Wanaoharibu Bunge ni Kina Nani?

Wanaoharibu Bunge ni Kina Nani?

Mimi nadhani katika multiple choice yako jibu ni "B" yaani wabunge wa upinzani baaasi!! nitaishia hapo. Lakini ukitaka nifafanue zaidi ni kwamba Kabla hatujaingia kwenye Siasa za vyama vingi bunge letu lilikuwa halina mgongano wowote kila kitu kilikuwa kinapita kwa 100% na tulizoea kelele zozote bungeni zilikuwa ni za kupongezana na kugonga meza. Lakini baada ya kuingia Siasa za vyama vingi hasa kipindi hiki ambacho wamepatikana watu wanaozijua sheria na wajibu wao kama wabunge mfano watu kama Tundu Lisu, Mnyika, Machali na Mkosamali wamekuwa wakiisumbua sana Meza ya Spika.

Kutokana na Kiti cha Spika kutokuzoea hizi changamoto za kuhojiwa hojiwa hivyo kimeamua kutumia nguvu ili kukilinda chama tawala dhidi ya fedheha kwa wananchi inayopelekea wapinzani pia kupatwa na hasira kutokana na ukandamizaji huu hivyo kusababisha haya yanayotokea Bungeni kutokukiheshimu tena kiti cha Spika. Hebu chukulia mfano Hasira za Ndugai kumtoa nje Tundu Lisu kwasababu tu anasimama mara nyingi kuomba muongozo na kuitafsiri kama ni fujo je sheria zinasemaje kuhusu mtu kuomba mwongozo? zimeweka kikomo? Kwahiyo wanao lihalibu Bunge to me ni Wabunge wa Upinzani Watanzania hatukuzoea watu CRITICAL.

Mkuu wa kwa maelzo yako haya mazuri ni dhahiri sasa jibu ni A...na siyo B. kwa sababu hao ndiyo hawajazoea changamoto kama unavyosema..
 
'A' yaweza kuwa sahihi zaidi.

Naona wachangiaji wengine wanajibu zaidi ya jawabu moja hivyo nami naongezea, hii attachment pia ndio inafanya wale wa 'class A' na 'wafuga mbwa' kushindwa kuainisha kilichomo ndani ya mafuvu yao.
View attachment 90546

Kwa mwenye akili ndogo hii ni ngumu sana kueleweka kwake...
 
Naibu spika haenei kwenye kiti chake kwa hiyo as a defensive mechanism anaamua kutoa maamuzi ya kipumbavu yanayotokea kwenye kichwa chake ambacho pia nahisi ni kibovu badala ya kufwata kanuni. Wabunge wa CCM wanatia hasira sana kwa mtu yoyote mwenyeakili timamu kutokana na yale wanayoyafanya bungeni, hasa kwa kukubali mambo ya kipuuuz kupita, suala kama la kutenga 1 Bilion kwa ajili ya kumzika Lukuvi badala ya kuielekeza fedha hiyo kwenye kuwasaidia wananchi waliohai.

Baada ya kusema hayo A na C ndio wanaotuharibia Bunge. Ikumbukwe kuwa kazi za wabunge ni kuisimamia Serikali na sio kuilinda serikali na wabunge kuwa ndio wasemaji wa serikali. Na Pia ni kuwakilisha mawazo na interests za wapigakura wao Bungeni, kwa wanayoyafanya wabunge wa ccm cdhani kama yanalenga kumfaidishwa mwanakijiji wa songambele au Msanga!!

Mawazo mazuri sana haya..kuna wachache sana ndani ya chama tawala wanaotambua wajibu wao
kama kina Fulikunjombe na Kina Bwana Mpina...Chama tawala waige kutoka kwao ambao ni wenzao
 
Spika na naibu wake hawa wanatakiwa kuwa neutral lakini unaona kabisa wako kiccm zaidi
 
Mkuu wa kwa maelzo yako haya mazuri ni dhahiri sasa jibu ni A...na siyo B. kwa sababu hao ndiyo hawajazoea changamoto kama unavyosema..

Tehe tehe!! mimi bado nahisi tatizo ni Wabunge wa upinzani ndiyo wanaoharibu Bunge letu na ninaamini tukiwang,oa meno na kuwatupa Mabwe pande ukimya utarudi tena Bungeni.....lol
 
Wabunge na viongozi wa bunge wasio na uchungu na umasikini ujinga na maradhi ya watanzania,wasiojiamini na waliopewa uongozi kama zawadi!!

mtu mwenye dira na malengo ni mwenye ujasiri hekima akili mvumilivu na mwenye kutetea hoja za kitaifa badala kuwa shabiki tu wa mambo au watu fulani huyu ni mnafiki na mvivu na hatari sana kwani agenda yake ni kumfurahisha tu yule aliyemzawadia cheo au ubunge!!!

Nachukizwa sana na watu wa namna hii na ni 85% ya viongozi wetu.


Namfagilia sana Marehemu Sokoine pamoja na kuwa alikuwa elimu ndogo lakini alisimamia maamuzi yake
 
Kwa mwenye akili ndogo hii ni ngumu sana kueleweka kwake...
na ndio chanzo cha matatizo yetu.
Leo asubuhi nilikuwa nafualia hii link cnn, hawa ndio watu walioachia wananchi wao kufikiri na sasa wanafikiri juu ya makazi nje ya dunia yetu lakini hapa tunaendelea kungangania wajinga wengi kuwakandamiza waelevu wachache ambao wangeliweza kutwambia ukweli wa ni kwa nini tuna rasilimali nyingi hivi lakini sio masikini tu bali hata chakula hatuna tunakufa na utapiamulo. Hivi sasa namsikia 'mchumi grade 1' akiseme mishahra ya walimu (ambayo ni 200,000+ hivi) haiwezi kupanda kwa 50% wakati yeye anakula 10m.

 
Chadema wanaharibu Bunge.

Mbowe kashindwa kuongoza upinzani.

Wabunge wa chadema wanajiendea tu kama mbuzi wa Vingunguti wasio na mchungaji.

Hamad Rashid aliongoza vizuri zaidi upinzani Bungeni katika Bunge la tisa.

Ndio maana hajaendelea kuwa kiongozi wa Upinzani....hii ni kama kusema flani alikuwa anajisomea vizuri na kuyamudu masomo vyema wakati amefeli!
 
Umeongea point mkuu hawa vijana wanageuza bunge ni sehemu ya kampeni.

Hao ambao hawajaligeuza jukwaa la Kampeni wanafanya nini...kuna thread inasema nyota ya mh....yang'ara jaribu kuisoma utaelewa...
 
Tehe tehe!! mimi bado nahisi tatizo ni Wabunge wa upinzani ndiyo wanaoharibu Bunge letu na ninaamini tukiwang,oa meno na kuwatupa Mabwe pande ukimya utarudi tena Bungeni.....lol

aisee mkuu uking'oa mmoja wanaibuka kumi wakali zaidi...
 
Ndio maana hajaendelea kuwa kiongozi wa Upinzani....hii ni kama kusema flani alikuwa anajisomea vizuri na kuyamudu masomo vyema wakati amefeli!

aisee huu ujumbe unaendana kabisa na hili swala..anajisomea vizuri na kuyamudu masomo vyema wakati amefeli
 
Kila sehemu sasa, ni mazungumzo ya Bunge na Utovu wa Nidhamu...
Kila mtu anazungumza...

Hata hapa mengi sasa ni kuhusu Bunge..
Wanaoharibu sasa ni kina nani?

A. Spika na Naibu Spika

B. Wabunge wa Upinzani

C. Wabunge wa CCM

D. Wote


Tungepata Poll hapa ingependeza zaidi...

Nchi sasa inalijadili Bunge...


Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania limekosa spika. Linaendeshwa kwa kufuata itikadi za kichamachama tu (CCM). Kiujumla Anna Makinda amedhihilisha kuwa Tanzania kuongozwa na Mwanamke inahitaji miaka mingi sana. Labda tunahitaji karne nzima. Haiwezekani mbunge wa CCM akitukana ni sawa; lakini mbunge wa upinzani hata akiteleza ulimi tu nnje. Matusi ya wazi kabisa yanatolewa na wanaccm lakini nothing is happening. Spika amelishushia heshima bunge letu.

Sipati picha siku raisi wa Jamuhuri wa Tanzania akiwa mwanamke itakuwaje. Sina hamu kabisa na bunge la Jamuhuri ya Muungano Tanzania.
 
kwa hapa jf huwezi kupata jibu sahihi kwa sababu hatuko objective bali tuna mahaba na vyama vyetu
 
Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania limekosa spika. Linaendeshwa kwa kufuata itikadi za kichamachama tu (CCM). Kiujumla Anna Makinda amedhihilisha kuwa Tanzania kuongozwa na Mwanamke inahitaji miaka mingi sana. Labda tunahitaji karne nzima. Haiwezekani mbunge wa CCM akitukana ni sawa; lakini mbunge wa upinzani hata akiteleza ulimi tu nnje. Matusi ya wazi kabisa yanatolewa na wanaccm lakini nothing is happening. Spika amelishushia heshima bunge letu.

Sipati picha siku raisi wa Jamuhuri wa Tanzania akiwa mwanamke itakuwaje. Sina hamu kabisa na bunge la Jamuhuri ya Muungano Tanzania.

umechangia kwa chuki dhidi ya gender ya ke.....hufai kuwa great thinker.

umechangia kwa kuzingatia mahaba ya chama chako. hufai kuwa great thinker.

umechangia bila kuangalia matusi na lugha za wabunge wa vyama vyote waliotoa matusi..hufai kuwa gt. hapa lazima tuache ukereketwa wa kichadema na kiccm ndio jibu sahihi litapatikana
 
Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania limekosa spika. Linaendeshwa kwa kufuata itikadi za kichamachama tu (CCM). Kiujumla Anna Makinda amedhihilisha kuwa Tanzania kuongozwa na Mwanamke inahitaji miaka mingi sana. Labda tunahitaji karne nzima. Haiwezekani mbunge wa CCM akitukana ni sawa; lakini mbunge wa upinzani hata akiteleza ulimi tu nnje. Matusi ya wazi kabisa yanatolewa na wanaccm lakini nothing is happening. Spika amelishushia heshima bunge letu.

Sipati picha siku raisi wa Jamuhuri wa Tanzania akiwa mwanamke itakuwaje. Sina hamu kabisa na bunge la Jamuhuri ya Muungano Tanzania.

mkuu hapo kwenye red, kuita watu mahanithi ni kuteleza ulimi???? kutumia biblia kutukana watu ni kuteleza ulimi???? acha ujinga..halafu sio wabunge wa upinzani ni wabunge wa chadema ndio wanaotukana na wanafahamika
 
iko wazi kwamba wabunge wa chadema ni tatizo lakini kwa sababu tumevaa upofu hatuwezi kuliona hili..
 
Wanaoharibu bunge ni wavuta bangi watoto wa kijiweni waliochaguliwa bungeni kwa jina la upinzani
 
baadhi ya wabunge wa chadema ni mzigo kwa chama na wanakiharibia...huo ndio ukweli mchungu
 
Back
Top Bottom