Wana jamvi, kabla ya yote niseme kwamba nilikuwa mwanachama wa CCM.
Nimeamua kuvua magamba niliyokuwa nayo CCM na sasa naangalia upepo unavyokwenda nikiwa nje ya Chama Cha Magamba. Kifupi ni kuwa nimekichukia vibaya as if sijawahi kuwa mwanachama wake.
Zamani tulizowea kuwazushia uongo wapinzani kwa kuwaita wakabila(Enzi za NCCR na CDM), wadini(CUF), wajimbo(UDP) na pia kusema kuwa wapinzani wanaendesha vyama vyao kama kampuni.
Leo hii tuhuma zote mbaya zipo CCM. CCM ni waroho wa madaraka(tazama sasa wanavyotoana macho kwa ajili ya urais). CCM ni waroho wa fedha na wachumia tumbo(tazama issue ya posho za vikao zilivyowatoa roho).
Mzee Malecela mwaka 1995 aliwahi kukaririwa akisema, CCM itatawala miaka 50 mbele, akiwa na maana hadi mwaka 2045. Nadhani mzee huyu alikosea hesabu na inawezekana alikusudia CCM itatawala mwisho 2010.
Tazama, Samwel Sitta anawananga wabunge wa upinzani ambao walikuwa wanachukua sitting allowance ktk bunge lililopita. INANISHANGAZA. mzee huyu amezeeka vibaya sana. Kwani haiwezi kutokea mtu akawa muovu lakini baada ya muda akaamua kuacha uovu na kumrejea Mungu wake? UBAYA UKO WAPI!!! Mbona yeye aliwahi kumuita naibu spika wake kuwa ni mtu wa kukurupuka lakini baadae alimuomba radhi na akasamehewa.
Sasa hivi ni aibu kwa kijana kuwa CCM, labda kwa wenye vyeo kama Nape, Januari, Bashe, Malisa na wengine kama wao. Leo hii si ajabu kukuta mtu anakwenda kwenye kikao cha UVCCM akiwa na nguo mbili. Moja(ya kawaida) anaivaa pindi akitoka nyumbani na wakati wa kurudi na ile inayoonesha kuwa ni mwanaCCM anaivaa katika kikao tu, akitoka anaivua na kuiweka ktk begi.
NIMETAFAKARI KWA UMAKINI, NA KWA MUDA SASA. CCM haitufai. Nakaa pembeni
Nimeamua kuvua magamba niliyokuwa nayo CCM na sasa naangalia upepo unavyokwenda nikiwa nje ya Chama Cha Magamba. Kifupi ni kuwa nimekichukia vibaya as if sijawahi kuwa mwanachama wake.
Zamani tulizowea kuwazushia uongo wapinzani kwa kuwaita wakabila(Enzi za NCCR na CDM), wadini(CUF), wajimbo(UDP) na pia kusema kuwa wapinzani wanaendesha vyama vyao kama kampuni.
Leo hii tuhuma zote mbaya zipo CCM. CCM ni waroho wa madaraka(tazama sasa wanavyotoana macho kwa ajili ya urais). CCM ni waroho wa fedha na wachumia tumbo(tazama issue ya posho za vikao zilivyowatoa roho).
Mzee Malecela mwaka 1995 aliwahi kukaririwa akisema, CCM itatawala miaka 50 mbele, akiwa na maana hadi mwaka 2045. Nadhani mzee huyu alikosea hesabu na inawezekana alikusudia CCM itatawala mwisho 2010.
Tazama, Samwel Sitta anawananga wabunge wa upinzani ambao walikuwa wanachukua sitting allowance ktk bunge lililopita. INANISHANGAZA. mzee huyu amezeeka vibaya sana. Kwani haiwezi kutokea mtu akawa muovu lakini baada ya muda akaamua kuacha uovu na kumrejea Mungu wake? UBAYA UKO WAPI!!! Mbona yeye aliwahi kumuita naibu spika wake kuwa ni mtu wa kukurupuka lakini baadae alimuomba radhi na akasamehewa.
Sasa hivi ni aibu kwa kijana kuwa CCM, labda kwa wenye vyeo kama Nape, Januari, Bashe, Malisa na wengine kama wao. Leo hii si ajabu kukuta mtu anakwenda kwenye kikao cha UVCCM akiwa na nguo mbili. Moja(ya kawaida) anaivaa pindi akitoka nyumbani na wakati wa kurudi na ile inayoonesha kuwa ni mwanaCCM anaivaa katika kikao tu, akitoka anaivua na kuiweka ktk begi.
NIMETAFAKARI KWA UMAKINI, NA KWA MUDA SASA. CCM haitufai. Nakaa pembeni