Wanafunzi UDOM wanalazwa wengi vyumbani na kuhamishwa usiku sababu ya ukarabati wa miundombinu

Ajaye

JF-Expert Member
Sep 25, 2020
319
595
Wakuu Habari za muda huu.

Wiki kadhaa zilizopita University of Dodoma iliripotiwa kuwa na matatizo ya kunguni wakajitetea haikuishia hapo kuna mwenzetu mmoja alitoa mada juu ya uchafu wa vyoo na miundombinu ya maji taka.

Sasa leo hii wakuu, College of Business Studies and Law CBSL, wanafunzi wanalala 10 au zaidi kwenye chumba kimoja, wanafunzi wanahamishwa usiku kutoka hosteli moja kwenda nyingine.

Sababu yao ni ya msingi sana kuwa wanaanza ukarabati wa miundombinu wakati huu, sasa katika hili nina maswali kwenu UDOM;

Mosi, Miezi zaidi ya mitatu wanafunzi walikuwa wamefunga vyuo kwenda kwenye field practical, katika kipindi chote hicho mlishindwa kufanya ukarabati wa vyoo na moundombinu ya majitaka mpaka muanze ukarabati kipindi wanafunzi wamefungua chuo tena wiki hii?

Mbili, kama mlishindwa kufanya wakati huo tajwa hapo juu kwanini msitafute suluhu ya malazi kwanza kwa wanafunzi kisha muanze kuwaondoa? Kuliko kuwabananisha kwenye chumba kimoja wanafunzi zaidi ya 10? Serikali ya wanafunzi mpo wapi?

Professor Mkenda Wasaidie wanafunzi wa UDOM maana ukaguzi wako uliofanyika miezi kadhaa iliyopita pale UDOM haujazaa matunda yoyote yale.

Tuwasaidie kupaza sauti.
 
Hivi vyuo vikuu vinavyoanzishwa kwa mihemuko ya kisiasa ni taabu sana. Hivi kulikuwa na haja ya serikali kupanua elimu ya chuo kikuu wakati hawana uwezo wa kufadhili vijana wote waliodahiliwa. Ilikuwaje wakajichanganya kuanza kutoa ufadhili kwenye vyuo binafsi wakiwa hawana bajeti ya kutosha?
 
Hivi vyuo vikuu vinavyoanzishwa kwa mihemuko ya kisiasa ni taabu sana........hivi kulikuwa na haja ya serikali kupanua elimu ya chuo kikuu wakati hawana uwezo wa kufadhili vijana wote waliodahiliwa. Ilikuwaje wakajichanganya kuanza kutoa ufadhili kwenye vyuo binafsi wakiwa hawana bajeti ya kutosha?
Mkuu UDOM ni hovyo sana, Sasa unaambiwa wanafunzi wanalala 10 kwenye chumba chenye vitanda 4, uwezo wa kumudu wote wanao, shida ni huo ukarabati wanaofanya muda huu baada ya likizo ya miezi 3
 
Wanadhulumu hadi pesa? Basi wafunguliwe mashataka
Mpaka sasa, wahitimu hawajilipwa refunds zao!

Yani hao, finalists mmeshindwa kuwalipa refunds zao na continous mmeshindwa hata kuzigeuza over payments zao kuwa 'direct costs' kweli?

Prof. Kusiluka na Management yako hapo chuoni mjitafakari kabla kauli ya Rais hajafika hapo!
 
Na hapo ndipo Wanafunzi wa kike wengi wanalazimika kulala kwenye mageto ya Wanafunzi wa kiume au Wanaume wa mtaani inaitwa "Sogea Tuishi"

Yaani Mwanafunzi anageuka kuwa Mke kabisa wa Mwanaume ambaye yamkini hakukusudia kuwa nae

Huko ataenda kugongwa sana na kuanza kutumia Vidonge vya kuzuia mimba na hata kutoa mimba

Hebu Uongozi uangalie namna ambavyo wanawaharibu Wanafunzi hasa wa kike

Hatari hii
 
Mpaka sasa, wahitimu hawajilipwa refunds zao!

Yani hao, finalists mmeshindwa kuwalipa refunds zao na continous mmeshindwa hata kuzigeuza over payments zao kuwa 'direct costs' kweli?

Prof. Kusiluka na Management yako hapo chuoni mjitafakari kabla kauli ya Rais hajafika hapo!
Wahitimu wanalipwa refunds za nn? Sijaelewa hapo Mkuu
 
Ukikaa kimya watu wata doubt kama wewe ni mjinga, ukiongea au ukitoa maoni yako watu wana thibitisha kuwa wewe hakika ni mjinga
 
Back
Top Bottom