Wanaovujisha taarifa na nyaraka muhimu za serikali, hii imekaaje?

Kama wana vujisha kwa maslahi ya nchi,nawaombea Mungu wazidi kupata zingine nyingi zaidi
 
Edward Snowden alivujisha siri za serikali lakini kwa usalama wake akakimbilia Hong Kong ambako ndiko alikofanyia hiyo "whistle blowing" kwa kumpa data mwandishi wa the Guardian ambae kwake ni source ya habari yake.

Baadae akifahamu madhara ya alichokifanya akaomba hifadhi ya ukimbizi nchini Russia na akatoroshwa na kuingia Moscow na hadi leo ni "most wanted man" na wamarekani.

Sasa Marekani ipo sheria na inakataza kuvujisha nyaraka na taarifa pamoja na siri za serikali, sheria hizi zimewekwa kwa makusudio fulani.

Je, kwa Tanzania twaona hali hiyo ni sawa kwasababu tu alevujisha amempa hizo taarifa Tundu Lissu?

Tuzungumze ukweli tusiwarubuni wasomaji wengine hapa.
Ondoa habari za Tundu Lissu. Ukitaja jina la Tundu Lissu tu tayari kuna watu wana bias. Hata akija msibani watu watasema kaja kisiasa.

Tuache specifics za case ya Tundu Lissu kiporo. Tutalirudia. Twende kujiuliza maswali kama ya Socrates ngazi kwa ngazi pole pole. Tutafika kwa Tundu Lissu. Lengo si kumtetea au kumuumbua Tundu Lissu. Lengo ni kupata ukweli.

Nimekuuliza swali hapo juu hujalijibu.

Mfanyakazi wa serikali anayefichua ubaya wa serikali kwa kuvujisha nyaraka za siri za serikali anastahili kutetewa kama whistleblower anayetuonyesha ubaya wa serikali au kuhukumiwa kama mfanyakazi msaliti aliyevunja maadili ya kazi yake kwa kuvujisha siri za serikali?

Sent from my Kimulimuli
 
Ondoa habari za Tundu Lissu. Ukitaja jina la Tundu Lissu tu tayari kuna watu wana bias. Hata akija msibani watu watasema kaja kisiasa.

Tuache specifics za case ya Tundu Lissu kiporo. Tutalirudia. Twende kujiuliza maswali kama ya Socrates ngazi kwa ngazi pole pole. Tutafika kwa Tundu Lissu. Lengo si kumtetea au kumuumbua Tundu Lissu. Lengo ni kupata ukweli.

Nimekuuliza swali hapo juu hujalijibu.

Mfanyakazi wa serikali anayefichua ubaya wa serikali kwa kuvujisha nyaraka za siri za serikali anastahili kutetewa kama whistleblower anayetuonyesha ubaya wa serikali au kuhukumiwa kama mfanyakazi msaliti aliyevunja maadili ya kazi yake kwa kuvujisha siri za serikali?

Sent from my Kimulimuli

Kwanza anaacha kazi na pili anatafuta mahali pa kujihifadhi na mwisho anatoa hizo nyaraka.

Mtumishi wa serikali huwa anakula kiapo cha kulinda siri za serikali kama masharti ya kuajiriwa.
 
Sidhani kama TISS wanajihusiaha na siasa.

Isitoshe kuna tetesi kwamba kuna jamaa wapo kwenye mikono salama saa hii wakiwasaidia TISS kuhusiana na hili la juzi.

Unaposema TISS ndiyo wanahuska kuvujisha hizo nyaraka na taarifa kwa maslahi mapana ya nchi unamaanisha nini?

Kwamba nchi itataifishwa? are you serious?

Tufafanulie kiongozi.

Hawajiusishi na siasa? Nani kakudanganya?
 
Kwanza anaacha kazi na pili anatafuta mahali pa kujihifadhi na mwisho anatoa hizo nyaraka.

Mtumishi wa serikali huwa anakula kiapo cha kulinda siri za serikali kama masharti ya kuajiriwa.
Nyaraka zipo katika computer yenye encryption ambayo mfanyakazi wa serikali tu ndiye anaweza kuzipata.

Akiacha kazi mara moja access yake kupata hizo nyaraka inakuwa terminated.

Nyaraka zinaonyesha serikali imeharibu kweli.

Afanyeje?

Avujishe akiwa mfanyakazi wa serikali na kusaidia umma hata kwa kuvunja miiko ya kazi au aangalie miiko ya kazi na kuacha serikali iharibu mambo na kuwa cost wananchi?

Sent from my Kimulimuli
 
Kama wana vujisha kwa maslahi ya nchi,nawaombea Mungu wazidi kupata zingine nyingi zaidi
Nchi zilizoendelea na kuwa na sheria nzuri hawa watu wana sheria za kuwatetea.

Sheria ya Wamarekani kutetea whistleblowers hii hapa.

Whistleblower Protection Act - Wikipedia

The Whistleblower Protection Act of 1989, Pub.L. 101-12 as amended, is a United States federal law that protects federal whistleblowers who work for the government and report agency misconduct. A federal agency violates the Whistleblower Protection Act if agency authorities take (or threaten to take) retaliatory personnel action against any employee or applicant because of disclosure of information by that employee or applicant. Whistleblowers[1] may file complaints that they believe reasonably evidences a violation of a law, rule or regulation; gross mismanagement; gross waste of funds; an abuse of authority; or a substantial and specific danger to public health or safety.

Sent from my Kimulimuli
 
Soma tena mkuu nadhani wewe ni wa kwanza kuuliza suali hilo.

Nimemtumia DT kama mfano.

Baaada ya taarifa kuwa zinavuja sana serikali ya Donald Trumpo iliamua kuomba kibali cha mahakama ambayo inaitwa US Foreign Intelligence Surveillance Court cha kufanya upelelezi kwa wandishi wote wa habari ambao wanaandika taarifa ambazo zinatokana na habari zilizovujishwa kutokea White House.

Iliaminika kuwa taarifa hizo zilikuwa zikivujishwa na ofisa wa serikali mstaafu, mwenye cheo cha juu ambae alikuwa ni mkuu wa moja ya idara za ujasusi wa Marekani.

Na huyu jamaa alikuwa alipata taarifa hizo kutoka kwa watumishi mbalimbali wa serikali ambao walikuwa chini ya raisi aliepita bwana Barak Obama.

Sasa kuna mtu hapa ametumia reference ya TISS kwamba wanavujisha taarifa na nyaraka.

Je kama ni hivyo je hii imekaa sawa kweli.

Hivi deni ni nyaraka za siri? Unajua maana ya nyaraza za siri?
 
Suala ni kuvujishwa kwa nyaraka za serikali na watumishi wa serikali je, ni halali kulingana na miiko yao ya kazi?

Si halali kabisa. Na hilo SIO SWALI unalotakiwa kuuliza. Hii ni dalili ya "dysfunctional government". ULIZA ni nini hasa kilichoharibika serikalini kufikia hali hii? Na, Serikali ifanye nini kurekebisha hali hiyo?

Halafu, je, ni sahihi Kwa anayevujishiwa nyaraka hizo kuzieneza kwa umma? (Zingatia dhana ya whistleblower). Kama siyo, hatua gani sahihi serikali imchukulie? Majibu hayana budi kuwiana na maslahi mapana ya taifa; si ya kikundi/vikundi vinavyotumia dola kwa maslahi na ustawi binafsi!
 
Tundu Lissu wa Chadema amethibitisha kwamba anazo taarifa na nyaraka mbalimbali ambazo amepewa na baadhi ya watu wanaoaminika kwamba ni watumishi wa serikali.

Tundu Lissu amepewa nyaraka hizi na watu hawa kwa minajili ya kuzitumia kwa manufaa yake yaani kupalilia safari yake kisiasa na kujipatia umaarufu.

Ni hivi majuzi tu raisi wa Marekani Donald Trump alichukua hatua ya kurekebisha hilo ambapo baadhi ya wasaidizi wake wametuhumiwa kuvujisha taarifa mbalimbali kutoka ndani ya White House kwa waandishi wa habari na wapinzani wake.

Taarifa nyingi za serikali zina utaratibu wake wa kuzihifadhi na hupewa jina maalum la "top secret" au "classified information" kuzuia uwezekano wa kudukuliwa au kuibiwa,

Je, sheria inasemaje juu ya hili la kuvujisha taarifa na nyaraka za serikali kwa watumishi wa umma?

Je, yapi majukumu ya mdhibiti mkuu wa nyaraka za serikali na msemaji wa serikali au maofisa habari "information officers" kwamba labda kuna mahali wanapwaya?

Karibu tujadili bila kuingiza siasa.

Tunapojadili tuzingatia umuhimu wa kuhifadhi nyaraka na taarifa za serikali na wajibu wa maofisa habari na mdhibiti mkuu wa taarifa na nyaraka za serikali.
Hivi kitu kama hichi nayo ni top secret au madudu ya serikali,...kuna watu nao wanachoka wanapenda nchi yao hawawezi kaa kuficha madudu, wafiche vitu vyaa maan sio madudu kama haya...tena watumishi kama hawa ndo tunao wataka maan sometimes serikali inapenda sana uongoo usio na tija si wangesema hadharani na hili ili tuwaunge mkono na tuoneshe uzalendo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wee unadhani TISS wanafanya kazi na ccm tu????

Waliotoa hizo secret Info we unadhani ni raia wa kawaida????

Usalama wanafanya hivyo kwa maslai mapama ya nchi.... Huo ndio uzalendo nchi ikija kutaifishwa kwa madeni ya kizembe nani atakae laumiwa?? Serikali, jeshi la polisi, jwtz au usalama nani atakae laumiwa???
Mungu akubariki sana mkuu .
 
Suala ni kuvujishwa kwa nyaraka za serikali na watumishi wa serikali je, ni halali kulingana na miiko yao ya kazi?
Siyo sahihi kabisa ila swala la kujiuliza kwanini inatokea what went wrong, weledi wa kiutawala unatakiwa, nafikiri ni wakati sasa viongozi wetu wa juu wakae kitako na kutafakari kwa kina kujua watumishi wake wanalalamika nini na shida zao ni zipi la sivyo tutakuja kupinduana kama siyo siri kuendelea kuvuja. Mungu bariki Taifa langu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nchi zilizoendelea na kuwa na sheria nzuri hawa watu wana sheria za kuwatetea.

Sheria ya Wamarekani kutetea whistleblowers hii hapa.

Whistleblower Protection Act - Wikipedia

The Whistleblower Protection Act of 1989, Pub.L. 101-12 as amended, is a United States federal law that protects federal whistleblowers who work for the government and report agency misconduct. A federal agency violates the Whistleblower Protection Act if agency authorities take (or threaten to take) retaliatory personnel action against any employee or applicant because of disclosure of information by that employee or applicant. Whistleblowers[1] may file complaints that they believe reasonably evidences a violation of a law, rule or regulation; gross mismanagement; gross waste of funds; an abuse of authority; or a substantial and specific danger to public health or safety.

Sent from my Kimulimuli
Hapa si walileta longolongo bungeni
 
Hapa si walileta longolongo bungeni
Bunge letu ukiiangalia ile sheria ya makosa ya mtandao ni the opposite of whistleblower protection.

Kuna siku niliweka opinion poll hapa, kuangalia watu wanavyo m support Magufuli kwa kura JF.

JF wakaitoa haraka sana. Eti kuna sheria inakataza wao kuwa na poll kama hiyo.

Vitu vya kijingajinga tunavipenda sana.

Sent from my Kimulimuli
 
Kwanza anaacha kazi na pili anatafuta mahali pa kujihifadhi na mwisho anatoa hizo nyaraka.

Mtumishi wa serikali huwa anakula kiapo cha kulinda siri za serikali kama masharti ya kuajiriwa.
Ndio maana Nchi za kiAFRICA zimekuwa na Watawala wajinga Sana....yaani Hata akiona Twiga wanapakiwa kwenye Ndege asiseme Sababu ameapa...duh...
Usifananishe America na Nch zenye watawala wapumbavu Kama huku Africa..ambapo Rais anagekuwa mungu....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa kama unachoshwa unajiondoa na baadae unasemea pembeni badala ya kukiuka maadili ya utumishi wa umma kwa kuvujisha nyaraka na taarifa?
mkuu, kama bosi mkuu mwenyewe anakiuka si maadili tu bali kuvunja katiba kabisa...wengine wafanyeje?

wacha mbwai na iwe mbwai bana hadi kieweleke utawala wa sheria utakapoanza kuheshimiwa tena!!
 
Mtoa mada ungelikuwa unajuwa faida za ma WHISTLEBLOWERS usingekuwa na shaka yoyote
 
Tundu Lissu wa Chadema amethibitisha kwamba anazo taarifa na nyaraka mbalimbali ambazo amepewa na baadhi ya watu wanaoaminika kwamba ni watumishi wa serikali.

Tundu Lissu amepewa nyaraka hizi na watu hawa kwa minajili ya kuzitumia kwa manufaa yake yaani kupalilia safari yake kisiasa na kujipatia umaarufu.

Ni hivi majuzi tu raisi wa Marekani Donald Trump alichukua hatua ya kurekebisha hilo ambapo baadhi ya wasaidizi wake wametuhumiwa kuvujisha taarifa mbalimbali kutoka ndani ya White House kwa waandishi wa habari na wapinzani wake.

Taarifa nyingi za serikali zina utaratibu wake wa kuzihifadhi na hupewa jina maalum la "top secret" au "classified information" kuzuia uwezekano wa kudukuliwa au kuibiwa,

Je, sheria inasemaje juu ya hili la kuvujisha taarifa na nyaraka za serikali kwa watumishi wa umma?

Je, yapi majukumu ya mdhibiti mkuu wa nyaraka za serikali na msemaji wa serikali au maofisa habari "information officers" kwamba labda kuna mahali wanapwaya?

Karibu tujadili bila kuingiza siasa.

Tunapojadili tuzingatia umuhimu wa kuhifadhi nyaraka na taarifa za serikali na wajibu wa maofisa habari na mdhibiti mkuu wa taarifa na nyaraka za serikali.
Hakuna nyaraka za siri zinazohusu wizi, nyaraka itakuwa siri iwapo hakutakuwa na wizi, kama ni hivyo hata escrow tusingeijua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom