Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,262
- 9,714
Ndugu zangu Wana CCM lazima Tufahamu kuwa Nguvu ya CCM na Wanaccm imekuwa Ni katika umoja wetu, Ushirikiano Wetu,mshikamano wetu ,upendo miongoni mwetu, UZALENDO wetu kwa chama na serikali yetu, misimamo yetu, kutanguliza mbele maslahi ya chama na serikali yetu, Sera na ajenda zetu pamoja na kuwa na Dira na muelekeo unaoeleweka na kuwa vutia watanzania katika kutuunga mkono na kutuchagua kila ufikapo uchaguzi wa aina yoyote Ile unapoitishwa na kufanyika
Nguzo hizi hatupaswi kuziacha, Wala kuzisahau,Wala kuzitupa,Wala kuhisi zimepitwa na wakati, Ni nguzo zilizotufikisha hapa Tulipo, Ni nguzo zilizokishikiria chama chetu, Ni nguzo zilizotufanya kuaminika kwa watanzania, kupigiwa kura kila uchaguzi, kupigania chama katika uchaguzi na kukilinda chama chetu kwa Hali na Mali, Ni nguzo zilizofanya maadui wa ndani na nje ya chama kukosa upenyo wa kukivuruga na kukisambalatisha chama chetu, Ni nguzo Zinazofanya chama hiki kionekane bado ni kijana kila siku, Ni nguzo zinazoongeza wanachama wapya kila siku,
Ni nguzo Zinazofanya kadi za CCM zitafutwe Kama Dhahabu katika ofisi zake na Ni nguzo ambazo zimekifanya CCM kuwa Tumaini la watanzania wa matabaka na Rika zote hapa nchini na zaidi Ni kuwa Ni nguzo Zinazofanya mwanachama akihama Leo CCM lazima kesho Arudi ndani ya CCM na kujutia uamuzi wake wa kukihama chama, mwisho ni kuwa hizi Ni nguzo Zinazofanya chama hiki kuwa kikubwa kuliko mtu binafsi na maslahi yake, Hakuna mkubwa ndani ya CCM, Kama huamini Hama leo CCM uone Kama kitayumba au kuyumbishwa
Hivyo lazima Tuendelee kuwa wamoja na kushikamana, Tusichonganishwe na mtu wa aina yoyote yule kwa misingi ya udini, ukabila, ukanda,jinsia Wala Hadhi, Tuseme na Tufahamu kuwa wote Ni sawa na tuna haki sawa ndani ya CCM, wote Tukipiganie na Tukilinde chama chetu kwa nguvu zetu zote, Hakuna mpinzani atakaye tulindia chama chetu Wala kutujengea chama chetu, Hakuna mpinzani anayependa kuona tukiwa wamoja, wapinzani wanatamani tusambalatike hata leo tu, Tusiwape upenyo huo
Tusiwape Siri zetu, Tusiwape mipango Wala mikakati yetu, Tusiwaonyeshe njia zetu.
Tumpe ushirikiano wakutosha Mwenyekiti wetu Mama Samia, Tumtetee kwa nguvu zetu zote popote tulipo, Tuwajibu wapinzani wetu kwa hoja nzito nzito, Tumbebe Samia wetu katika mikono yetu, na migongo yetu, Tusikubali ashambuliwe na wapinzani wetu,
Tufahamu akishambuliwa yeye Ni sawa na kwamba tumevamiwa sote, siasa Ni hoja na Ni sayansi, lazima Tuwe watu wa hoja muda wote zidi ya wapinzani wetu,CCM Ni moja, Wana CCM Ni wamoja na chama ni kimoja Tu CHAMA CHA MAPINDUZI, Tusiumizane, tusipaniane.
Tusiwekeane mitego wenyewe kwa wenyewe Wala Tusichukiane wenyewe kwa wenyewe, Wala Tusiangushane wenyewe kwa wenyewe kwa kumnufaisha mpinzani wetu
Kazi iendeleee Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge
LUCAS Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu
Nguzo hizi hatupaswi kuziacha, Wala kuzisahau,Wala kuzitupa,Wala kuhisi zimepitwa na wakati, Ni nguzo zilizotufikisha hapa Tulipo, Ni nguzo zilizokishikiria chama chetu, Ni nguzo zilizotufanya kuaminika kwa watanzania, kupigiwa kura kila uchaguzi, kupigania chama katika uchaguzi na kukilinda chama chetu kwa Hali na Mali, Ni nguzo zilizofanya maadui wa ndani na nje ya chama kukosa upenyo wa kukivuruga na kukisambalatisha chama chetu, Ni nguzo Zinazofanya chama hiki kionekane bado ni kijana kila siku, Ni nguzo zinazoongeza wanachama wapya kila siku,
Ni nguzo Zinazofanya kadi za CCM zitafutwe Kama Dhahabu katika ofisi zake na Ni nguzo ambazo zimekifanya CCM kuwa Tumaini la watanzania wa matabaka na Rika zote hapa nchini na zaidi Ni kuwa Ni nguzo Zinazofanya mwanachama akihama Leo CCM lazima kesho Arudi ndani ya CCM na kujutia uamuzi wake wa kukihama chama, mwisho ni kuwa hizi Ni nguzo Zinazofanya chama hiki kuwa kikubwa kuliko mtu binafsi na maslahi yake, Hakuna mkubwa ndani ya CCM, Kama huamini Hama leo CCM uone Kama kitayumba au kuyumbishwa
Hivyo lazima Tuendelee kuwa wamoja na kushikamana, Tusichonganishwe na mtu wa aina yoyote yule kwa misingi ya udini, ukabila, ukanda,jinsia Wala Hadhi, Tuseme na Tufahamu kuwa wote Ni sawa na tuna haki sawa ndani ya CCM, wote Tukipiganie na Tukilinde chama chetu kwa nguvu zetu zote, Hakuna mpinzani atakaye tulindia chama chetu Wala kutujengea chama chetu, Hakuna mpinzani anayependa kuona tukiwa wamoja, wapinzani wanatamani tusambalatike hata leo tu, Tusiwape upenyo huo
Tusiwape Siri zetu, Tusiwape mipango Wala mikakati yetu, Tusiwaonyeshe njia zetu.
Tumpe ushirikiano wakutosha Mwenyekiti wetu Mama Samia, Tumtetee kwa nguvu zetu zote popote tulipo, Tuwajibu wapinzani wetu kwa hoja nzito nzito, Tumbebe Samia wetu katika mikono yetu, na migongo yetu, Tusikubali ashambuliwe na wapinzani wetu,
Tufahamu akishambuliwa yeye Ni sawa na kwamba tumevamiwa sote, siasa Ni hoja na Ni sayansi, lazima Tuwe watu wa hoja muda wote zidi ya wapinzani wetu,CCM Ni moja, Wana CCM Ni wamoja na chama ni kimoja Tu CHAMA CHA MAPINDUZI, Tusiumizane, tusipaniane.
Tusiwekeane mitego wenyewe kwa wenyewe Wala Tusichukiane wenyewe kwa wenyewe, Wala Tusiangushane wenyewe kwa wenyewe kwa kumnufaisha mpinzani wetu
Kazi iendeleee Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge
LUCAS Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu