Super Sub Steve
JF-Expert Member
- Jul 9, 2011
- 17,647
- 11,227
Hakuna Chema toka CCM kwa sasa.
Yaani kwa wanamtwara sio Makongoro tu kwa Wana Mtwara CCM ni tatizo ni janga inapaswa wasiisahau,ni juzijuzi tu wameonja shida wameishi kama wapo enzi za ukoloni wa Mjerumani,Mtwara kulikuwa hakuna uhuru,hakuna kukaa katika vikundi vya mijadala kwa kweli nakusapoti Asilimia mia Moja wakiona mtu yeyote wa CCM inabidi wapaze sauti kubwa ya kumkataaa.wana Mtwara Say No to CCM
Mada umeiona lakini kwenye post namba moja? au wewe umeniona mimi tu?
Waliuliwa na Simba au waliliwa na Simba? Ulikuwapo wakati wanaliwa? Na kama ulikuwepo, ulifanya nini ili kuwasaidia?
Prof. Kazilahabi kwenye kitabu chake cha Gamba la nyoka anasema "hilo zoezi lilikuwa kama kukamua usaha."
Ukiuacha, unauma na ukiukamua, unalea maumivu. Ukichema nchale, ukimumunya nchale, ufanye nini?
Leo hii Gas inapatikana, itakuwa rahisi kupata huduma vijijini kuliko wangeliachwa waishi kama Wamongolia.
Ukisikia kiongozi lazima awe na uwezo wa kuamua majukumu magumu, ndiyo alikuwa Nyerere.
Kwamba walikuwepo watu fulani Mataahira na wazembe kama Mzee Ruksa aliyeanza kuuwa vikongwe huko Shinyanga, hilo ni swala jingine. Kwenye operation kubwa kama hizo, makosa lazima yatokee. Vijiji vilianza na tumesoma wengi wetu humu ndani. Nyie mmeanzia shule za kata, hahahahaaa shule za kata.
![]()
Nimeielewa vizuri sana,Urais ni taasisi kama hujui na hapo CCM hamkwepi.Soma vizuri mada, uelewe nani aliwalisha kwa simba wana Mtwara, usirushe.
Mbona sikuelewi hoja yako ni nini haswa ya kwamba unapinga kwa Wanamtwara hawakudhuriwa na Simba kwenye hivyo vijiji walikosombewa ambavyo havikutayarishwa kuishi binadamu?
chuki dhidi ya nyerere haitawafikisha popote.....mpende msipende ndo baba wa taifa la Tanzania period...kwani simba alikuwa anawatuma yeye..mbona maeneo mengi ya tanzania watu wanaliwa na simba hadi leo...na nyerere hayupo...acheni chuki...
Hayo angesema FaizaFoxy angeambiwa "mdini" analeta "udini".
Kwan sera ya villagilization ilikuwa mbaya kuwen waungwana..nyerere asingefanya ivo tanganyika ya leo ingekuwa vipande vipande
Pouwa!
Kwan sera ya villagilization ilikuwa mbaya kuwen waungwana..nyerere asingefanya ivo tanganyika ya leo ingekuwa vipande vipande
Unajua kusema kweli linapokujagaHayo angesema FaizaFoxy angeambiwa "mdini" analeta "udini".
Unajua kusema kweli linapokujaga
suala la dini,tunatakiwa kuwa makini kwenye kuchangia,
Mjadala wa huyu jamaa unaona uko neutral
ni wa kitaifa zaidi,lakini angesema ''Nyerere alisababisha
waislam wa mtwara waliwe na simba''
tungemnanga na tungesema ni mdini.
Sasa pitia mijadala yote uliyochangia ukaitwa mdini
ipitie mara mbili-mbili utakuta element za udini
na hizo kila mtanzania aliyeiva lazima azipige vita.
Lakini sehemu nyingine mbona unachangia vizuri
na watu wanakupa LIKE?