Wanaotembea nusu uchi wana lao jambo……….!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,398
Kuna wakati wanaume hudhani kwamba, wanawake wanaovaa nusu uchi huwa wanafanya hivyo kwa sababu ya kutafuta soko kwa wanaume. Inawezekana kukawa na wale ambao wana sababu hizo, lakini wapo wale ambao wanalipa fidia kutokana na kuamini kwao kwamba, sura zao zimewaangusha, hivyo miguu yao mizuri inabidi kuziba pengo au udhaifu huo.

Wakati mwingine hata wanawake wanaodhani au kudhaniwa kuwa ni wazuri, wamekuwa wakivaa nguo fupi zinazoonyesha maungo yao. Hawa nao ni lazima wanalipa fidia ya kasoro fulani waliyo nayo. Inawezekana wameshindwa kulinda ndoa zao, au inawezekana hawajaolewa na sasa wanataka kuonyesha kwamba, pamoja na kutoolewa kwao, bado wao wana sura na miguu au miili mizuri.

Udhaifu wowote ambao unamkera mwanamke iwe ni wa moja kwa moja au kupitia nyuma ya ubongo wake, unaweza kuonyeshwa kwa mwanamke huyo kuyatangaza yale maeneo ya mwili wake ambayo anaamini ni mazuri. Kuyatangaza huko humpa ahueni kwa kuamini kwamba bado anayo thamani, kwani ataangaliwa sana na wanaume, kusifiwa na pengine kutongozwa.

Hebu angalia wanawake ambao wanavaa nguo za kubana huku wakiwa na makalio makubwa. Hawa mara nyingi wana sura ambazo wao au wengi huamini kwamba ni mbaya. Huvaa nguo hizi ili kuonyesha kwamba, pamoja na ubaya wa sura zao, bado wao ni wazuri sana katika maeneo mengine ya mwili ambayo wanaume na hata wanawake wengi huyapenda au kutamani kuwa nayo.

Wengi hawavai tu nguo hizi za kubana kwa sababu ni fasheni, la hasha, wengi hili ni kimbilio la udhaifu wao.
 
habari ndefu zinakosesha raha ya kuzisoma.halafu mwingine anaiquote.mkuu mademu wanashindana wao kwa wao.
 
Hili lina ukweli mkubwa sana,coz mara nyingi udhaifu huwatesana wasiojiamini!
 
Kuna wakati wanaume hudhani kwamba, wanawake wanaovaa nusu uchi huwa wanafanya hivyo kwa sababu ya kutafuta soko kwa wanaume. Inawezekana kukawa na wale ambao wana sababu hizo, lakini wapo wale ambao wanalipa fidia kutokana na kuamini kwao kwamba, sura zao zimewaangusha, hivyo miguu yao mizuri inabidi kuziba pengo au udhaifu huo.

Wakati mwingine hata wanawake wanaodhani au kudhaniwa kuwa ni wazuri, wamekuwa wakivaa nguo fupi zinazoonyesha maungo yao. Hawa nao ni lazima wanalipa fidia ya kasoro fulani waliyo nayo. Inawezekana wameshindwa kulinda ndoa zao, au inawezekana hawajaolewa na sasa wanataka kuonyesha kwamba, pamoja na kutoolewa kwao, bado wao wana sura na miguu au miili mizuri.

Udhaifu wowote ambao unamkera mwanamke iwe ni wa moja kwa moja au kupitia nyuma ya ubongo wake, unaweza kuonyeshwa kwa mwanamke huyo kuyatangaza yale maeneo ya mwili wake ambayo anaamini ni mazuri. Kuyatangaza huko humpa ahueni kwa kuamini kwamba bado anayo thamani, kwani ataangaliwa sana na wanaume, kusifiwa na pengine kutongozwa.

Hebu angalia wanawake ambao wanavaa nguo za kubana huku wakiwa na makalio makubwa. Hawa mara nyingi wana sura ambazo wao au wengi huamini kwamba ni mbaya. Huvaa nguo hizi ili kuonyesha kwamba, pamoja na ubaya wa sura zao, bado wao ni wazuri sana katika maeneo mengine ya mwili ambayo wanaume na hata wanawake wengi huyapenda au kutamani kuwa nayo.

Wengi hawavai tu nguo hizi za kubana kwa sababu ni fasheni, la hasha, wengi hili ni kimbilio la udhaifu wao.

jamani mambo gani tena haya ya kuamshana tamaa?
 
wanawake wanavaaa ili 'kushikishana adabu' wao kwa wao.....

kuoneshana nani 'anajua kupendeza'.....
 
Mimi ninachoamini wanawake wengi wa kiafrika wanfanya kuvaa ngu fupi au za kubana jwa kuiga tu na kama wapo ambao wanamalengo ni wachache sana inaweza ikawa hata chini ya 10% ya wanaovaa ivyo
 
Sikubaliani na matumizi yako ya ''wengi''...''mara nyingi'' kwasababu ulichofanya ni kuassume na kushutumu ila ukweli haugusu hata nusu ya asilimia unayoongelea.

Watu unaoongelea wewe ni wale wasiojiamini....but again mtu asiyejiamini hata kuvaa nguo inayobana sana ama fupi kwake ni tabu kwasababu bado atakua hajiamini na ataishia kujishtukia kila atakapoangaliwa na mtu mwingine.
Uvaaji wa mtu unareflect level ya kujiamini kwake na kujikubali kwake.Tatizo ni kwamba wengine mmejiaminisha kwamba kila anachofanya mtu mwingine anafanya kwaajili ya waliomzunguka kwasababu ndivyo mlivyojifunza/ndivyo mlivyo. Mnasahau kwamba kuna watu ambao ''they are all about self satisifaction''. Akipaka wanja ni kwasababu yeye anapenda/anaona unampendezesha...akivaa viatu virefu ni kwasababu anaamini vinampendeza ...akivaa kimini ni kwasababu anapenda kinavyomkaa or just the sight of he legs in it...akivaa surualI inayombana ni kwasababu anapenda au inaendana na mazingira ya shughuli zake and so so.

Mf. mimi wakati nakua nilikua sivai magauni isipokua siku ya xmass because all the other girls looked dressy and I didn't wanna be left out...nakumbuka hata kwenye ubarikio wa dada yangu sikutaka kuvaa gauni nikanunuliwa suruali na shati vinavyofanana ,yote kwasababu mimi nilikua napenda. Ila nilivyoenda kusoma Moshi watoto wengine wakawa wananicheka na kunitania kwamba navaa kama mvulana kwasababu ndivyo walivyofundisha na kuamini....suruali/kaptula ni nguo za wavulana.Nikaacha kabisa kuvaa suruali hata nilipokua likizo mjini mpaka nilipofikisha miaka kumi na tatu. Then nikaamua kwamba napenda suruali na ntavaa bila kujali watu wengine wanafikiria nini kwasababu mimi napenda na ni practical kwangu...nikitaka kukimbia/kucheza najiachia bila kujali sketi/gauni langu kupanda. Pia nikijisikia kuvaa gauni/sketi navaa kwasababu napenda na sio kumfurahisha yeyote kama nilivyofanya hapo nyuma. It's all about me...me....me..me and no one else.

Sasa wewe unaposhutumu watu eti wanavaa nguo fupi/zinazobana/suruali kwasababu ya madhaifu (sijui sura mbaya and the likes) unanishangaza. Usimjudge mtu kabla hujajua namna yake ya kufikiri ....sababu ya kufanya afanyayo kwasababu wewe sio mtaalamu wa kujua mawazo na nia zao. Uliza...ili ukisema kitu kuhusu mtu hata kama ni mmoja uwe na uhakika na unachokisema.

Na hapana sikatai kwamba wapo wanaovaa kwa kufuata mkumbo ama kujionyesha ila sio wengi kama unavyotaka tuamini.
 
Sikubaliani na matumizi yako ya ''wengi''...''mara nyingi'' kwasababu ulichofanya ni kuassume na kushutumu ila ukweli haugusu hata nusu ya asilimia unayoongelea.

Watu unaoongelea wewe ni wale wasiojiamini....but again mtu asiyejiamini hata kuvaa nguo inayobana sana ama fupi kwake ni tabu kwasababu bado atakua hajiamini na ataishia kujishtukia kila atakapoangaliwa na mtu mwingine.
Uvaaji wa mtu unareflect level ya kujiamini kwake na kujikubali kwake.Tatizo ni kwamba wengine mmejiaminisha kwamba kila anachofanya mtu mwingine anafanya kwaajili ya waliomzunguka kwasababu ndivyo mlivyojifunza/ndivyo mlivyo. Mnasahau kwamba kuna watu ambao ''they are all about self satisifaction''. Akipaka wanja ni kwasababu yeye anapenda/anaona unampendezesha...akivaa viatu virefu ni kwasababu anaamini vinampendeza ...akivaa kimini ni kwasababu anapenda kinavyomkaa or just the sight of he legs in it...akivaa surualI inayombana ni kwasababu anapenda au inaendana na mazingira ya shughuli zake and so so.

Mf. mimi wakati nakua nilikua sivai magauni isipokua siku ya xmass because all the other girls looked dressy and I didn't wanna be left out...nakumbuka hata kwenye ubarikio wa dada yangu sikutaka kuvaa gauni nikanunuliwa suruali na shati vinavyofanana ,yote kwasababu mimi nilikua napenda. Ila nilivyoenda kusoma Moshi watoto wengine wakawa wananicheka na kunitania kwamba navaa kama mvulana kwasababu ndivyo walivyofundisha na kuamini....suruali/kaptula ni nguo za wavulana.Nikaacha kabisa kuvaa suruali hata nilipokua likizo mjini mpaka nilipofikisha miaka kumi na tatu. Then nikaamua kwamba napenda suruali na ntavaa bila kujali watu wengine wanafikiria nini kwasababu mimi napenda na ni practical kwangu...nikitaka kukimbia/kucheza najiachia bila kujali sketi/gauni langu kupanda. Pia nikijisikia kuvaa gauni/sketi navaa kwasababu napenda na sio kumfurahisha yeyote kama nilivyofanya hapo nyuma. It's all about me...me....me..me and no one else.

Sasa wewe unaposhutumu watu eti wanavaa nguo fupi/zinazobana/suruali kwasababu ya madhaifu (sijui sura mbaya and the likes) unanishangaza. Usimjudge mtu kabla hujajua namna yake ya kufikiri ....sababu ya kufanya afanyayo kwasababu wewe sio mtaalamu wa kujua mawazo na nia zao. Uliza...ili ukisema kitu kuhusu mtu hata kama ni mmoja uwe na uhakika na unachokisema.

Na hapana sikatai kwamba wapo wanaovaa kwa kufuata mkumbo ama kujionyesha ila sio wengi kama unavyotaka tuamini.

Ulichofanya ni kujitetea sana dadaangu lizzy...
NI ngumu sana kujustify kitu kwa kujitumia wewe mwenyewe kama mfano lazima utakuwa 'biased'!!..
 
hili sredi wazee kama siye kina ODM huwa tunakaa pembeni kuangalia linachangiwaje.

Tukishajirizisha tunaanza kuchakachua.
 
Ulichofanya ni kujitetea sana dadaangu lizzy...
NI ngumu sana kujustify kitu kwa kujitumia wewe mwenyewe kama mfano lazima utakuwa 'biased'!!..

Siwezi kujitetea kwasababu sie niliyeshutumiwa....nilichofanya ni kuonyesha kwamba sio kila mtu anafanya mambo kwa kuangalia fulani...na fulani...na fulani.Pia siwezi kua biased...na ndio maana mwishoni nimeonyesha kwamba naelewa wapo watu wa aina inayoongelewa ila sio ''wengi'' wala haitokei ''mara nyingi'' kama mtoa mada anavyopendekeza.
 
afadhali mkuu umenipa mwanga. kumbe wanafanya kubalance. kwa mfumo huu nakumbuko msemo wa mzee mmoja kijijini kwetu aliniambia kua "ipo cku sisi wanume tutajuta kuzaliwa wanaume kwani kila kukicha wanawake wanakuja na mitindo mipya ya kutuingiza ktk mitego yao" sikumuelewa kwa kipindi hicho ila sasa naanza kuelewa kwani wakati mwingine unajikuta umeingia ktk vishawishi bila hata kujiandaa.
mhhhh. haya
 
Back
Top Bottom