Wanaomkosoa Magufuli wako mtandaoni tu

Wanaomkosoa Magufuli wako mtandaoni tu

Sijui kama mmegundua hili? Wale vidampa wanaomkosoa Magufuli wengi wao wamejibanza mtandaoni tu na hasa Jamiiforums.

Mtaani mambo ni tofauti sana. Watu wanamkumbuka sana Jemedari wa vita (chuma cha pua) kwa mambo mengi mema aliyoyafanya.

Hawa vidampa na mafisadi sugu waliojibanza mitandaoni ndio wanaorusha vijembe dhidi ya Magufuli.

Unakuta fisadi moja linamiliki ID's saba zenye maudhui na malengo mfanano ya kumchafua jemedari. Kazi yake ni kubwata na kufoka.

Fisadi lenyewe limebebelea mavyeti feki. Eti na lenyewe linataka ajira!

Nitoe indhari kwa Rais Samia awe makini sana na hawa mafisadi sugu. Wengi wao ni wale oya oya wanaopenda kudoea doea na kufanya janja janja.

Ahsante.
Hawa wanaomkuosoa Magu wanajikosoa. Kwani alishafunga kitabu chake. Tusipoteze muda na Magu. Kufanya hivyo, ni kuzidi kuwapa hawa Mangungo fursa ya kutuchuuza utumwani kwa waarabu na wazungu na magabacholi
 
Asante sana,

Hayo maua - maua halisi, this is no mere figure of speech- mimi tayari nina pink rose bush hapa nyumbani ninapoishi, linachanua vizuri in the spring. Pia nina red rose bush kubwa sana in Bronx, New York. Nilipanda kwenye nyumba yangu ya Bronx miaka mingi sana iliyopita.

Mimi kila nikijenga au kununua nyumba kitu cha kwanza najipa ni maua au mti wa matunda, kwa hivyo, ukiniongezea nashukuru, lakini, usiponipa, nishapanda maua mwenyewe kwenye nyumba zangu.

Moja ya vitu nilivyojifunza katika maisha ni ku appreciate vitu kama flora and fauna, huu ni utajiri kuliko pesa.

Umenifanya kufikiria kuanzisha thread ya vitabu ninavyosoma, kuvifanyia review, na kusikiliza wengine walisoma wanavifikiriaje.

Nafikiri thread hiyo, tukiwa na inclusivity nzuri, na kuondoa obvious troll, tunaweza kuwa na mazungumzo mazuri.

Wiki hii nilikaa na wachumi fulani, wakanipa mrejesho wao kuhusu kitabu fulani nilichokuwa nakiona kizuri sana kuhusu uchumi, halafu, kutokana na mrejesho wao, nikakiona tofauti kabisa, nikajifunza mambo mengi kutoka kwao.

Kwa hivyo, kama utapenda tuwe na threads fulani za kujadili vitabu na articles fulani, ambazo naona ni muhimu, naweza kuanzisha series hiyo.


Mimi binafsi napenda sana kaka. SIYO mimi tu namini pia wapo wanaopenda uwepo wako HAPA. Tunaomba kama utaweza ufanye hivyo kaka. Tutajifunza mengi sana.
 
Hawa wanaomkuosoa Magu wanajikosoa. Kwani alishafunga kitabu chake. Tusipoteze muda na Magu. Kufanya hivyo, ni kuzidi kuwapa hawa Mangungo fursa ya kutuchuuza utumwani kwa waarabu na wazungu na magabacholi
Mkuu,

Jaribu kufikiri kwamba maisha ya Magufuli, mtu aliyekuwa public figure, yana mafunzo kwa wengine, na kwa kuyaangalia mabaya au mazuri yake, wengine wanaweza kujifunza.

Ndiyo maana watu wanasoma history, wanasoma ma Pharaohs, Caesar,Caligula, Napoleon, Hitler.

Kuna mambo ya kujifunza kutoka kwenye maisha yao.
 
Back
Top Bottom