Wanaomkosoa Magufuli wako mtandaoni tu

Wanaomkosoa Magufuli wako mtandaoni tu

Sijui kama mmegundua hili? Wale vidampa wanaomkosoa Magufuli wengi wao wamejibanza mtandaoni tu na hasa Jamiiforums.

Mtaani mambo ni tofauti sana. Watu wanamkumbuka sana Jemedari wa vita (chuma cha pua) kwa mambo mengi mema aliyoyafanya.

Hawa vidampa na mafisadi sugu waliojibanza mitandaoni ndio wanaorusha vijembe dhidi ya Magufuli.

Unakuta fisadi moja linamiliki ID's saba zenye maudhui na malengo mfanano ya kumchafua jemedari. Kazi yake ni kubwata na kufoka.

Fisadi lenyewe limebebelea mavyeti feki. Eti na lenyewe linataka ajira!

Nitoe indhari kwa Rais Samia awe makini sana na hawa mafisadi sugu. Wengi wao ni wale oya oya wanaopenda kudoea doea, kupiga madili na kufanya ujanja ujanja.

Ahsante.
Halafu wengi wao wameajiriwa wanalipwa mshahara
 
mkaanzishe serikali yenu huko mavumbini na wewe mleta mada uteuliwe kuwa waziri wa mizizi
 
Back
Top Bottom