Kamati ya Uchunguzi ya Kufeli kwa Wanafunzi Law School yasema haijapata Ushahidi wa Kutosha kutoka kwa Wanafunzi kuhusiana na Madai yao

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Aug 2, 2021
1,024
1,611
KAMATI ya tathmini ya mafunzo yanayotolewa na Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST), imesema haijapokea uthibitisho wa kutosha kutoka kwa wanafunzi na walalamikaji wengine kuhusu tatizo la kufeli kwa wingi wanafunzi

Kamati hiyo iliyoongozwa na Mwenyekiti, Waziri mstaafu wa Sheria, Dk. Harrison Mwakyembe, ilipewa mwezi mmoja kukamilisha uchunguzi wake na jana iliwasilisha ripoti hiyo.

“Pamoja na wadau kuwasilisha malalamiko ya rushwa, uonevu au upendeleo katika utungaji au usahihishaji wa mitihani, hakuna ushahidi uliowasilishwa kuthibitisha tuhuma hizo,” alisema.

“Hata hivyo, kwa kuzingatia unyeti wa taasisi na wajibu ilionao ambao unahitaji uadilifu wa hali ya juu wa taasisi ili uweze kufuatilia mienendo yao. Tuhuma zikiendelea, kamati inashauri wakufunzi wanaolalamikiwa wahamishiwe katika idara nyingine za serikali ili kulinda taswira ya taasisi.”

Kamati hiyo ilibaini kasoro kwenye taasisi hiyo ni pamoja na kukosekana na huduma ya chakula katika eneo hilo, hosteli hususani kwa wanafunzi wanaotoka nje ya Dar es Salaam hali inayowafanya waishi maisha magumu.

Pia miundombinu chakavu ambayo haijafanyiwa ukarabati muda mrefu ikiwamo kutofanya kazi kwa kangavuke (generator), uchakavu wa viti vya kukalia, mifumo ya sauti katika kumbi za mihadhara kutokufanya kazi vizuri, kumbi za mikutano kuvuja, mifumo ya Tehama na viyoyozi kutokufanya kazi.

Mengine ni baadhi ya vyumba vya semina kutokuwa na vifaa vya kazi kwa vitendo kama vile vizimba vya kujifunzia vinavyochangia kuathiri mfumo mzima wa uendeshaji wa mafunzo ya uanasheria kwa vitendo.

Kutokuwapo kwa mahakama ya kufundishia kwa vitendo ili kuwezesha wanafunzi kujifunza kwa kushuhudia wenyewe mashauri yanayoendeshwa na mahakama, nyaraka zinazotegemewa na weledi katika kujenga hoja na utetezi.

Kuhusu malalamiko ya wanafunzi kwa Taasisi hiyo ya sheria nchini Dk. Mwakyembe alisema: “Kamati ililalamikiwa na wanafunzi kuwa LST kwa mujibu wa kanuni za rufani inatoa fursa kwa wanafunzi kukata rufani ndani ya siku 14 tangu kutangazwa kwa matokeo endapo hawakubaliani nayo, lakini wanafunzi wanadai kuwa fursa hiyo ni kiini macho kwa sababu mwanafunzi anaruhusiwa kukata rufani bila kuona karatasi yake ya mitihani iliyosahihishwa au bila kuelezwa swali gani alishindwa kujibu vizuri.”

“Pili, mwanafunzi anaruhusiwa kukata rufani akilalamikia ukokotoaji wa alama za ufaulu bila kuona karatasi yake ya mitihani iliyosahihishwa. Wanafunzi walilalamikia utaratibu wa LST kukaa na mitihani iliyokwisha kufanyika kwa zaidi ya miezi saba bila kutoa majibu kwa wanafunzi na kuwafanya wasijue udhaifu na ubora wao na namna ya kujipanga.”

“Walilalamikia mfumo wa utoaji matokeo kielektroniki kuwa unatoa matokeo yenye mkanganyiko, mathalani, kubadilika kwa alama za ufaulu na kusababisha taharuki kwa watahiniwa,”alisema na kuongeza:

“Kamati ilipokea malalamiko kuhusu kuwapo kwa mgongano wa kiutendaji ndani ya bodi ya uendeshaji wa taasisi katika kushughulikia rufani za wanafunzi. Bodi hiyo inathibitisha matokeo ya mitihani na majibu ya rufani kutoka kwenye kamati ya mafunzo na mitihani na wakati huohuo bodi hiyo inafanya kazi kama chombo cha mwisho cha maamuzi ya rufani.”

Mwenyekiti huyo alisema kamati iliona msingi wa hoja hizo za wanafunzi za malalamiko na kushauri ufanyiwe marekebisho.

“Kamati imeuona msingi wa hoja wa malalamiko ya wanafunzi kuhusu mchakato wa rufani dhidi ya matokeo ya mitihani yanayolalamikiwa kwamba haujakaa vizuri kwani haumpi haki mlalamikaji kujua kwa uhakika msingi wa malalamiko yake.

“Vilevile kanuni za rufani tajwa hazilazimu taasisi kushughulikia rufani na kutoa majibu kwa mwanafunzi katika kipindi mahsusi. Kuhusu chombo kimoja ambacho ni bodi ya taasisi kuidhinisha taarifa za rufani na wakati huohuo kuwa chombo cha mwisho cha rufani, kamati nayo inauona mkwamo bayana wa uwajibikaji.

“Hivyo inashauri kanuni ziweke sharti litakalomtaka mwanafunzi wa somo ambalo ameshindwa, kuainisha maswali ambayo alishindwa na alama alizopata. Pili, kanuni ziainishe muda mahsusi wa kushughulikia rufani na kutoa matokeo kwa mlalamikaji na ziweke sharti kuwa matokeo ya mitihani yakitangazwa, michakato yote ikiwa ni pamoja na rufani za mitihani ziwe zimekamilika.”

Kuhusu taasisi hiyo kukaa muda mrefu bila kusahihisha mitihani ya wanafunzi hao, Dk. Mwakyembe alisema: “Kamati haijaridhishwa na sababu za Taasisi na kushauri iondokane na utaratubu huo na imeshauri iimarishe mfumo wa Tehama ili kuondoa malalamiko. Pia ilishauri kutumia vitendo zaidi kuliko nadharia.”

Kamati hiyo ilishauri kwamba umefika wakati kwa serikali kuunda kwa haraka Baraza la Elimu ya Sheria nchini, sekretarieti yake, ofisi zake na kuipa bajeti yake ili kuiwezesha kutekeleza majukumu yake yote yaliyoainishwa kisheri ikiwamo kushirikiana na TCU kupandisha vigezo vya ufaulu wa mitihani ya kidato cha sita na nne kwa watakaotaka kusoma sheria vyuo vikuu nchini.

Kamati hiyo iliundwa Oktoba 13, mwaka huu na Waziri wa Katiba na Sheria kwa ajili ya kufanya tathmini ya mafunzo yanayotolewa kufuatilia malalamiko ya wanafunzi kuwa kuna rushwa mbalimbali ikiwamo ya ngono na kufelisha wanafunzi bila sababu.

Chanzo: Nipashe
 
Advocates wengi hawana uelewa mpana. Yaani wako shallow sana. Ukiwapa thinking na logic kidogo wanafeli vibaya. Nilisema tangu mwanzo hawana akili haoo
 
Hii kamati imefanya kazI kijanja janja tu.

Kwanini inashauri kama malalamiko yakiendelea, walimu wanaolalamikiwa wahamishiwe idara nyingine za serikali, kwani hayo malalamiko yameanza leo?
 
KAMATI ya tathmini ya mafunzo yanayotolewa na Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST), imesema haijapokea uthibitisho wa kutosha kutoka kwa wanafunzi na walalamikaji wengine kuhusu tatizo la kufeli kwa wingi wanafunzi

Kamati hiyo iliyoongozwa na Mwenyekiti, Waziri mstaafu wa Sheria, Dk. Harrison Mwakyembe, ilipewa mwezi mmoja kukamilisha uchunguzi wake na jana iliwasilisha ripoti hiyo.

“Pamoja na wadau kuwasilisha malalamiko ya rushwa, uonevu au upendeleo katika utungaji au usahihishaji wa mitihani, hakuna ushahidi uliowasilishwa kuthibitisha tuhuma hizo,” alisema.

“Hata hivyo, kwa kuzingatia unyeti wa taasisi na wajibu ilionao ambao unahitaji uadilifu wa hali ya juu wa taasisi ili uweze kufuatilia mienendo yao. Tuhuma zikiendelea, kamati inashauri wakufunzi wanaolalamikiwa wahamishiwe katika idara nyingine za serikali ili kulinda taswira ya taasisi.”

Kamati hiyo ilibaini kasoro kwenye taasisi hiyo ni pamoja na kukosekana na huduma ya chakula katika eneo hilo, hosteli hususani kwa wanafunzi wanaotoka nje ya Dar es Salaam hali inayowafanya waishi maisha magumu.

Pia miundombinu chakavu ambayo haijafanyiwa ukarabati muda mrefu ikiwamo kutofanya kazi kwa kangavuke (generator), uchakavu wa viti vya kukalia, mifumo ya sauti katika kumbi za mihadhara kutokufanya kazi vizuri, kumbi za mikutano kuvuja, mifumo ya Tehama na viyoyozi kutokufanya kazi.

Mengine ni baadhi ya vyumba vya semina kutokuwa na vifaa vya kazi kwa vitendo kama vile vizimba vya kujifunzia vinavyochangia kuathiri mfumo mzima wa uendeshaji wa mafunzo ya uanasheria kwa vitendo.

Kutokuwapo kwa mahakama ya kufundishia kwa vitendo ili kuwezesha wanafunzi kujifunza kwa kushuhudia wenyewe mashauri yanayoendeshwa na mahakama, nyaraka zinazotegemewa na weledi katika kujenga hoja na utetezi.

Kuhusu malalamiko ya wanafunzi kwa Taasisi hiyo ya sheria nchini Dk. Mwakyembe alisema: “Kamati ililalamikiwa na wanafunzi kuwa LST kwa mujibu wa kanuni za rufani inatoa fursa kwa wanafunzi kukata rufani ndani ya siku 14 tangu kutangazwa kwa matokeo endapo hawakubaliani nayo, lakini wanafunzi wanadai kuwa fursa hiyo ni kiini macho kwa sababu mwanafunzi anaruhusiwa kukata rufani bila kuona karatasi yake ya mitihani iliyosahihishwa au bila kuelezwa swali gani alishindwa kujibu vizuri.”

“Pili, mwanafunzi anaruhusiwa kukata rufani akilalamikia ukokotoaji wa alama za ufaulu bila kuona karatasi yake ya mitihani iliyosahihishwa. Wanafunzi walilalamikia utaratibu wa LST kukaa na mitihani iliyokwisha kufanyika kwa zaidi ya miezi saba bila kutoa majibu kwa wanafunzi na kuwafanya wasijue udhaifu na ubora wao na namna ya kujipanga.”

“Walilalamikia mfumo wa utoaji matokeo kielektroniki kuwa unatoa matokeo yenye mkanganyiko, mathalani, kubadilika kwa alama za ufaulu na kusababisha taharuki kwa watahiniwa,”alisema na kuongeza:

“Kamati ilipokea malalamiko kuhusu kuwapo kwa mgongano wa kiutendaji ndani ya bodi ya uendeshaji wa taasisi katika kushughulikia rufani za wanafunzi. Bodi hiyo inathibitisha matokeo ya mitihani na majibu ya rufani kutoka kwenye kamati ya mafunzo na mitihani na wakati huohuo bodi hiyo inafanya kazi kama chombo cha mwisho cha maamuzi ya rufani.”

Mwenyekiti huyo alisema kamati iliona msingi wa hoja hizo za wanafunzi za malalamiko na kushauri ufanyiwe marekebisho.

“Kamati imeuona msingi wa hoja wa malalamiko ya wanafunzi kuhusu mchakato wa rufani dhidi ya matokeo ya mitihani yanayolalamikiwa kwamba haujakaa vizuri kwani haumpi haki mlalamikaji kujua kwa uhakika msingi wa malalamiko yake.

“Vilevile kanuni za rufani tajwa hazilazimu taasisi kushughulikia rufani na kutoa majibu kwa mwanafunzi katika kipindi mahsusi. Kuhusu chombo kimoja ambacho ni bodi ya taasisi kuidhinisha taarifa za rufani na wakati huohuo kuwa chombo cha mwisho cha rufani, kamati nayo inauona mkwamo bayana wa uwajibikaji.

“Hivyo inashauri kanuni ziweke sharti litakalomtaka mwanafunzi wa somo ambalo ameshindwa, kuainisha maswali ambayo alishindwa na alama alizopata. Pili, kanuni ziainishe muda mahsusi wa kushughulikia rufani na kutoa matokeo kwa mlalamikaji na ziweke sharti kuwa matokeo ya mitihani yakitangazwa, michakato yote ikiwa ni pamoja na rufani za mitihani ziwe zimekamilika.”

Kuhusu taasisi hiyo kukaa muda mrefu bila kusahihisha mitihani ya wanafunzi hao, Dk. Mwakyembe alisema: “Kamati haijaridhishwa na sababu za Taasisi na kushauri iondokane na utaratubu huo na imeshauri iimarishe mfumo wa Tehama ili kuondoa malalamiko. Pia ilishauri kutumia vitendo zaidi kuliko nadharia.”

Kamati hiyo ilishauri kwamba umefika wakati kwa serikali kuunda kwa haraka Baraza la Elimu ya Sheria nchini, sekretarieti yake, ofisi zake na kuipa bajeti yake ili kuiwezesha kutekeleza majukumu yake yote yaliyoainishwa kisheri ikiwamo kushirikiana na TCU kupandisha vigezo vya ufaulu wa mitihani ya kidato cha sita na nne kwa watakaotaka kusoma sheria vyuo vikuu nchini.

Kamati hiyo iliundwa Oktoba 13, mwaka huu na Waziri wa Katiba na Sheria kwa ajili ya kufanya tathmini ya mafunzo yanayotolewa kufuatilia malalamiko ya wanafunzi kuwa kuna rushwa mbalimbali ikiwamo ya ngono na kufelisha wanafunzi bila sababu.

Chanzo: Nipashe
Aliyeteuliwa kuongoza kamati ndiye aliyeongoza kamati dhidi ya Lowassa na akasema.hadharani kuwa alificha baadhi ya taarifa....

Sijawahi kumuamini tangu siku hiyo ingawa tunatoka njia moja.


Kamati katika hadidu zake ilipaswa kuwaita wahitimu na kuhojiana nao na kama ingeonekana kuna hofu wangechapisha pia fomu mtandaoni ya dodoso kisha wakazifanyiakazi hizo dodoso kubaini ukweli. Kamati ilifeli kwenye kuundwa kwakwe na tusitegemee inhekuja na majibu muafaka.

Kuondoa bias wangemteua hata Kibatala kuongoza jopo
 
Advocates wengi hawana uelewa mpana. Yaani wako shallow sana. Ukiwapa thinking na logic kidogo wanafeli vibaya. Nilisema tangu mwanzo hawana akili haoo
Sio wote ni baadhi tu ambao hawana zaidi ya miaka 5 katika practice.
 
KAMATI ya tathmini ya mafunzo yanayotolewa na Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST), imesema haijapokea uthibitisho wa kutosha kutoka kwa wanafunzi na walalamikaji wengine kuhusu tatizo la kufeli kwa wingi wanafunzi

Kamati hiyo iliyoongozwa na Mwenyekiti, Waziri mstaafu wa Sheria, Dk. Harrison Mwakyembe, ilipewa mwezi mmoja kukamilisha uchunguzi wake na jana iliwasilisha ripoti hiyo.

“Pamoja na wadau kuwasilisha malalamiko ya rushwa, uonevu au upendeleo katika utungaji au usahihishaji wa mitihani, hakuna ushahidi uliowasilishwa kuthibitisha tuhuma hizo,” alisema.

“Hata hivyo, kwa kuzingatia unyeti wa taasisi na wajibu ilionao ambao unahitaji uadilifu wa hali ya juu wa taasisi ili uweze kufuatilia mienendo yao. Tuhuma zikiendelea, kamati inashauri wakufunzi wanaolalamikiwa wahamishiwe katika idara nyingine za serikali ili kulinda taswira ya taasisi.”

Kamati hiyo ilibaini kasoro kwenye taasisi hiyo ni pamoja na kukosekana na huduma ya chakula katika eneo hilo, hosteli hususani kwa wanafunzi wanaotoka nje ya Dar es Salaam hali inayowafanya waishi maisha magumu.

Pia miundombinu chakavu ambayo haijafanyiwa ukarabati muda mrefu ikiwamo kutofanya kazi kwa kangavuke (generator), uchakavu wa viti vya kukalia, mifumo ya sauti katika kumbi za mihadhara kutokufanya kazi vizuri, kumbi za mikutano kuvuja, mifumo ya Tehama na viyoyozi kutokufanya kazi.

Mengine ni baadhi ya vyumba vya semina kutokuwa na vifaa vya kazi kwa vitendo kama vile vizimba vya kujifunzia vinavyochangia kuathiri mfumo mzima wa uendeshaji wa mafunzo ya uanasheria kwa vitendo.

Kutokuwapo kwa mahakama ya kufundishia kwa vitendo ili kuwezesha wanafunzi kujifunza kwa kushuhudia wenyewe mashauri yanayoendeshwa na mahakama, nyaraka zinazotegemewa na weledi katika kujenga hoja na utetezi.

Kuhusu malalamiko ya wanafunzi kwa Taasisi hiyo ya sheria nchini Dk. Mwakyembe alisema: “Kamati ililalamikiwa na wanafunzi kuwa LST kwa mujibu wa kanuni za rufani inatoa fursa kwa wanafunzi kukata rufani ndani ya siku 14 tangu kutangazwa kwa matokeo endapo hawakubaliani nayo, lakini wanafunzi wanadai kuwa fursa hiyo ni kiini macho kwa sababu mwanafunzi anaruhusiwa kukata rufani bila kuona karatasi yake ya mitihani iliyosahihishwa au bila kuelezwa swali gani alishindwa kujibu vizuri.”

“Pili, mwanafunzi anaruhusiwa kukata rufani akilalamikia ukokotoaji wa alama za ufaulu bila kuona karatasi yake ya mitihani iliyosahihishwa. Wanafunzi walilalamikia utaratibu wa LST kukaa na mitihani iliyokwisha kufanyika kwa zaidi ya miezi saba bila kutoa majibu kwa wanafunzi na kuwafanya wasijue udhaifu na ubora wao na namna ya kujipanga.”

“Walilalamikia mfumo wa utoaji matokeo kielektroniki kuwa unatoa matokeo yenye mkanganyiko, mathalani, kubadilika kwa alama za ufaulu na kusababisha taharuki kwa watahiniwa,”alisema na kuongeza:

“Kamati ilipokea malalamiko kuhusu kuwapo kwa mgongano wa kiutendaji ndani ya bodi ya uendeshaji wa taasisi katika kushughulikia rufani za wanafunzi. Bodi hiyo inathibitisha matokeo ya mitihani na majibu ya rufani kutoka kwenye kamati ya mafunzo na mitihani na wakati huohuo bodi hiyo inafanya kazi kama chombo cha mwisho cha maamuzi ya rufani.”

Mwenyekiti huyo alisema kamati iliona msingi wa hoja hizo za wanafunzi za malalamiko na kushauri ufanyiwe marekebisho.

“Kamati imeuona msingi wa hoja wa malalamiko ya wanafunzi kuhusu mchakato wa rufani dhidi ya matokeo ya mitihani yanayolalamikiwa kwamba haujakaa vizuri kwani haumpi haki mlalamikaji kujua kwa uhakika msingi wa malalamiko yake.

“Vilevile kanuni za rufani tajwa hazilazimu taasisi kushughulikia rufani na kutoa majibu kwa mwanafunzi katika kipindi mahsusi. Kuhusu chombo kimoja ambacho ni bodi ya taasisi kuidhinisha taarifa za rufani na wakati huohuo kuwa chombo cha mwisho cha rufani, kamati nayo inauona mkwamo bayana wa uwajibikaji.

“Hivyo inashauri kanuni ziweke sharti litakalomtaka mwanafunzi wa somo ambalo ameshindwa, kuainisha maswali ambayo alishindwa na alama alizopata. Pili, kanuni ziainishe muda mahsusi wa kushughulikia rufani na kutoa matokeo kwa mlalamikaji na ziweke sharti kuwa matokeo ya mitihani yakitangazwa, michakato yote ikiwa ni pamoja na rufani za mitihani ziwe zimekamilika.”

Kuhusu taasisi hiyo kukaa muda mrefu bila kusahihisha mitihani ya wanafunzi hao, Dk. Mwakyembe alisema: “Kamati haijaridhishwa na sababu za Taasisi na kushauri iondokane na utaratubu huo na imeshauri iimarishe mfumo wa Tehama ili kuondoa malalamiko. Pia ilishauri kutumia vitendo zaidi kuliko nadharia.”

Kamati hiyo ilishauri kwamba umefika wakati kwa serikali kuunda kwa haraka Baraza la Elimu ya Sheria nchini, sekretarieti yake, ofisi zake na kuipa bajeti yake ili kuiwezesha kutekeleza majukumu yake yote yaliyoainishwa kisheri ikiwamo kushirikiana na TCU kupandisha vigezo vya ufaulu wa mitihani ya kidato cha sita na nne kwa watakaotaka kusoma sheria vyuo vikuu nchini.

Kamati hiyo iliundwa Oktoba 13, mwaka huu na Waziri wa Katiba na Sheria kwa ajili ya kufanya tathmini ya mafunzo yanayotolewa kufuatilia malalamiko ya wanafunzi kuwa kuna rushwa mbalimbali ikiwamo ya ngono na kufelisha wanafunzi bila sababu.

Chanzo: Nipashe

Taarifa hii ni bora zaidi kuliko Ile ya kishabiki tokea mwananchi:

Dk Mwakyembe akabidhi ripoti uchunguzi kufeli mawakili

Kwamba walalamikiwa waondolewe chuoni hapo, hiyo ni hatua njema.

Kwamba utaratibu wa rufani haufai ubadilishwe, hilo ni jema.

Kwamba yapo mengi yaliyo fyongo kwa miungu watu wale waliowaaminisha wengine wao ndiyo wapakwa mafuta, hilo ni hatua njema.

Muhimu ni ripoti hiyo kuwekwa hadharani Ili kuyaona yote yaliyozingatiwa na pia kupuuzwa na kamati hii.

"Hata hivyo nani alitegemea zile sera zetu za kulindana na kufunika makombe wana haramu wapite kutokuwemo tokea kwa Mwakyembe?'

Shime wahanga wa jamii hizi za kidhwalimu ambako haki ni kwa "the rule of the jungle."

Wanafunzi Law School kulikoni kushindwa kujisimamia

"Aluta Continua."
 
Niliwaambia watu hapa siku hizi wanafunzi wetu wengi ni "vilaza" nikashambuliwa sana hapa JF.
Wakili anashindwa kuandaa hati ya mashtaka mnataka afaulu.

Kwani ndivyo ripoti ilivyosema mkuu? Haina lolote kuwahusu walalamikiwa?

Ulichoandika ni kuakisi zile roho za watanzania wale maskini kabisa.
 
Wanaharibu kiswahili. Wanaanzisha lugha mpya ndani ya kiswahili. Walikishindwa nini kutohoa na kuliita JENERETA. Mbina maneno mengi tumeyachukua kama yalivyo.
Hili nalo BAKITA wakaliangalie,ni usumbufu usio wa lazima
 
Kwani ndivyo ripoti ilivyosema mkuu? Haina lolote kuwahusu walalamikiwa?

Ulichoandika ni kuakisi zile roho za watanzania wale maskini kabisa.

Kwamba kusema wanafunzi wana uwezo mdogo "vilaza" kwamba nimejitungia?
Si ndio tume imetafiti na imekuja na ripoti au una nongwa na mimi?
Umasikini unao wewe.
 

Attachments

  • IMG-20221121-WA0001.jpg
    IMG-20221121-WA0001.jpg
    64.8 KB · Views: 8
Kwamba kusema wanafunzi wana uwezo mdogo "vilaza" kwamba nimejitungia?
Si ndio tume imetafiti na imekuja na ripoti au una nongwa na mimi?
Umasikini unao wewe.

Kuna tofauti ya umaskini na roho za kimaskini. Zingatia Hilo mkuu.

Jingine la kuzingatia ni "nongwa". Mtu anakuwaje na nongwa na mtu asiyejulikana?

Ni hayo tu ndugu mjumbe.
 
Back
Top Bottom