Wana MMU tushirikiane kuboresha Jukwaa letu

Wana MMU tushirikiane kuboresha Jukwaa letu

Status
Not open for further replies.

Mr Rocky

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2007
Posts
15,178
Reaction score
14,383
Wana MMU,

Wengi wetu hasa wale ambao tumejiunga kitambo tumekuwa tukilalamika mara kwa mara juu ya Jukwaa hili letu Pendwa la MMU Kuzorota kila siku zinapoenda. Members mbali mbali wamerusha threads za kulalamika na wengine kushauri juu ya tatizo lililopo kwenye Jukwaa hili.

Cha kusikitisha siku zinavyozidi kwenda hali inazidi kuwa mbaya zaidi na zaidi. Jukwaa la MMU ilikuwa ni Jukwaa ambalo ukiingia hukosi kitu kipya na cha kukujenga katika Mahusiano, Mapenzi na Urafiki. Members walikuwa wakichangia wanachangia kwa hoja, na hata utani ukiwepo ulikuwepo ndani ya mada na si kwa kuvuruga mada. Ilikuwa ukikuta thread ina posts nyingi, unakuwa na moyo wa kusoma post zote sababu post zote zilikuwa ni kuhusiana na mada hivyo za kujifunza pia.

Kumekuwa na wimbi za mada za Kushushiana hadhi, za kitoto, zile zinazoelemea ngono tu, zile zinazolenga kujadili utumiaji wa Tigo, na mbaya zaidi zile zilizolenga kubomoa taasisi ambayo ni nyeti katika jamii yetu ambayo ni "Ndoa". Tukiendelea hivi hivi MMU itakuwa ni moja ya Lubricator wa kubomoa maadili katika Jamii. Haipendezi.

Kama mnakumbuka thread ya kwanza kabisa kugusia mada zisizofaa hapa MMU ni ile ya Mod INNOVATOR aliyorusha hapa October, 2011. So far inaonekana kuwa nguvu kazi ya kuondoa mada hizo imeelemea kwa Mods tu na hivyo wao pia huzidiwa. Mkuu Invisible amekubali kutupa ushirikiano na kaahidi sasa hivi atatupa Mod aliye dedicated kwenye Jukwaa huku pia akitafuta suluhisho la kudumu.

Kilicho baki kwetu ni jitihada zetu kushirikiana kuweza kuboresha Jukwaa kwa njia hizi;


1. Kila tunapo ona Bandiko halifai tutumie Button ya Report Abuse kutoa taarifa mara moja ili itolewe.
2. Tujitahidi kurusha mada za kujenga na sio kubomoa au kumkomoa fulani au kuonyesha madhaifu fulani ya jamii yetu kwa kila atakae weza.
3. Tujitahidi kujadili kwa hoja na kupunguza mizaha na kejeli kwa warusha mada. Kama mada haifai ni kheri kufanya namba moja hapo juu badala ya kuchangia.
4. Kuondoa dharau kwa Mwanamke na Mwanaume pia. Mada za kusanifu Mwanaume ama Mwanamke hazijengi, zinabomoa tu.
5. Tujitahidi kuangalia pande zote za mijadala, isiwe vitu negative tu. Mfano sasa hivi kila inapokuja mada inayohusiana na ndoa huwa ni ya kukatisha tu tamaa, hata wale ambao hawapo kwenye taasisi hiyo hukatishwa tamaa kwa kukuza negatives tu na hali kuna positives pia kwa upande wa ndoa na sio kila ndoa ni majangaa au ina matatizo wapo wenye raha na furaha kwa ndoa zao
6. Masuala ya Ngono, Maumbile ni kheri yakajadiliwe Jukwaa la Wakubwa ambapo kule mjadala utakuwa wa wazi na utapata majibu yote unayoyataka na utajibiwa kwa uwazi bila kificho.


Wapendwa wana MMU, Tukiangalia baadhi ya mambo niliyo ainisha tutatambua kuwa ni vitu ambavyo vipo ndani ya uwezo wetu kurekebisha. Take note haya si mawazo yangu tu, ni mawazo ya members mbali mbali tokana na michango yao kwenye threads za malalamiko na mijadala ya hapa na pale. Hivyo pia mnaweza ongeza maarifa mengine pia.

Naomba Ushirikiano wenu wa dhati tuweze kurudisha hadhi ya Jukwaa letu pendwa la MMU Lilivyokuwa awali.

Ingependeza ujumbe huu uwafikie wadau wote wa MMU. Nimejitahidi kadri ya uwezo wangu ku mention members wengi, ila bado sijaweza kukumbuka wote, hivyo kila ambae ataona kuna mdau kasahaulika tafadhali naomba tushirikiane katika hili pia.



CC: AshaDii, BAK, EMT, The Finest, The Boss, Dark City, Bishanga, Asprin, snowhite, SnowBall, HorsePower, Lizzy, Erickb52, King'asti, Blaki Womani, Husninyo, Heaven on earth, Lady doctor, amu, mimisa, Chocs, Mtambuzi, Mrembo by Nature, charminglady, Dena Amsi, Nicas Mtei, Smile, mwaJ, Judgment, watu8, Baba V, Kongosho, sweetlady, Mamndenyi, Marejesho, ladyfurahia, KOKUTONA, Roulette, Kaizer, KakaKiiza, The secretary, Mwali, Katavi, Fixed Point, Paloma, Passion Lady, cacico, kiwatengu, mimisa, sosoliso, Dark City, Kimey, Teamo, MwanajamiiOne, Preta, Arabela, Nivea, Avemaria, KOKUTONA, Bujibuji, Eiyer, Ruttashobolwa, Rutashubanyuma, Fidel80, Mzee wa Rula pakajimmy, Vin Diesel, WiseLady, Maeskron, Mentor, Mwita Maranya, Mungi, Arushaone, Tuko, Speaker, Fang, Moderator, Invisible, INNOVATOR, Pruner grafani11, Blaine
 
Nakubaliana na wewe Mr Rocky ni vyema kuweka na kujadili mada ambazo kwa namna moja au nyingine zinaweza kusaidia kuwajenga watu badala ya kuwavunja moyo na kuwakatisha tamaa. Sijui ni kwanini, baadhi ya wadau huwa hawapendi kuchangia kwenye mada za namna hii, na badala yake hupenda mada zinazolenga stori zaidi na kuchat badala ya kujenga na kuelimisha jamii.
 
Asante Binamu Mr Rocky, kusema ukweli jukwaa siku hzi limedoda.
Mtu anakuja eti anauliza "natafuta demu mkali" jamani, ina mana mtaani au kazini kwenu hakuna?
Kma kweli mnakera sana.

Sana sana hili la kujadili maumbile au madhahifu ya jinsia fulani ndo yamezidi humu.
Mr Rocky...bora umewapa ukweli.
.....Nitarudi.
 
Last edited by a moderator:
Nakubaliana na wewe Mr Rocky ni vyema kuweka na kujadili mada ambazo kwa namna moja au nyingine zinaweza kusaidia kuwajenga watu badala ya kuwavunja moyo na kuwakatisha tamaa. Sijui ni kwanini, baadhi ya wadau huwa hawapendi kuchangia kwenye mada za namna hii, na badala yake hupenda mada zinazolenga stori zaidi na kuchat badala ya kujenga na kuelimisha jamii.
HorsePower tatizo lilililopo ni kuwa watu wana majibu mepesi kwa maswali mazito na watu hawapendi mada za kuchangamsha vichwa ila zile nyepesi za kuchat na kujibu kifupi na ukileta mada ndefu tena wanalalamika ni ndefu mno hata kusoma na inachosha so hawawezi kuchangia
 
Last edited by a moderator:
Naunga mkono hoja. Na threads zinazolenga kushambulia makabila hasa wachagga zilegezwe makalio yake.

Mijitu kila kukicha ni wachaga tu. Shenzy taipu zao na nusu.

Mi nakasirikaga chapchap sana.

Wanafunzi warudi madarasani, siku hizi wamepewa BRN.
 
Rocky mie nashukuru kwa jitihada zako, na nakubaliana na hoja uliyotoa na zilizotolewa na wengi hapo nyuma.

Kuna tatizo kubwa pia ambalo mie nime observe, naona kama vile tatizo lingine kubwa ni unafiki pia. Kuwa sababu nimezoeana na Rocky (bila kujalisha ni jamvini ama nje ya jamvi) basi siwezi kumkosoa hata kama nimeona kakosea. Hilo kwa kweli nalo ni tatizo…

Kuna wadau wengine hata si waku post sana ila ni wasomaji, na katika usomaji wao hujenga trust katika michango ya baadhi ya members. Hivyo anapo ona huyo mtu ambaye yeye kajenga trust kwake anaunga mkono kitu ambacho kinachukuliwa nje ya maadili basi hata yeye follower inakuwa rahisi kwake kuamini ama kufanya hicho kitu.

Majukwaa ya MMU/CC ndio majukwaa hapa Jf yanayo ongoza kwa members kupendana na kushikamana, inaweza kuwa si wote ila ndio hivyo ikifuatiwa na Jukwaa la Tech and Gadgets and Education. Kupendana kwetu na urafiki wetu usitufanye kufumbia macho ama kuchekea kitu ambavyo kimsingi hata wewe unae unga mkono unaona si sawa, ama waona basi ni kheri usichangie kabisa kuliko kuenda tofauti. Hilo suala halijengi.

Tatizo lingine ambalo nalo halijengi ni tabia ya wadau baadhi ambao wapo karibu (bila kujalisha ni jamvini or not) kuleta habari zao private (Za PM na maisha ya nje ya mtandao) hapa kwa malengo ya kulipuana. Hilo ni suala baya… Ni wengi ambao inaweza tokea kukwazana wa wetu wa karibu but ni kheri mkaongea pembeni na mkamaliza tofauti kuliko kwa njia ya kuanikana. Si nzuri kabisa maana inatokoa tu faida kwa wengine wengi na pia kukusesha raha baadhi kuendelea kushiriki hapa Jamvini na kuwafanya wengine hata kubadili ID. Ubaya wa hili inaongeza hata makundi katika majukwaa... Unakuta huyu is for this member, yule for that member... Na kuweka mazingira hata kama member anakosea sababu tu you consider yupo upande wako basi unashindwa kumkosoa.

Naamini kabisa kama members... Hizo suggestions ulizotoa tukizizingatia na wote tukacheza nafasi zetu Jukwaa litakuwa bora na kuwa vile tutakavyo. Na wengi tutajifunza na kuelimishana pia.

Naona watu wengi wa kuwa CC Umejitahidi kukumbuka. Naomba niongeze hawa ;

BelindaJacob, Zion Daughter, Azimio Jipya, gfsonwin Elia, figganigga, Gaga, Globu, Matola, jouneGwalu, kinyoba, Keren_Happuch, klorokwini, ndyoko, kivuma, lara 1 , Madabwada, MadameX, MAMMAMIA, Mamzalendo, Manyanza, Mbu, Manumbu, Speaker, PetCash, queenkami, Ndahani,
 
Asante Binamu Mr Rocky, kusema ukweli jukwaa siku hzi limedoda.
Mtu anakuja eti anauliza "natafuta demu mkali" jamani, ina mana mtaani au kazini kwenu hakuna?
Kma kweli mnakera sana.

Sana sana hili la kujadili maumbile au madhahifu ya jinsia fulani ndo yamezidi humu.
Mr Rocky...bora umewapa ukweli.
.....Nitarudi.

Binamu Madame B na urudi kweli
Kama wanahitaji kutaja maumbile kwa uwazi wakawatafute akina Kimbweka na mwenzake funzadume watawatajia bila wasi wasi ila humu tujadili mada za kuchangamsha na kujifunza na humu tupo kwa kuwa tunahitaji kujifunza
cc AshaDii
 
Last edited by a moderator:
AshaDii asante sana kwa mchango wako sikutaka kuucopy wote maana nitakuwa nawatesa watumiaji wengine wa simu #
Mchango wetu wa kila mmoja ni mzuri sana katika kufikia lengo na kufikia pale tunapotaka
Lengo la MMU libakie lile lile ambalo limebebwa na maana nzima ya MMU na si zaidi
Lisiwe chanzo cha magomvi au kufarakana au kuwa chanzo cha ugomvi ila liwe chachu ya malezi na mafunzo
 
Last edited by a moderator:
i miss u Mr Rocky how are u then ni kweli nina muda sasa MMU nachungulia tu nakukimbia hadhi imeshuka sana.


I miss u too dear Nivea naomba sasa usikimbie ila uwe chanzo cha kubadilisha mambo humu ndani turudi kwenye uhalisia na mchango wako ni muhimu sana humu ndani Dark City dah acha tuu imekuwa fashion kujadili wachagga humu ndani as if ni wao tuu wenye kasoro au ni wao tuu hawajui baadhi ya mambo au hawajui kabisa dhana ya mapenzi
 
Last edited by a moderator:
Na hii biashara ya kamjamaa kamoja kanaanzisha threads mia nne kwa siku! Yani zote ni viumbea tuuu.

Mi nakasirikaga mpaka naenda kuzimia kule jukwaa la wakubwa.

Mkuu Asprin katika watu waliopotea ni wewe mkuu
Dah karibu sana mkuu bora turudishe MMU yetu bana enzi AshaDii na Lizzy wanatoa topic unajiuliza nijibu au nichangie nini au uanjikuta umebaki msomaji tuu maana mada ni moto
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom