Wanasema Ndoa ni Zaidi Kufanya Mapenzi, Naomba 'Components' Nyingine za Ndoa

Uwapo kwenye ndoa,tendo la ngono baina ya Mme na mke linageuka kuwa tendo takatifu. Tendo la ndoa limebeba ndoa kwa kiasi kikubwa kwa sababu moja ya wajibu Mkubwa na agizo kuu walilopewa wanandoa na Mungu ni kuzaa watoto na kuwalea vema. Kwa hiyo tendo la ndoa siyo kila kitu kwenye ndoa Bali ni sehemu tu ya ndoa. Kuna matendo mengine makuu pia na yakikosekana hayo basi pamoja na matendo ya ngono ni kazi bure mf. Kupendana, Kusameheana na Kuvumiliana. Kwenye kuvumiliana hapo ina maana kuna wakati mmoja Wa wanandoa anaweza kuwa hana uwezo Wa kuzalisha au kuzaa japo anafanya tendo la ndoa na mwenzake bado mtatakiwa kukubali hali hiyo pasipo kinyongo. Haya ni machache tu ndoa ni zaidi ya tendo la ndoa.
Kwahiyo ukiacha kufanya mapenzi kuna nini cha ziada katika ndoa?
 
Mkuu, naomba nitofautiane na ww kidogo hapo kwenye kuvunjika kwa ndoa na sababu ikiwa ni mmoja wenu hawezi kufanya tendo la ndoa. Hoja inakuja kwamba kwa mfano katika pilikapilika za maisha yenu ikatokea kwamba mmoja wenu anapata ajali au ugonjwa na ugonjwa huo ukamwathiri kiasi kwamba hataweza tena kufanya tendo la ndoa. Hapo utatakiwa kuendelea katika ndoa hiyo na ndoa haitavunjwa.
Lakini pia inawezekana Ndoa ikavunjwa kutokana na Hatari ya kudhuru Uhai kati yenu. Kwa mfano jaribio la kuua (Kwa sumu au njia nyingine) linalojirudia-rudia au vitisho, kipigo kilichokithiri, Uasherati/Uzinzi n.k. Kwa kifupi ni kwamba zipo sababu nyingine pia ambazo ndoa inaweza kuvunjwa sio tu kwa kushindwa tendo la ndoa.
Ndugu kwa Wa RC ndoa haivunjwi kwa sababu yoyote ile tofauti na kifo. Labda mwanandoa mwenzake akifariki hapo ndoa itakuwa imevunjika na ataruhusiwa kuoa mwanamke mwingine au kuolewa na mtu mwingine. Sijajua kwa madhehebu mengine. Kitanzi cha milele kiko pale "niko tayari kuishi nae kwenye shida na raha, Magonjwa...." na "Hakika aliunganishalo Mungu Mwanadamu hawezi lifungua". Hapo mbwembwe zote zinakuwa zimeishia hapo.
 
Ndoa inaweza kuvunjwa huko kanisani ikiwa mmoja anaefunga ndoa Hawezi kufanya tendo La ndoa.
Hii ina maana ndoa natendo lake Ndio msingi wa ndoa.
Mengine yote unaweza kufanya na yeyote Mfano unaweza kushauriwa, kupikiwa, kupewa fedha n. K Na yeyote lakini ole wako ufanye tendo La ndoa na mwingine asie mwenzi wako hiyo inakua Kesi kubwa na chanzo cha matatizo.
Ndoa bila tendo la ndoa Sio ndoa ni urafiki Wa karibu tu Kama urafiki mwingine.
Kwa wakristo ndoa haivunjiki. Hayo unayosema yanapaswa kutatuliwa mwanzoni kabisa kabla ya ndoa. Hivyo kukiwa na shida zitazogundulika mapema ndoa haitafungwa na siyo kuvunjika.
 
Back
Top Bottom