Wanasheria wetu! Tumaini jipya?

Wanasheria wetu! Tumaini jipya?

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,527
Reaction score
830,085
Miaka ile ya 2000 wakati wa Gen P. Musharaf wa Pakistan, vyama vingine vyote vya siasa vikiwa vimebanwa mbavu na kuminywa hasa.... Likatokea jambo la nadra sana, sikumbuki vizuri ilikuwaje lakini nakumbuka wanasheria walichokonolewa wakachokozwa.

Hawakukubali, wakaandaa maandamo ya amani kuelekea Islamabad mji mkuu wa Pakistan, maandamano hayo yalitokea miji mingine mikuu kama Peshawar, Lahore na Karachi.

Nakumbuka wiki ya maandalizi ya yale maandamano wanasheria walitishwa sana... Lakini wakashikilia msimamo wao wa kuandamana kwa amani.... Na hatimaye wakaandamana..

Huku kwetu kuna kila dalili ya yale ya Pakistan kujirudia.... Ni wazi na sio siri vyama vya siasa vile vyenye nguvu vimebanwa kila kona na vinafanyiwa hujuma zisizoisha kila uchao, viongozi wanakatishwa tamaa kwa malundo ya kesi, hujuma ni nyingi mno na kesi pia ni nyingi.... Ni mkakati maalum uliosukwa kwa ufundi kudhoofisha na hatimaye kuua kabisa vyama makini vya upinzani..

Lakini siku zote penye nia pana njia! Wote tunajua hofu waliyokuwa nayo watawala kwa Lisu kuchaguliwa kuwa rais wa chama cha wanasheria Tanganyika! Tulishuhudia vibweka vya kila aina.... Wanasheria wakagoma kuburuzwa, wakagoma kupangiwa wakagoma kupelekeshwa! Na kubwa kuliko yote wakagoma KUNUNULIWA..

Mshikamano wao wakati ule wa uchaguzi likikuwa jambo geni, wengi walidhani baada ya pale wataachana njiapanda.... HAWAKUFANYA HIVYO..... kauli yao imekuwa SOLIDARITY FOREVER!

Mambo ya nadra yameendelea kutokea kwenye kaliba hii ya wasomi wanataaluma mahiri.... Tumeshuhudia kwenye kesi ya Lisu, tumeshuhudia kwenye kesi ya mwanamama machachari Bi Fatma Karume.... kuna bonding ya aina yake kwa hii kaliba ya sheria... Mamlaka hazipedi kabisa hili jambo lakini pengine ndio ule wakati umetimia sasa.....

A long way to freedom!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vyama vya upinzani vimekuwa vikijitahidi sana kuiwajibisha serikali kwa namna mbalimbali tatizo limekuwa kwenye taasisi nyingine binafsi na wananchi. Huko ndo bado hakuna mwamko wa kutosha na ndo mtaji mkubwa wa CCM. Kuna matukio ya kidhalimu ya wazi kabisa yamekuwepo lakini ni wananchi wachache sana wanajitokeza kwa vitendo kuunga mkono upande unaosimamia haki. Utakuta mtu anakosoa sana serikali ikifika wakati wa uchaguzi bado haendi kupiga kura.
 
Tasnia ya sheria tayari imeingiliwa na siasa. Inshu ya Pakistani ni ya kipekee kabisa. Musharaf alifukuza wanasheria (majaji) katika utumishi wa umma na ndio ikawa chanzo cha maandamano, migomo na machafuko. Kwa hapa tz mambo ni tofauti. Siasa zinalazimishwa ziingie katika sheria. TLS nayo inalazimishwa iwe ya kisiasa pasipo kuzingatia kwamba ndani ya TLS kila kitu kinaenda kwa utaratibu wake kikanuni.
Siasa zimefanya baadhi ya wanasheria wawe na kiburi, wanavimba vichwa kwa sababu wana wafuasi wa kisiasa. Wanalazimisha walete siasa hadi kwenye masuala ya sheria.
Ifikie hatua umma ufahamu kuwa hakuna siasa mahakamani. Mpinzani au mfuasi wa chama cha upinzani akishindwa kesi wanasema mahakimu au majaji wamenunuliwa, wakishinda wanatamba kuwa mahakama ni mkombozi wao. Mahakama ikishaingiliwa kisiasa hatutakuwa tena na uhuru wa mahakama. siasa ya namna yeyote ile au ya kutoka kwa yeyote yule, ikiwa ni pamoja na umma, ni hatari sana kwa uhuru wa mahakama.
Tasnia ya sheria ibaki kuwa taaluma. Sheria ikihusishwa ma masuala ya siasa hakika taifa litaangukia pabaya.
 
No easy way to go
Lawyers-Clash-with-Police-Mar-07-Pakistan1.jpg
b4f0ac5241bfde2cfc273f46e4e39ac2.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
Kibano hiki hakikuwavunja moyo bali kiliwapa morali ya kusonga mbele
1276646fc3617dd4d8fdc8013698fc71.jpg
 
Asante kwa kutukubali. Fahamu kuwa tasnia yetu hairandani na porojo,utapeli na propaganda. Ni mambo ya kifungu kwa kifungu;hoja kwa hoja. Mambo yako mahakamani mkuu!

Mtani...hivi kweli unaona/unadhani hiyo kesi aliyoifungua bi Karume ina mashiko?

Na kweli ni kesi ya kuwakilishwa na mawakili 29?

Hata kesi ya karne [O.J. Simpson murder trial] O.J. hakuwakilishwa na mawakili 10....

Au ni kiki tu hizo?
 
Back
Top Bottom