Wanajeshi watoa kichapo mandela road

Wanajeshi watoa kichapo mandela road

Wanajeshi wetu wanapenda sana uonevu na ubabe usio na msingi kwa raia wa kawaida
 
Halafu huwa hawachukuliwi hatua zozote za kinidhamu jeshini kwao. Sijui na wakuu wao wanaunga mkono huu upuuzi wa hawa kuruta? Nawachukia sana hawa watu
 
mhhhhh huyo mjeda labda afe ila ninavyojua mn kazima aje na wenzake walipize kisasu
 
Leo kuna foleni kali hasa kwa magari yatokayo ubungo kwenda buguruni.

Tulivyo vuka daraja la matumbi tukasikia kin'gora kumbe ni Magari ya wana jeshi yamebeba zana za kivita wanatumia barara itokayo buguruni kwenda ubungo wao wamefanya kinyume .

Sasa kuna gari zikawa zinakuja MP wakateremka ili magari yakae kando heee kumbe dereva wa gari ndogo alikua amepaki gari pembeni si mjeshi mmoja akaanza kumtandika hadi basi. Tukio nimeliona vizuri sema picha nilishindwa kuchukua.

Wanajeshi siku zote huwa wana kiburi na kitu kidogo tu huwa wanapiga hawana cha onyo.
Ndio mkiambiwa jipangeni vizuri kwa kuweka mfumo mzuri wa serikali kiepuka hayo, mnasema ohoo...... Mnatishwa...... Haya sasa
 
ni uonevu huu, hawa wanatakiwa wakutana na trafic waliopinda kama yule wa mwaka 2011....
heshma ni kitu cha bure.tusitumie cheo kama kunyanyasa watu...kwenye uonezi kujitetea muhimi.nadhani huyo ni fundisho asifikiri kila mtu na askari wa kuomuonea,kuna wengine si askari lakini ni balaa
 
Acha wapige tu maana CCM Ainawapigia upatu wachukue nchi, acha tuzoee kwata.
 
Wanatumika ki-Siasa..Wanajua kabisa wakifanya hivyo watu wataingia uoga..Sababu ni serikali mbili..

Huu mchezo hata Zanzibar wanautumia sana kipindi cha kampeni..

Rais na Lukuvi Wametoa matamko ...Hayo ni maagizo kutoka juu..
 

Mwanajeshi kupiga raia ni stori,raia kupiga mwanajeshi ni stori ya kusisimua.

Hawa jamaa wanatumia batiki zao kunyanyasa raia.
 
kama wana hamu na vita si wapindue inchi waone muziki wake,yatakuja majeshi ya kigeni ndani ya wiki 1 tu watanyoosha mikono juu wanatuletea usengerema raia tu
 
Halafu huwa hawachukuliwi hatua zozote za kinidhamu jeshini kwao. Sijui na wakuu wao wanaunga mkono huu upuuzi wa hawa kuruta? Nawachukia sana hawa watu
ndyo mkulu anadai mkipendekeza serikali 3 atawakabidhi labda ndyo wanaanza kutoa onyo
 
Hakuna jeshi lolote duniani linaweza kushinda nguvu ya umma, labda Kama wananchi ni mazezeta.
 
Hata mm niliwaona tena walipofika Riverside pale wakatutana na foleni, wahakama barabara na kuvamia ya magari yatokayo Buguruni kwenda Town. Tena zilikuwa ni mizinga za Kizamani sana. Kwa nini wasisafirishe usiku vitu vya usalama wa nchi? Tanzania ina wageni wengi wa holela, wakiwemo Al Shabab, Al-kaida,etc. Kila mara kupiga raia utadhani ni sifa nzr. Kama wanabeep JK awapeleke Afghastan waone mziki wake!!!
 
Wakistaafu wanatuomba 200 mtaani

umeongea point sana mkuu, huwa wanajeshi wastaafu wanakuwa wapole sana huku kitaa tena wengi huingia kwenye ulokole, tupigane na maisha na sio kupumbazika uwepo na kicheo fulani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom