Wanaowasha full light barabarani usiku


sheria ya usalama barabara no.30 ya mwaka 1973 na marekebisho yake no 16 ya 1996 sehemu ya 39 kifungu cha 39c kifungu cha 5 inasema: dipped (beam) itaruhusiwa kwenye
(a) mitaa ya watu wengi na zipo taa za kandokando mwa barabara,
(b) iwapo anamkaribia mwenzake ili wapishane vizuri
(c) iwapo anataka kulipita gari la mbele yake
(d) mtu yeyote akitenda kinyume cha hapo atakuwa ametenda kosa.
 
Mimi usiku nawasha full light kama hakuna gari napishana nayo, ila niko makini nikiona gari inakuja naondoa full light. Nikiona mwenzangu yuko full, na mimi naweka full ghafla naondoa tena kama hashtuki namwekea full moja kwa moja tukomoane tuu.

Kiustaarabu mwenzako akikushtua ni vyema ukamheshimu, la sivyo na yeye atakuwekea maana unamwumiza
 
Ebu jaribu kutoa matumizi ya hizo taa,je ziwashwe mchana tu?
 


Wala hawana haja ya ku design upya, zipo tayari duniani. Kuna magari yanakuja nazo.

Kiasi cha serikali kuagiza tu kuwa lazima kila gari ifungwe hicho kifaa.

Jisomee:Automatic Vehicle Headlight Dipper/Dimmer Circuit | Homemade Circuit Projects
 

Nenda mafunzo ya udereva Ndugu ndio utajua matumizi ya taa ,wapi na wakati gani inapaswa kutumika.
 
Kama wewe hujui kuendesha gari usidhani wote wapo kama wewe> Nimesoma driving na leseni ninayo> ninaendesha magari tangu miaka ya mapema ya 1980. Usikurupuke humu jf.
 

Umeongea jambo la msingi sana na kitu ambacho huwa nakifanya pia, ajabu kuna mtu unamshutua ili apunguze halafu wala hajigusi wanakera sana hawa watu kwakweli
 

Asante kwa hii post, naamini kuna watu watabadilika baada ya kusoma huu uzi kama tu watajifunza kuwa wastaarabu
 
Katika latest design ya magari Toyota Landcruiser vx v8 inayotarajiwa kutoka mwaka 2016, hayo yote yameangaliwa, Gari itabadilisha yenyewe taa kulingana na mazingira na mahali, itapunguza mwendo yenyewe endapo umeisogelea gari nyingine kwa nyuma ili kuepusha ajali au kusimama yenyewe kama gari iliyoko mbele yako imesimama na kama wewe huko kwenye nafasi ya kuipita. yapo mengi sana yaliyoboreshwa.
 
Kweli kabisa hata kwa waenda kwa miguu...hususan tukiwa tumepiga maji
 
funga spot light anayekupiga full na wewe unafanya yako!

Unamuogesha na lijitaa hiloo........
ila mimi nadhani........ili kupunguza ajali.....serikali ifanye barabara zote za masafa marefu ziwe double road.......katika mfano huu.......Ili hata kwenye kupigana taa........msipatane.......
 

Attachments

  • image.jpg
    19 KB · Views: 146
Kweli kabisa hata kwa waenda kwa miguu...hususan tukiwa tumepiga maji

Tena ukiwa maji......unaona kama ni pikipiki mbili zinakuzengua............bora kusiwe na hizo taa kabisa...........
 

Haswa wale walio rithi leseni badala ya mali, wale walio okota leseni na wale wanao endesha magari ya shemeji zao wana adabu mbaya sana tena mara nyingine una mpa na ishara hata ashtuke chaa ajabu ana kuwa mkaidi na mwingine ndio anakuwashia na spotlight!
 
Hili tatizo liko sana kwa madereva wa mjini. Siku akioata safari atajuta atakapokutana na lori lina mifull ya ajabu.

Kuepukana na tatizo hili tembea na kioo cha kujiangalizia kile cha nyumbani ukipigwa full unakiweka pale mbele wala huna haja ya kumflash lazima atazima mifull yake maana reflection yote ataipata mwenyewe.
 
Unamuogesha na lijitaa hiloo........
ila mimi nadhani........ili kupunguza ajali.....serikali ifanye barabara zote za masafa marefu ziwe double road.......katika mfano huu.......Ili hata kwenye kupigana taa........msipatane.......

Hata kwenye double ukikaa upande wa kulia utajuta ukikutana na mtu ana sports light zake zile za xenon full hd headlight. Lazima utaingia mtaroni.

Kuepuka shari wakati wa usiku nakaa upande wa kushoto kwenye hizi double sitaki shida.
 
Unamuogesha na lijitaa hiloo........
ila mimi nadhani........ili kupunguza ajali.....serikali ifanye barabara zote za masafa marefu ziwe double road.......katika mfano huu.......Ili hata kwenye kupigana taa........msipatane.......

Hata kwenye double ukikaa upande wa kulia utajuta ukikutana na mtu ana sports light zake zile za xenon full hd headlight. Lazima utaingia mtaroni.

Kuepuka shari wakati wa usiku nakaa upande wa kushoto kwenye hizi double sitaki shida.
 
Khaa!! Hapa inabidi ujisogeze kidogo kwenye driving
 
Usiombe kupishana na Coaster za bagamoyo huku Boko Ile mijitu haijui dim yenyewe ni full light halafu inaendesha hovyo,sijui ndo viroba fake halafu karibia wote...nshafunga spot lights ni mwendo wa piga nikupige nikikuflash ukawa mstaarabu Nami nanywea wengine wale wa maselela wanawasha maspots ya juu ni shida kabisa,tubadilike.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…