasema umelogwa,mpaka mkutane wote waelewa,wakweli,wastaarabu,mnaheshimiana mnaweza ishi.
 
Binafsi naweza kusema ni lack of confidence and self-prophecy on part ya waoaji, ndoa ngapi wanawake hawana elimu, mali au kipato na hazina mawasiliano mazuri? Tuache Patriarchy form of relation nadhani
 
nimeoona hii kitu sana kwa wanaume hapa wanakuwa intimidated. wakiona kuwa uko successful, siku zote atajitahidi akuonyeshe kuwa na yeye anaweza na itafika a point itakuwa kero kwako. nimeona pia wanaume wengine wanasema 'amewezeshwa' baada ya kuona mwanamke anafanya yake, inasikitisha ila sijui ufumbuzi uko wapi hapa maana ni tatizo la upeo 'mentality' ya baadhi ya wanaume. najua kabisa rafiki zangu ambao wameamua kutotaja kazi zao, kama ana kampuni, mafanikio,mali, hata jina lake la mwisho wakiwa/wakianza relationship na mwanaume ili asijisikie intimidated na yeye, ili mwanaume awe more free. kama nilivosema ni baadhi ya wanaume. labda wadau wanaume mtuambie ni kwanini inakuwa hivi?
 
Mleta mada hujanizidi kipato sema tu sijakupenda.
 
Back
Top Bottom