baba-mwajuma
JF-Expert Member
- Feb 1, 2014
- 2,710
- 4,450
Sijasema kama Taliban sio waovu, ila ni ujinga kudhani Jeshi la marekani ni watu wema, kwanza wao ndio waliokaa Meza moja Na taliban muda si mrefu kabla ya kutangaza wanaondoka, hujui walikubaliana nini mpaka wameamua kuondoka Afghanistan.Walitoroka waafghani wangapi wamarekani walipovamia nchi yao? Wapiganaji wa Taliban wapo nje ya uwanja wa ndege, wakipiga risasi hewani. Bila kuzingatia kwamba kuna watoto ndani ya umati wanaojaribu kuutawanya. Hao watoto watakumbuka nini kuhusu watawala wapya wa nchi yao?
Na nimweka link huko juu, naiweka tena hapa, huyu ni mwanajeshi wa marekani amefungwa kwa kutoa Siri za jeshi, jinsi walivyo kuwa wakiua wananchi wasio na hatia huko Afghanistan
Former intelligence analyst sentenced to prison for drone program leak
Air Force intelligence analyst gave military documents to journalist to ‘dispel the lie that our lives are worth more than theirs’
www.theguardian.com
Huo ni ushahidi kutoka ndani ya Jeshi lenyewe.
Lakini pia kuna report mbalimbali toka vyombo vya habari vikubwa duniani namna wanavyopiga shule, harusi na mikusanyiko mingine
Hii incidence ya 2008 harusi ilipigwa bomu na wa marekani watoto 23 walikuwa na wanawake 10, wanaume 4 tu.
Wech Baghtu wedding party airstrike - Wikipedia
en.m.wikipedia.org
Haska meyna nako Harusi nyengine ilipigwa Bomu wanawake 39 na watoto 8 hakukuwa na mwanamme mtu mzima hata mmoja
Haska Meyna wedding party airstrike - Wikipedia
en.m.wikipedia.org
Kwa mwaka maelfu ya watoto wanakufa, toka 2005 zaidi ya watoto 26,000 wamepoteza maisha sababu ya Jeshi la marekani kuingilia Nchi za watu zisizowahusu.
Afghanistan war: 26,000 Afghan children killed or maimed since 2005
An average of five children have been killed or wounded every day, Save the Children says.
www.bbc.com
Leo hii eti unapost kipicha kimoja mwanajeshi kamshika mtoto, unasahau mamilioni ya watu walioharibiwa maisha, maelfu ya watoto waliouliwa, wengine kama hivyo wanauliwa harusinI, unapata wapi Guts za kutetea uovu kama huu?