Wamasai tunadharaulika pasipo sababu

Wamasai tunadharaulika pasipo sababu

Muhudumu wa Bar: Karibu
Masai: Asante
Muhudumu: Nikuhudumie nini.
Masai: Nataka bia ya baridi..
Muhudumu: Bia gani?
Masai: Ile yenye chui
Muhudumu: Hii hapa nifungue?
Masai: Fungua
Muhudumu: Haya nimefungua karibu.
Masai: Kwenye hii glass pima ya bia 200 na inayobaki uzia rafiki ingine..
 
Pamoja na kuiingizia nchi matrilioni kupitia utalii. Lakini pindi tu mtu anajua wewe ni mmasai anaanza dharau za ghafla. Kama vile umejinyea. Shida ni nini wandugu? Au kwa sababu tunavaa lubega? Sisi wote ni watanzania.

UPDATE 29.11.2016
Wamasai wengi ni watu wenye uelewa mkubwa kushinda makabila mengi hapa nchini, hususani wavaa KOBAZI na washindia ubwabwa, kutwa kuongeza wake huku nguvu zenyewe hamna. ACHENI DHEREU.
Unalalamika ubaguzi,ilhali na wewe unafanya ubaguzi?
 
me sipendi tabia yako ya kupandisha mori na kupiga watu ovyo utakuta aliyemchokoza mwengine lakini atayepita karibu halali yake,hata serikali imenyoosha mikono,huoni inawaachia mtembee na silaha huku mkihatarisha usalama(wa kabila lingine akitembea na silaha inakuwa kesi kubwa) na mambo yenu ya kudharau wakulima kulisha mifugo popote hadi mnasababisha mapigano ya kutisha.
 
Masai yuko salon yangu anasuka pouwa. Ila akingia kingi anasuka bulee mteja anaondoka then anasema mama yeyoo....iyo ngumusi nitakuja enhee? Sheeyyyyweeee
 
Papaa masai...hivi hawa jamaa hua wanahudhuria misiba kweli? Sema masai wengi bado sana wanaamini vitu ambavyo vimepitwa na wakati itawachukua miaka mingi kufikiri na kutenda kisasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Muhudumu wa Bar: Karibu
Masai: Asante
Muhudumu: Nikuhudumie nini.
Masai: Nataka bia ya baridi..
Muhudumu: Bia gani?
Masai: Ile yenye chui
Muhudumu: Hii hapa nifungue?
Masai: Fungua
Muhudumu: Haya nimefungua karibu.
Masai: Kwenye hii glass pima ya bia 200 na inayobaki uzia rafiki ingine..
Umetisha!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Halafu eti kwanini wengine ni wakorofi kupenda kwenda kuingiza mifugo yetu kwenye mashamba ya wakulima?
Hamuoni ni ukorofi mkubwa na uchokozi?
Halafu kisha mmewaweka viongozi mkononi wa vijiji kwa kuwa mnajua wakati wowote mkiuza mnyama mnapata pesa?
Je mngekuwa ninyi ndo wakulima mkawafinyiwa hivyo mngejisikiaje ?


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Halafu kwani ndani ya jamii ya wamasai wanawake ni wachache?
Kwanini huwa mnaoa vitoto vidogo?
Kwani wakubwa waliokwisha vunja ungo hawapo ili kusudi muwaache hao wadogo wakue kwanza kiasi cha kuvunja ungo na kufikisha miaka 18?


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom