Sinai
JF-Expert Member
- Jan 20, 2011
- 288
- 47
Leo hii asubuhi nikiwa ktk daladala, niliwasikia akina dada wanaongelea mambo yao ya jana usiku, mmoja akiwa anamweleza mwenzake kuwa, baada ya kuona jamaa anamwangalia kwa ishara ya kumtamani, na huku akiwa anatoa wallet iliyotuna kulipia vinywaji, mdada akaamua kumwomba kaka yule wakae meza moja! Kisha alipo pewa ruksa, akaanza kumlegezea hadi jamaa akatia timu, cha ajabu walipoenda kunako mambo, yule dada hakulipwa chochote na wala jamaa hakuwa na pesa kama yule dada alivyozania! Yule dada akasema wanaume wengine bwana, washenzi sana wana mawallet makubwa kumbe hayana kitu ndan! Hivi akina dada, kwanini macho yenu yanaelekezwa zaidi kwenye wallet za wanaume kuliko upendo wa kweli???????????