Wakati Mzee wetu Reginald Abraham Mengi anajaribu kupambana na Mafisadi Papa, ndani ya nyumba yake si shwari hususan katika Kampuni ya The Guardian Ltd.
Wafanyakazi wanapiga miayo bila mishahara, huku wanene wakipigana vita ya kupata utukufu wa Bwana Mengi.
Ndugu yetu Kiondo Mshana, Mkurugenzi Mtendaji wa IPP MEDIA, amefaulu kumuondoa sakina kwa mbinu mbili--Ushirikina na fitina kali ambayo kwa karibu alisaidiwa na bibie Joyce Kisaka au Wakuvunga ukitaka.
Joyce kamaliza swahiba wake Sakina kwa kumchunguza nyendo zake na kisha kuripoti kwa wanene. Mshana kaendelea kuingia viwanja kutafuta uchawi ili kuhakikisha anabakia kuwa top. Sakina kaangukia pua sasa ameamua kujiuzulu.
Msaki aliponusa vita ijayo, akaamua kuchomoka na kurudi Mwananchi. Eti kila alipokuwa akiingia ofisini mara kichwa, mara macho hayaoni, akiwa nje mzima kama bikira wa Kiarabu!
Sasa mkakati unaendelea na kuna wahariri wawili ambao wanalengwa kwa udi na uvumba lazima wang'oke ili Mshana apata kupumua. Katika Mkakati huo, ataendelea kumtumia bibie Kisaka---Mrembo anayewaliza hata wanene pale Ikulu.
Joyce kabebwa na Sakina kwa miaka kadhaa na inasemekana walikuwa mashoga wakubwa, wanaosafiri pamoja na kutembea pamoja lakini cha ajabu, Sakina hajui nyumbani kwa Joyce na wala hata kama ni mke wa mtu.
Wahariri hao wawili ambao inasemekana wana msimamo thabiti dhidi ya uongozi dhaifu wa Mshana, ni lazima waondoke kwa gharama ya yoyote ile ikibidi hata kuuaawa. Nimefanikiwa kupenyeza kinasa sauti ndani ya Kikao cha siri kati ya Mshana na Kisaka punde tu aliporudi toka Uingereza anakodai alikwenda kuhudhuria semina.
Lakini ukweli alitumwa kwenda kupiga fitina na mnene mmoja ndani ya Ikulu ikiwa ni pamoja na kuiba nyaraka za Serious Fraud Office Zinazowahusu wakubwa hapa Bongo, baada ya kudai anaweza kuleta faili lote.
Lakini kaambulia patupu na mmoja wa wanene wanaotuhumiwa kwenye kesi ya SFO sasa anadai arudishiwe ngawira zake, na Mama katishia kulipua bomu. Mshana anaujua Mpango huu ambao bosi wake hana taarifa nao.
Ndani ya miezi mitatu ijayo mtayasikia haya na mtanikumbuka.