Waliouziwa mashamba Mkuranga wametapeliwa

Sabasaba

Senior Member
Jul 12, 2007
102
54
Hii inakuwaje jamani, sheria ya umiliki ardhi kama mashamba inasemaje kuhusu hili wadau?

Serikali wilayani hapa Mkoa wa Pwani, imesema baadhi ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, waliouziwa mashamba katika kijiji cha Mwanzega wametapeliwa kwa sababu haijashirikishwa katika zoezi hilo.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa Wilaya hiyo, Henry Clemens wakati akizungumza kuhusu kukamatwa kwa Mwenyekiti wa Kijiji hicho na Jeshi la Polisi Wilaya ya Mkuranga kwa mahojiano zaidi huku mtendaji wake akisakwa baada ya kutoroka kuhusiana na uuzaji wa mashamba hayo kiholela.

Alisema makundi ya watu kutoka jijini humo yamekuwa yakimininika wilayani humo kununua mashamba katika kijiji hicho bila ya serikali hiyo ya Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga kuwa na taarifa.

Clemens, alisema makundi ya watu kutoka jijini humo yamekuwa yakimiminika katika kijiji hicho kupitia taasisi moja kwa lengo la kukabidhiwa mashamba ambayo imedai imewatafutia wakati si kweli.

"Wilaya ya Mkuranga haina ardhi kama hiyo, wilaya ipo karibu na jiji la Dar es Salaam, inapaswa kupangwa vizuri ili ilete manufaa kwa watu wa Mkuranga kwa wanaotaka kuja wafuate taratibu kwa kupitia halmashauri, wasipitie katika asasi wasipitie kwa mtu wa kati lazima ardhi itolewe kwa uhalali," alionya mkuu huyo.

Clemens, alisema mwishoni mwa wiki watu 1,000 kutoka Dar es Salaam walifika wilayani humo na magari mengi wakidai wameletwa na taasisi hiyo kukabidhiwa mashamba ambayo imewatafutia bila ya tarafa, kata halmashauri na wilaya kufahamu mpango huo.

"Kuna umuhimu wa kujua ardhi kama ilitolewa kiuhalali je kuna watu wangapi watafika katika kijiji hicho kwa malengo yapi,licha ya kupewa ardhi lakini kijiji kina mamlaka ya kutoa eka 50 wakati watu wapo 1,000 halmashauri ndiyo yenye uwezo wa kutoa ekari 100 zaidi ya hapo ni wizara, kwa hiyo ekari 50 ndio zitakuwa halali hao wengine watapelekwa wapi? " Alihoji. Alisema uongozi wa wilaya hiyo uliwazuia watu waliouziwa baadhi ya mashamba wasifanye kitu chochote kwa vile kuna matatizo ya mipaka baina ya kijiji hicho na jirani cha Msorwa.

" ... tayari uongozi wa taasisi hiyo umeandika barua ya kuomba radhi kwa wilaya kwa usumbufu na wilaya imeridhia lililojitokeza na mambo mengine yataendeshwa kwa taratibu na sheria za ardhi zilizopo,tunataka amani iwepo siku zote" alisema.


Source: IPP media
 
Wabongo wengi hata wasomi twapenda njia za panya (short-cuts), na ndio maana maendeleo ya nchi yamekuwa duni kutokana na mambo kama haya ya kienyeji yanayopelekea kutiana hasara kiuchumi.


Sheria ya Ardhi ya Vijiji (The Village Land Act) 1999 inatambua mamlaka ya Vijiji kumiliki Ardhi kupitia hati Maalumu (derivative right ) na inaweza kugawa ardhi hiyo kwa mtu au jumuiya yeyote awe wa ndani au nje ya Kijiji husika kwa kuzinagtia utaratibu maalum uliowekwa na sheria.

Sheria yatamka haya hapa kwa lugha ya Kitaalamu:


Section 12.-(l) A Village land shall be divided into-
(a) ......


(b) land which is being occupied or used by an individual or family or
group o. f persons under customary law; or


(c) land which may be made available for communal or individual occupation and use through allocation by the village- council in accordance with the provisions of this Part.

(2) A Village land referred to in paragraphs (b) and (c) of subsection (1) may be made the subject of a grant, in accordance with the provisions of this Part, by a village council to the occupier of that land or a citizen who is a villager or a group of citizens who are villagers or any other citizens who may be provided for in this Part, of a customary right of occupancy, by means of a document to be known as a certificate of customary title.


(3) A Village land referred to in paragraph (c) of subsection (1) may be made the subject of a derivative right granted by a village council in accordance with the provisions of this Part.



22 (2); A person or group of persons not ordinarily resident in a village may apply for a customary right of occupancy.
(3) An application for a customary right of occupancy shall be-
(a) made on a prescribed form-
(b) signed- (i) by the applicant; or (ii) where the application is made
by a family unit,.............


(iii) where the application is by a group of persons recognised as such under customary law, by not less than
two persons who are recognised by that law as leaders or elders of the group;



23-(1) A village council shall within ninety days of the submission of an application or within ninety days of the submission of further information or a satisfactory explanation for its non-availability, determine that application.




(2) In determining whether to grant a customary right of occupancy, the village council shall-

(a) comply with the decisions
that have been reached by any committee or other body on the adjudication of the boundaries to and rights in the land which is the subject of the application for a customary right of occupancy;



(b) have regard to any guidance from the Commissioner concerning an application from a non-village

organisation;
(d) where the application is from a non-village organisation, the village council shall seek guidance from the Commissioner who shall have regard to-


(i) any advice which has been given to the application by the district council or as the case may be the urban authority having jurisdiction in the area where the village is situate;

(ii) the contribution that the non-village organisation has made or has undertaken to make to the community and public facilities of the village;







SWALI: Je, hilo shirika lilikuwa na umiliki halali wa ardhi ya kijiji wakati likikusanya wakazi wa Dar kuwapeleka Mkuranga kuwamegea maeneo?. Lilifuata taratibu husika?, na hao wenzetu waliokusanywa na kupelekwa huko pengine kwa gharama kubwa, waliuliza mapema kujua hadhi ya hilo shirika juu ya ardhi ambayo iliwamegea?.




 
kikubwa ni kuhakikisha unapitia serikali ya kijiji unapotafuta ardhi ya kununua. tena ni vema kujiridhisha hata kabla ya kutoa fedha. ., lakini tukumbuke kuna aina mbili ya ardhi katika kijiji. kwanza ni ardhi ambayo inamilikiwa na mtu binafsi na pili inayomilikiwa na serikali ya kijiji. kama unanunua kwa mtu binafsi ni vema ukajiridhisha kwa kijiji kama kweli ardhi ya muuzaji ni yake kihalali au la. kama unataka kuomba ardhi ya kijiji basi ni kufuata taratibu zilizoainishwa katika sheria (ila urasimu wake mhhhhh!!- kutegemea na uongozi wa kijiji husika).
 
Mmmmmmhhhhh

jamani mjini humu akuna adabu kabisa kuna watu unawaona unawaheshimu kumbe ni wahuni kupindukia.....kama mmesikia hivi karibuni kuna chama cha wasanani wakawaita wasanii na kuwambia wachange sh 53,000 ati wanagaiwa kiwanja..hamad na mimi nilikuwa niingie mkumbo huo aliekuja akdai sio tu wasanii hata wenye biashara ndogo na ndogo na kampuni zao...mi nikasema jamani kiwanja 53000 cha wapi hicho

hatimae jana mkuu wa iwlaya ya kisarawe ametoboa kuna matapeli wamekuja wakadai wanataka uhusiano na kisarawe kama wasanii..baaada ya muda wakaenda kuwarubuni baadhi ya wananchi wawauzie viwanja vyao ...baadhi ya wanakijiji wakakimbilia hapa kwetu makao makuu ya wilaya na kutuuliza kuna jambo kama hili ni kweli

hakika napenda kuwambia ukweli huyo anaejiita mwenyekiti alikuja kwangu akadai anataka kununua sehemu ya kisarawe tukmwambia imemilikishwa na halmashauri na si ya watu binafsi

akaondoka baadae tukaja ambiwa hayo mambo nikampigia akujibu kabisa naomba niwaweke wazi watanzania akuna ardhi ya wasanii hata moja kisarawe imejaa ...na hao waliochukua hela zenu pelekeni mahakamani
namnukuu mh

majuzi kibonde katk kipindi chake cha jahazi ailisifia kusikia wasani kupewa ardhi na gadna akasema alikuwa mmoja waliopewa na kuonyeshwa na kusifia ni nzuri sana watakuwa pamoja kibonde akaomba radhi alitinwa akuweza kwenda ila alishalipa na akipata nafasi ataenda kuona hekari zake...
Jamani wasanii msipendee cha bure nendeni mbweni huko mkatoe mamilion hekari nzuri ufurahie ardhi yako hivi vya bure vinaua

naomba serikali mfwatilie na kuwakamata wote waliohusika kuchukua hela za watu warejeshewe kabla hukumu ya mungu aijawaangukia...naamini kuna wasaanii nao wamehusika kwenye hili tujulishwe liwe fundisho
 
mmmh nguli hebu njoo utuambie hii kitu.................ina maana uongo?! Msanii njoo utupe habari hii plz
 
mmmh nguli hebu njoo utuambie hii kitu.................ina maana uongo?! Msanii njoo utupe habari hii plz

mkuu req taarifa ya jaba ya habari wakutumie tbc ndio uamini mi chiongei..pole kama ...
 
Hiyo hela ni ndogo sana.

Watu tumeliwa kwenye Hisa za NICOL na tumekaa kimya tu. Au kwakua hao wanafahamika!?
 
hiyo hela ni ndogo sana.

Watu tumeliwa kwenye hisa za nicol na tumekaa kimya tu. Au kwakua hao wanafahamika!?

mkuu kwakuwa umeliwa hela kubwa tukae kimya matapeli waendelee kutuibia anyway pole kwanza nahisi mpaka deci ulikuwepo
 
Jamani bora hao waliotoa 53 elfu sisi tulitoa laki 1 tena noti za elfu 10. 10. Naelekea Mwananyamala hospital kucheki presha kichwa kinauma sana. Msanii wa JF ni kati ya watu wakutafutwa na polisi ngoja niweke evedence hapa.
 
Jamani bora hao waliotoa 53 elfu sisi tulitoa laki 1 tena noti za elfu 10. 10. Naelekea Mwananyamala hospital kucheki presha kichwa kinauma sana. Msanii wa JF ni kati ya watu wakutafutwa na polisi ngoja niweke evedence hapa.

pole Nguli, kwani c muwakamate hao waliopokea hizo pesa?
 
Sishangai kuona hata wasanii na waandishi wa habari wakipigwa bao, katika kila jambo unaloambiwa lazima ulichanganue na kulipeleleza ili uone kama kuna ukweli wowote, kila sehemu zina mamlaka yake kuanzia mkoani hadi kijijini, sasa hao hawakutafuta uhalali wa hicho kitu kisha wanamuamini mwenyekiti wao, hii sio sahihi na ni lazima ujue sasa dunia imeisha so hakuna kumuamini mtu kirahisi.

Poleni sana, mmempa mtu hela ya kula, fikiri kama mpo 500*53,000 ni shilingi ngapi? Kuweni makini jamani na kuwa wepesi kupembua mambo.
 
Mbaya zaidi kuna wale matapeli wa TEDET (Ofisi yao iko pale mnazi m1), walidanganya wananchi kuwa wanatoa ekari 5 kwa laki mbili tu, matokeo yake watu kibao walitoa na kupelekwa huko nyamwage Rufiji 'kuoneshwa' ekari zao.

Then what happened??? Kuna michango ya ziada kibao, ambayo inafanya bei ya hizo ekari kuwa zaidi ya milioni 2!! teh, na bado hakuna mtu aliyepata kiwanja kudadadeki!! Natamani kuwachoma moto yule tapeli anayejiita Dr. Mugishagwe na wenzake... inaniuma sana wadau..:confused2:
 
Mbaya zaidi kuna wale matapeli wa TEDET (Ofisi yao iko pale mnazi m1), walidanganya wananchi kuwa wanatoa ekari 5 kwa laki mbili tu, matokeo yake watu kibao walitoa na kupelekwa huko nyamwage Rufiji 'kuoneshwa' ekari zao.

Then what happened??? Kuna michango ya ziada kibao, ambayo inafanya bei ya hizo ekari kuwa zaidi ya milioni 2!! teh, na bado hakuna mtu aliyepata kiwanja kudadadeki!! Natamani kuwachoma moto yule tapeli anayejiita Dr. Mugishagwe na wenzake... inaniuma sana wadau..:confused2:


na wewe pia umeuvaa mkenge?
 
Elimu....vitu vya bure vina madhara..naskia waliahidiwa watajengewa na nyumba na kikwete..nilimshangaa lakini nilijua elimu ni muhimu
 
Elimu....vitu vya bure vina madhara..naskia waliahidiwa watajengewa na nyumba na kikwete..nilimshangaa lakini nilijua elimu ni muhimu

Inaonekana wewe huishi Tanzania na ungekuwa unaishi TZ usingesemaa hayo uliyosema! Eti tunapenda raisi?
 
....wengi walishauvaa mkenge kwenye hizi mambo za ardhi wandugu....nashangaa watu hatujifunzi kutoka kwa wengine.......!
 
Mbaya zaidi kuna wale matapeli wa TEDET (Ofisi yao iko pale mnazi m1), walidanganya wananchi kuwa wanatoa ekari 5 kwa laki mbili tu, matokeo yake watu kibao walitoa na kupelekwa huko nyamwage Rufiji 'kuoneshwa' ekari zao.

Then what happened??? Kuna michango ya ziada kibao, ambayo inafanya bei ya hizo ekari kuwa zaidi ya milioni 2!! teh, na bado hakuna mtu aliyepata kiwanja kudadadeki!! Natamani kuwachoma moto yule tapeli anayejiita Dr. Mugishagwe na wenzake... inaniuma sana wadau..:confused2:

Ni DR. HAJI MUGISHAGWE?:mad2:
 
Elimu....vitu vya bure vina madhara..naskia waliahidiwa watajengewa na nyumba na kikwete..nilimshangaa lakini nilijua elimu ni muhimu


Umenena............ni paka pale watu mtakapoelewa kuwa MTakula kwa jasho lenu......................!
Lakini nawapa pole mmejifunza kwa njia ngumu!
 
Hayo ni matokeo ya Serikali kutokuwa na utaratibu madhubuti wa ugawaji viwanja. Matapeli wanaingilia hapohapo!
 
Back
Top Bottom