Wamemtia hasara kubwa sana Lowassa

Wamemtia hasara kubwa sana Lowassa

Jembemtaji

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2014
Posts
1,192
Reaction score
928
Kati ya watia nia ya urais Lowassa ndie aliongoza kwa uekezaji kwenye dhamira yake kuliko wote 42.

1. Kuanzia mda aliotumia kusaka urais alianza mapema kuliko wote na alifanikiwa kujenga mazingira mazuri.

2. Misaada aliyotoa kwenye nyumba za ibada kama misikitini na makanisani.

3. Kwenye harambee mbalimbali

4. Mikutano ya bodaboda.

5. Gharama za mikutano ya kutangaza nia ni babkubwa kuliko wote.

Apa CCM wangeangalia na kumpa ata miaka 5 tukaona angewafanyia
nini watanzania.

Siamini kabisa kama atakubali kua ndio basi Iwe amekosa lazima kuna maamuzi magumu atayafanya.
 
Kosa lake kubwa ni kupambana na Jk otherwise angepata anachotaka, kila aliekuwa na bifu na Rais au Ridhwan alikuwa Team Lowassa, alisahau kuwa Sumaye, Mbowe na Slaa wote wanatoka eneo moja walijaribu kumkabili huyu Mkwere wakashindwa nae anatokea kulekule akatumia njia zile zile.
 
The biggest Loser in the history of this country . He won the Battle BUT lost the War. Kaanza kuomba kura kwa wananchi wakati muda bado. Ni sawa na mtu anotaka kuagiza gari ya gharama Japan halafu akaanza kulipa ushuru Tra wakati gari yenyewe ata hajanunua.
 
Kosa lake kubwa ni kupambana na Jk otherwise angepata anachotaka, kila aliekuwa na bifu na Rais au Ridhwan alikuwa Team Lowassa, alisahau kuwa Sumaye, Mbowe na Slaa wote wanatoka eneo moja walijaribu kumkabili huyu Mkwere wakashindwa nae anatokea kulekule akatumia njia zile zile.

Wale ni marafiki wakubwa na wote waliwai kukiri kua marafiki,bifu lilitoka wapi tena?
 
Alichokua anajaribu kufanya EL ni uwekezaji ktk siasa.sasa limebuma.mitaji aliyokopa kushnei. Nadhan asubiri kufa ili aje awekewe maua ya dhahabu
 
Siasa ni mchezo mchafu sana lakini ni mzuri sana kwa wanaojua kuucheza,wapambe wake waliamua wampige chini Membe na kura zote zikaelekea kwa Magufuli,atakuwa kama familia ya Oginga tangia baba sasa mtoto wote wanaukosakosa "ukubwa"
 
Wale ni marafiki wakubwa na wote waliwai kukiri kua marafiki,bifu lilitoka wapi tena?

Bifu lilianza kwenye Kikao cha Halmashauri kuu pale Lowassa alipojipanga kujibu madai ya Richmond kwa kumhusisha Rais kuwa alikuwa anajua kila kitu, kipindi hicho anamkabili Rais wajumbe wenzie wa NEC walikuwa wameacha On simu zao ili waandishi wasikie kila kitu kesho yake wakairipoti, jk nae akalipa kwa kuja na Kuvuana magamba. 2011 iyo ndo vita ikapamba moto
 
The biggest Loser in the history of this country . He won the Battle BUT lost the War. Kaanza kuomba kura kwa wananchi wakati muda bado. Ni sawa na mtu anotaka kuagiza gari ya gharama Japan halafu akaanza kulipa ushuru Tra wakati gari yenyewe ata hajanunua.

Lakin alifanya hayo kwa faida ya chama pia mkuu
 
Siasa ni mchezo mchafu sana lakini ni mzuri sana kwa wanaojua kuucheza,wapambe wake waliamua wampige chini Membe na kura zote zikaelekea kwa Magufuli,atakuwa kama familia ya Oginga tangia baba sasa mtoto wote wanaukosakosa "ukubwa"

Hahahahaaa umemaliza!
 
Bifu lilianza kwenye Kikao cha Halmashauri kuu pale Lowassa alipojipanga kujibu madai ya Richmond kwa kumhusisha Rais kuwa alikuwa anajua kila kitu, kipindi hicho anamkabili Rais wajumbe wenzie wa NEC walikuwa wameacha On simu zao ili waandishi wasikie kila kitu kesho yake wakairipoti, jk nae akalipa kwa kuja na Kuvuana magamba. 2011 iyo ndo vita ikapamba moto

Nimekuelewa mkuu sasa napata picha.
 
kama vipi watu wawe waungwana wamrudishie hela zake huyu mzee zimuuguze uguze kidogo maana hali yake kiafya sio nzuri
 
Back
Top Bottom