Wanasheria wetu hamna kitu

Wanasheria wetu hamna kitu

Wanasheria wa kibongo wapo tu na vyeti vyao tu mkuu

Wengi ni njaa na opportunists wanajipendekeza kuja kupata ulaji tu... Lakini nadhani hilo ni tatizo la kitaifa kwa kizazi hiki...
 
Umenena kweli mkuu, hata mahakama zetu zinapokea maelekezo kutoka chama cha mapinduzi. Kwa mfano hukumu tata ya mita 200, huitaji hata kuwa na degree ya sheria kujua kutambua kilichoandikwa kwenye sheria lkn majaji wetu ndo hivyo
 
Ukiona hivyo,fahamu kuwa hakuna sheria iliyokiukwa au kuvunjwa.Hata hivyo,mtu yeyote anaruhusiwa kupeleka shitaka kama hilo mahakamani na siyo lazima mwanasheria peke yake.
 
Kwa Uelewa wangu mdogo ,inawahusu wale waliosomea fani hiyo ingawa najua wako wa aina tofauti tofauti nadhani kama nchi hatukosi magwiji ambao wanahusika na maswala ya katiba katita jumuia yote ya wanasheria hata mmoja jamani RIP Mchungaji mtikila gone too soon1
 
Nchi yetu inaenda "automatic" katiba ni maandishi tu.

Kwa kweli hii nchi in ya ajabu sana eti nayo inawao wanasheria.

Wanasheria wenyewe si ndio aina ya Tulia...

wasomi wa bongo ni mizigo wla sio kwny sheria tu

tatzo njaa bro wanasheria njaa tupu unafikiri watafanya maamuzi ya maana kweli hii ndo nchi ya wadanganyika

Nchi inaendeshwa na watu wachache ambao hujifungia dodoma na kutunga sheria zao binafsi kwa kwa maslahi yao, sheria hio unaijua.?

Kwa jina jengine ilani ya ccm
 
Kama jaji anakuwa appointed na rais unafikil nn fedha za walipa kodi zikufa et wanasomeshwa wamsaidie nan kama awatambui kazi yao ni ipi katika jamii
 
Nilikuwa nawaza semister hii walimu wa constitutional law watafundisha nn wanafunzi wa first yr? Watatoa mifano gani? Sion haja ya kuendelea kufundisha sheria vyuoni

Mbona wanafundisha tena vyema tu..hata kuvunjwa kwa katiba wanawafundisha dhahiri. Walimu wanaelewa udhaifu wa katiba na wanawaeleza wanafunzi wao. Hata walio serikalini wanajua katiba hii ni dhaifu na wenye madaraka wanajua fika. Hivyo walimu vyuoni huwasaidia wanafunzi wa sharia waijue katiba yao vyema. Majaji tu nao wanajua udhaifu huo na mahakimu pia. Tatizo ni kuweka siasa katika katiba na kuingilia muhimili wa Juduciary na wanasiasa. Ila tutafika tu...
 
ulitaka tujali matumbo ya mama yako? tulisoma kwa shida halafu tufanye kesi zisizo na malipo hizo kwani tulisoma bure? kama ndio hivyo wewe si ungesoma sheria,,utajuta kwanini mlikimbia sheria na kwenda huko hopeless. tupatieni pesa muone kama hatuwasaidii hapa nchni.
Duh! kwa uandishi huu na wewe unajisifia ni mwanasheria? Kweli hii fani imevamiwa.
 
tunawaonea bure. kwan cc raia wa kawaida tumechukua hatua gan?
 
Mwanasheria akiwa upande wa serikali hawezi kuApply sheria bali kutekeleza order tu.
 
Wanasheria wetu wachovu HAMNA KITU,katiba inavunjwa hakuna kesi mahakamani,katiba imevunjwa kufuta matokeo zanzibar wako kimya,katiba imevunjwa kutangazwa matokeo wako kimya,katiba imevunjwa kumpa cheti jpm wako kimya,katiba imevunjwa kumuapisha wako kimya,katiba imevunjwa kuitisha bunge wako kimya ,katiba imevunjwa kuwaapisha wabunge wako kimya na bado katiba itavunjwa kwa Jpm kuhutubia bila kuwa na Baraza la wawakilishi hakuna watakachofanya.

Nahisi kuna wanachoogopa kutumia weledi wao kutatua hili swala.Nadhani katiba Inakataza kuhoji matokeo mara baada ya rais Kutangazwa lakini sidhani kamapia imekataza kuhoji michakato mingine.Lowasa aliona mbali sana katika swala la elimu ,elimu ,elimu.
Inawezekana hata wao kupata huo uwakili katiba ilivunjwa nani amnyooshe mwingine kidole:lock1:
 
kasikilize wimbo WA Tundaman akiwa na Spark unaitwa Pesa. unaimbwa pesa uko juu ya sheria, ni mafukara ndio tunaumia, kwani haki YANGU nadhulumiwa nafungwa, ukiwa na pesa utavishwa dini na ukisema we Mungu watakuamini.
 
Wanasheria gani unaowazungumzia Mkuu? Fafanua tafadhali

Nilitegemea wanasheria ndiyo mngekuwa busy kutuelimisha kuhusu haki zetu.Bahati mbaya 90% ya wanasheria wetu wanasubiria uteuzi wa kuwa majaji.

Nilitegemea wanasheria wetu kupiga na kiume mahakamani kufika mpaka ICJ ili kutetea haki za msingi za RAIA wa Tanzania kuchagua Viongozi wao,haki ya kuishi,Haki ya kupiga kura,haki ya kuwa kiongozi hata kama zipo kwenye list ya familia za watawala.Peter bahati mbaya wanasheria wetu wengi siyo wazalendo wengi wao wamekuwa sababu ya maovu kuongezeka dhidi ya raia
 
  • Thanks
Reactions: Art
Kwa Uelewa wangu mdogo ,inawahusu wale waliosomea fani hiyo ingawa najua wako wa aina tofauti tofauti nadhani kama nchi hatukosi magwiji ambao wanahusika na maswala ya katiba katita jumuia yote ya wanasheria hata mmoja jamani RIP Mchungaji mtikila gone too soon1

Hv kweli unadhani mgogoro wa Zanzıbar nı wa kikatiba kweli?Lipi lijadiliwe,madaraka ya Jecha kufuta uchaguzi Zanzibar,Seıfu kujitangaza mshindi au Shein kuendelea kuwa rais!
 
Kama jaji anakuwa appointed na rais unafikil nn fedha za walipa kodi zikufa et wanasomeshwa wamsaidie nan kama awatambui kazi yao ni ipi katika jamii

Wengi hamuelewi dhana ya uwepo wa mataifa na serikali zake.Wewe ungependa Judge ajiteue au iweje?Ni judge yupi uliyesıkia amevuliwa ujaji wake na Rais?Vyovyote na popote,judge anateuliwa japo vyombo vya uteuzi vyaweza kuwa tofauti.
 
Back
Top Bottom