Nape najua ni kijana mdogo ambaye anajipambanua kama kijana wa wakati huu. Mwanasiasa anayedai amejijenga kwa nguvu zake mwenye, wakati mwingi akidai wazee ndio sababu ya kuzorota uchumi na kuanguka kwa maadili makubwa ya uongozi.
Nape amekuwa kijana ambaye anathibitisha elimu, maadili, utu na heshima kwa watu anaotaka kuja kuwaongoza hana. Nape anatakiwa atafakari sana kwa nini ameshindwa kuchaguliwa hata na kundi dogo la wanachama wake kupeperusha bendera ya chama chake Ubungo-Ulimi wenye dharau, sifa, majivuno, kujiamini kupindukia na sasa kuwatukana watanzania.
Nape unasema leo vinyago ndio wanatoka CCM, umewahi kutumia maneno kama kushikishwa ukuta, ukanda, ukabila nk. Naona inakubidi urudi shule usome nini maana ya kuwa kiongozi wa umma kiongozi unayetegemea kuongoza watu, mwana siasa wa kizazi cha sasa karne ya 21 na kuendelea.
Ulimi kaka utakuponza sana, kuliko hata hao wazee unaowaona hawana akili.
Najua utajisikia vibaya, lakini ninyi hamuharibu tu chama chenu mnataka taifa la matusi, dharau na udhalilishaji. Ukijaribu kuangalia maneno unayotumia wewe , Wasira, Lusinde, Nchemba nk yanasikitisha sana.
Watanzania hawatakubali kutukanwa kwa sababu yeyote ile. Ni haki ya mtanzania kuwa CUF, TLP, CCM, CDM, TADEA Nk na kupewa heshima na haki yake. Hakuna mtanzania kinyago hata kama serikali ya CCM imenyima haki zake za msingi ili imeone kinyago. Ukinyago wa watanzania ni wakutengeneza ndio watanzania wanaonekana vinyago wanapodai, shule bora, maji, barabara, huduma bora za afya maisha bora na utekelezaji wa makusanyo ya kodi zao.
Nape siasa sio matusi
Chief Mkwawa wa Kalenga- Ukiishiwa sera hutukana-ndio kauli za kushindwa