Wanashangilia mazingaombwe na wanasifia viini macho! ... Silly People!

KUna uwezekano kwamba lolote kubwa laweza kuchukuliwa dhidi ya wale wanaodaiwa kuchukua rushwa?
 
Na wewe pia unalalamika, so no difference! Hata hivyo hapo kwenye bold ulipaswa kuandika hatu na sio hawa-. Unategemea nani achukue hatua wakati wewe unaishia ku-post tu JF? Huu nao ni UDHAIFU wa Watz!
ha ha ha ha ha Mkuu SJumaa26, ukifika kwenye ofisi yangu ndio ungetambua anyway sikoupande wowote wa kimaamuz ya public.
 
ha ha ha ha ha Mkuu SJumaa26, ukifika kwenye ofisi yangu ndio ungetambua anyway sikoupande wowote wa kimaamuz ya public.
If you remain neutral in cases of injustice, that means you have chosen the side of the oppressor. You are either with us or against us! Period.
 
KUna uwezekano kwamba lolote kubwa laweza kuchukuliwa dhidi ya wale wanaodaiwa kuchukua rushwa?

Zaidi ya kusaidi kupunguza nguvu ya upepo utakao pita sidhani! Ni upepo tu mdogo mdogo unapita ila ili usichukue karatasi zetu za katuni tunazozichora basi acha tukinge mikono yetu dhidi ya upepo lol!
 
Ama kweli tumejifunza kufurahi. hata hapo kwenye picha uloambatanisha inaonyesha nyuso za furaha!!
 
Kwamba Mhando (Mkurugenzi wa Tanesco) amejipa mkataba yeye na mke wake na kukiuka waziwazi sheria ya maadili ya viongozi wa umma ya 1998 halina shaka. Lakini cha kushangaza ni kuwa ati Waziri anaenda kumlipua Bungeni badala ya aliyemteua kumfukuza kazi, kumtia pingu na kuhakikisha anaingia gerezani yeye na wote waliowezesha dili hilo.
MMM

Mzee Mwanakijiji,

Hii nchi ina sheria na taratibu zake, huwezi kukurupuka tu kumtia mtu pingu na kumtupa lupango bila kufuata hatua stahili. Kama ndio hiyo Tanzania mnayotaka kutuletea basi itakuwa vurugu mechi mitaani. Tulieni msikie hatua zitakazochukuliwa usikurupuke tu kutaka kuona watu wanatiwa pingu mwishowe yanakuwa yale yale ya Dowans wanasiasa kina Zitto kufurahisha wananchi kama wewe mwishowe ina tu cost nchi nzima tunalipa fidia mabilioni.

Msipende kuhadaa wananchi...
 
SDC12308.JPG

Katika umaskini wetu tumejifunza kufurahia! MM​
Mzee Mwanakijiji,
Hii nchi ina sheria na taratibu zake, huwezi kukurupuka tu kumtia mtu pingu na kumtupa lupango bila kufuata hatua stahili. Kama ndio hiyo Tanzania mnayotaka kutuletea basi itakuwa vurugu mechi mitaani. Tulieni msikie hatua zitakazochukuliwa usikurupuke tu kutaka kuona watu wanatiwa pingu mwishowe yanakuwa yale yale ya Dowans wanasiasa kina Zitto kufurahisha wananchi kama wewe mwishowe ina tu cost nchi nzima tunalipa fidia mabilioni.Msipende kuhadaa wananchi...
Kwa bahati nzuri sana MMM kaweka hiyo picha ambayo kwa mtanzania yeyote anajua kuwa hii inaonyesha hasa uhalisia wa tulio wengi. Tukishasoma vichwa vya magazeti hapo (hasa yale ya shigongo) unabishana kama dakika 10-30 alafu unasepa. Hatuwezi tena kufikiria mambo kwa makini na usahihi na woga umepitiliza.
Kwa hiyo wewe wananchi unaowaongelea kuwa wanahadaiwa ndio hao na serikali inafurahia tu. Lakini swali ni kuwa ...ungelifurahia kuwa miongoni (sehemu) mwa hawa wanaoonekana katika picha???



 
Mkuu Mzee Mwanakijiji umeongea na nakubaliana na uchambuzi wako
Ila tatizo watu wetu ni wasahaulifu sana na ni watu wa matukio
Likitokea hili wanasahau lile la mwanzo na kuanza ushabiki wa hili jipya na hakuna hatua zozote wanazochukua kuonyeshwa kukerwa kwao na hilo lililopita
Asante sana kwa uchambuzi wako
Usisahau kwamba huo ujinga tulonao wa kushabikia matukio ndo kete yao ili kutuburuza.
Na kwakuwa walisha litambua hilo, ndio maana mazingaombwe hayeshi, kila siku kuna ingizo jipya!
Ukihoji lililopita limeishia wapi, utasikia aaa bwana mdogo kitu iko kwa mahakama usiijadili/ulizia.
mwisho wa siku uchaguzi huo tunawapa tena nafasi kwa kete hizo hizo za kujinasibu kwamba tunawajali na tunapambana kweli kweli na wezi,kama mnavyoshuhudia kesi ziko mahakamani.
 
Maneno mengiii, ili kutaka jamii ikuone umesema jambo la maana! Ukweli utabaki pale pale wewe subiri siku ukishika nchi uje na hizo SERA zako zinazo wezekana, lakini kwa sasa endelea tu kupiga domo watu wanapiga kazi.

Wanapiga pesa au wanapiga kazi. Mpaka wamalize nchi yote. Tusubiri mpaka wakombe. Ukipiga domo utapelekwa MABWEPANDE tena ungolewe meno na kucha +kuvunjwa mbavu na/au kulishwa sumu ufe. Acha wapige pesa usiseme lolote nyamaza. Wewe ni domokaya=CDM= CHADOMO
-By Kuwadi wa CCMABWEPANDE
 
Mzee Mwanakijiji,

Hii nchi ina sheria na taratibu zake, huwezi kukurupuka tu kumtia mtu pingu na kumtupa lupango bila kufuata hatua stahili. Kama ndio hiyo Tanzania mnayotaka kutuletea basi itakuwa vurugu mechi mitaani. Tulieni msikie hatua zitakazochukuliwa usikurupuke tu kutaka kuona watu wanatiwa pingu mwishowe yanakuwa yale yale ya Dowans wanasiasa kina Zitto kufurahisha wananchi kama wewe mwishowe ina tu cost nchi nzima tunalipa fidia mabilioni.

Msipende kuhadaa wananchi...
Tulieni mpaka tushibe!! tutaunda tume au tutakamata kichaa tumpeleke mahakamani ili kuziba midomo michafu (usiingilie mahakama). Tufuate taratibu na sheria!! EPA, nani alikamatwa!!?? Richmond nani alikamatwa!? hivi Rostam ni mmiliki wa DOWANS na Richmond yuko wapi? Rostam aliyemfadhili JK kwenda ikulu akamatwe na nani? Sheria zipi na taratibu zifuatwe? Nyie wezi wa EPA rudisheni fedha mlizoiba kidogo kidogo ama tusijelaumiana!! by JK. hizi ndizo taratibu na sheria!!
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji umeongea na nakubaliana na uchambuzi wako
Ila tatizo watu wetu ni wasahaulifu sana na ni watu wa matukio
Likitokea hili wanasahau lile la mwanzo na kuanza ushabiki wa hili jipya na hakuna hatua zozote wanazochukua kuonyeshwa kukerwa kwao na hilo lililopita
Asante sana kwa uchambuzi wako
Usiwalaumu wananchi Mkuu. Haya mambo yanahasisiwa na Chama Tawala ili yawe hivi, recently kuna kitengo maalumu Ikulu cha kuasisi upuuzi huu, ili tu Mfalme asizungumziwe. Na wamefanikiwa.
 
Sasa naamini kile alichokisema Confucius (551-478)BC Mwanafalsafa wa uchina kuwa "Kwa nchi inayotawaliwa vizuri umaskini ni kitu cha aibu na kwa nchi inayotawaliwa vibaya utajiri ni kitu cha aibu pia".Rasilimali na fursa pekee havitoshi bali ni uongozi bora na wenye fikra hai!!
 
Sasa ninaamini kile alichokisema Confucius (551-478)BC Mwanafalsafa wa uchina kuwa "Kwa nchi inayoongozwa vizuri umaskini ni kitu cha aibu na kwa nchi inayoongozwa vibaya utajiri ni kitu cha aibu pia".Rasilimali na fursa pekee hazitoshi bali ni uongozi bora na wenye fikra hai!
 
Usisahau kwamba huo ujinga tulonao wa kushabikia matukio ndo kete yao ili kutuburuza.
Na kwakuwa walisha litambua hilo, ndio maana mazingaombwe hayeshi, kila siku kuna ingizo jipya!
Ukihoji lililopita limeishia wapi, utasikia aaa bwana mdogo kitu iko kwa mahakama usiijadili/ulizia.
mwisho wa siku uchaguzi huo tunawapa tena nafasi kwa kete hizo hizo za kujinasibu kwamba tunawajali na tunapambana kweli kweli na wezi,kama mnavyoshuhudia kesi ziko mahakamani.

Nafikiri mkuu Kisoda2 haya mambo ya kusema kesi iko mahakamani haifai kuhojiwa yafikie mwisho wake tuone kile kinachotokana na hizo kesi mahakamani
Maana inawezekana kesi mahakamani then mshatakiwa anakuja kuachiliwa kwa kukosa ushahidi au kutokuwa na kesi ya kujibu na hapo moto wa ile kitu unakuwa umeisha kabisa
Tufikie mahali tuhoji haya mambo tuone wahusika wanapelekwa kweli mahakamani na kesi yao inaamuliwa kwa kipindi kifupi na tunaona uwajibikaji au wa kurudisha kile kilichopotea au kufilisiwa
Kesi za akina Mramba na Yona mpaka leo ni danadana hatuoni maemdeleo na itafika 2015 tutadanganywa kuwa tumewafikishamafisadi mahakamani na si mnaona akina fulani na kura tutawapa tena
haya ndio yanayotumpumbaza wananchi tuache kuhoji mambo ya maana tuwasikilize uwongo wanaotulisha


Usiwalaumu wananchi Mkuu. Haya mambo yanahasisiwa na Chama Tawala ili yawe hivi, recently kuna kitengo maalumu Ikulu cha kuasisi upuuzi huu, ili tu Mfalme asizungumziwe. Na wamefanikiwa.
Mkuu Sangarara nakubaliana na wewe kabisa
Kuna sehemu wamekaa watu wanaanzisha zengwe wananchi wajadili kwa hasira na pupa wakiona single yao inaanza kuchuja wanalianzisha tena jingine ili wananchi wasahau lile la kwanza zito waanze kujadili jepesi
yaani hizi single zao hazikao sokoni kabisa yaani zinatolewa mara kw amara wanapoona kuna haja ya kutoa single kuwasahaulisha wananchi na yale yaliyopita
Wasahau mpaka shida zao waanze kujadili lile tukio
 
Last edited by a moderator:
Tulieni mpaka tushibe!! tutaunda tume au tutakamata kichaa tumpeleke mahakamani ili kuziba midomo michafu (usiingilie mahakama). Tufuate taratibu na sheria!! EPA, nani alikamatwa!!?? Richmond nani alikamatwa!? hivi Rostam ni mmiliki wa DOWANS na Richmond yuko wapi? Rostam aliyemfadhili JK kwenda ikulu akamatwe na nani? Sheria zipi na taratibu zifuatwe? Nyie wezi wa EPA rudisheni fedha mlizoiba kidogo kidogo ama tusijelaumiana!! by JK. hizi ndizo taratibu na sheria!!

Wewe kama hujui kama wezi wa EPA walikamatwa basi hustahili kuwa kwenye hili jukwaa.
 
Nafikiri mkuu Kisoda2 haya mambo ya kusema kesi iko mahakamani haifai kuhojiwa yafikie mwisho wake tuone kile kinachotokana na hizo kesi mahakamani
Maana inawezekana kesi mahakamani then mshatakiwa anakuja kuachiliwa kwa kukosa ushahidi au kutokuwa na kesi ya kujibu na hapo moto wa ile kitu unakuwa umeisha kabisa
Tufikie mahali tuhoji haya mambo tuone wahusika wanapelekwa kweli mahakamani na kesi yao inaamuliwa kwa kipindi kifupi na tunaona uwajibikaji au wa kurudisha kile kilichopotea au kufilisiwa
Kesi za akina Mramba na Yona mpaka leo ni danadana hatuoni maemdeleo na itafika 2015 tutadanganywa kuwa tumewafikishamafisadi mahakamani na si mnaona akina fulani na kura tutawapa tena
haya ndio yanayotumpumbaza wananchi tuache kuhoji mambo ya maana tuwasikilize uwongo wanaotulisha



Mkuu Sangarara nakubaliana na wewe kabisa
Kuna sehemu wamekaa watu wanaanzisha zengwe wananchi wajadili kwa hasira na pupa wakiona single yao inaanza kuchuja wanalianzisha tena jingine ili wananchi wasahau lile la kwanza zito waanze kujadili jepesi
yaani hizi single zao hazikao sokoni kabisa yaani zinatolewa mara kw amara wanapoona kuna haja ya kutoa single kuwasahaulisha wananchi na yale yaliyopita
Wasahau mpaka shida zao waanze kujadili lile tukio

Mkuu, Ninachokiona ni kwamba, wanajisababishia pressure kubwa dhidi yao uko mbeleni, sababu soon watu wataachana na Keyboards na kwenda kuongea na wananchi uso kwa uso. Na hili inabidi tujiandae nalo sababu uwezu wa wenzetu wengi ni mdogo sana na kwa sababu wengi pia hawana matumaini na maendeleo ya ziada wanakuwa wepesi sana kusahau wanachokitaka ni nini wanaishia kununua hizi stupid singles.
 
tumeshindwa kutumia bongo na elimu zetu sasa tusubiri kuzikwa tukiwa hai maana hata katika uzima wetu hatuna tofauti na wafu.sisi ni kama marehemu tu.
 
Mkuu, Ninachokiona ni kwamba, wanajisababishia pressure kubwa dhidi yao uko mbeleni, sababu soon watu wataachana na Keyboards na kwenda kuongea na wananchi uso kwa uso. Na hili inabidi tujiandae nalo sababu uwezu wa wenzetu wengi ni mdogo sana na kwa sababu wengi pia hawana matumaini na maendeleo ya ziada wanakuwa wepesi sana kusahau wanachokitaka ni nini wanaishia kununua hizi stupid singles.

tatizo lililopo Mkuu Sangarara ni kuwa bado wana ule wimbo wa kuwa fikora za mwenyekiti ni sahihi siku zote
Na bado hawafikirii wala kujiuliza je wananchi wa sasa ni kama wale wa enzi zile ambao unaweza kuwadanganya kwa pipi na wakakupa dhahabu
bado wanawaza miaka ile ambapo masuala yao kuonekana kweney vyombo vya habari ilikuwa mwiko
Bado hawajajua kuwa wananchi wameerevuka mpaka vijijini wanasoma magazeti na wanaona kwenye luninga potelea mbali ni ya mwenyekiti wa kijiji
Hawajui haya madudu wanayoyafanya na hizi single zao mpaka vijijini watu wanaziimba na wamenyamaza kimya kabisa kuangalia ni kipi watu watafanya
Then yule ambaye ametuhumiwa au amekula cha kwake cha juu ni huyo huyo ataenda tena kule kule kwa wanakijiji akawaimbie wimbo ule ule wa ahadi mia moja ambazo wananchi wanajua kwa uhakika hawezi kutekeleza hata moja
Jua litawaka kutapambazuka na mambo haya yataanikwa hadharani kumjua mbaya wa wananchi ambaye alisababisha wasipate sukari ya kuwasaidia asubuhi wapate chai au aliyesababisha mgao wa umeme au aliyesababisha daktari akagoma au mwalimu akagoma
Aliyesababisha au kupitisha budget mbovu ambayo hamsaidii mkulima wala mfanyakazi
hapo ndipo watajiuliza walikuwa wapi muda wote kugundua kuwa wananchi wamewajua
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom