Waliomuua Dr.Mgimwa hawa hapa

Waliomuua Dr.Mgimwa hawa hapa

nzobhe

Member
Joined
Dec 8, 2013
Posts
51
Reaction score
58
Sasa imebainika wazi waliomuua aliyekuwa waziri wa Fedha Dr.Mgimwa.

Watuhumiwa hao walitumia ustadi na umakimi wa hali ya juu kuhakikisha kuwa huyu waziri anaondoka katika nafasi ya Waziri wa Fedha kwani anaziba mirija ya uchotaji wa fedha za Escrow. Hata mabepari hao inasemekana walianza kupiga ndogondogo kwa mkubwa (prezdaa) Mgimwa aondolewe ktk nafasi hiyo na apewe mmoja wa wabunge (ambaye amepata mgawo wa fedha hizo kwa sasa.)

Ilikuwa hivi-Kuanzia mwaka 2012 baada ya kuwa waziri wa fedha Dr.Mgimwa alianza kuandamwa na kufuatwa na mabepari hao ili wajadiriane kuhusu pesa za escrow account lakini kwa uzalendo wake alikataa katakata pesa hizo kutoka na kulipwa huyo Singasinga na Washirika wake.

Baada ya kuona kuwa ameziba kila sehemu na njama zao kugonga mwamba wauaji hao walimuwekea sumu ambayo inasemekana iliwekwa kwenye maji ya kunywa na hapo ndipo Dr.mgimwa alipatwa na ugonjwa wa ajabu na kushindikana kutibiwa hapa nchini mwisho wake wakampeleka nchini Afrika ya kusini ambapo aliugua huko kwa muda wa miezi takribani 3 akaaga dunia.

🙊USHAHIDI wa MAUAJI HAYO🙈
Ikumbukwe kwammba Dr.Mgimwa alipelekwa Afrrika ya Kusini kutibiwa kati ta mwezi wa august na septemba 2013 na hakurudi mzima, na huu ndiyo ulikuwa muda (sept-december 2013 ) ambao mchakato wa malipo ya fedha za ESCROW ulianza mpaka malipo yake yakafanyika.

Chanzo cha habari kinasema barua zote za kuanza nchakato wa malipo mpaka kukamilika kwa malipo hayo yalikuwa ktk kipindi hiki (sept-december,2013) ambacho Dr.Mgimwa alikuwa hayupo na baada ya kuonekana ni kigingi kwa fedha hizo kutoka.

Ndugu zangu, Fedha hizo zilichotwa kiulani kipindi Waziri wa sasa wa Fedha Saada Mkuya akiwa Naibu waziri wa Fedha,hivyo hili saga na yeye analijua vizuri sana na inasemekana wabunge wameshamwambia aachie ngazi kabla fagio lao litakapofika.

Hivyo tarehe ya kuanza kuugua na kusafirishwa kwenda Afrika Kusini na tarehe ta kuchotwa pesa za umma.
Masikini Mgimwa alijitahidi kuwatetea watanzania katika kuzuia wizi huo lakini mapepali wakamshinda,leo Mungu anawaumbua...

My take..serikali uchunguze kwa kina kifo cha Dr.mgimwa sambamba na kuchotwa fedha za Escrow

Pili,waziri wa sasa wa Fedha awajibishwe kwani anahusika kwa namna moja au nyingine.
 
Mh tutaona mengi hadi ya siku ya uchaguzi mkuu utakapowadia.
 
Hii habari ya UKWELI.....ESCROW monies killed Dr. Mgimwa....hata Kafulila kasema mara nyingi sana kuhusu hili...!!!!

So Tanzania, ni zaidi ya uijuavyo....TUTAFANYA MAKOSA MAKUBWA SANA KTK KATIBA PENDEKEZWA tukiipitisha, kwani ikiwa kuanzia Rais, Waziri Mkuu hawataweza KUSHTAKIWA ikiwa walifanya maovu in public offices MARA BAADA ya kustaafu ni KOSA KUBWA SANA.....

=> Haya yote yataisha ikiwa tu RASIMU YA KATIBA ya Jaji Warioba ITARUDIWA UPYA BUNGENI....!!
 
Wako wapi wewe mtoa mada acha uboya

Lisemwalo lipo, kama halipo lipo nyuma linakuja. Hata wakati ESRCOW inaibuliwa kuna watu waliitwa tumbili. Hata kashfa ya Buzwagi zito alikula adhabu ya kufungiwa kuhudhuliria vikao vya bunge kwa madai kuwa ni mzushi. hatakashwa zingine ilibidi ziibuliwe Mwembe yanga baada bungeni kunyimwa nafasi kwa madai kuwa ni waongo na wanataka kuigawa nchi. The time will tell, is just matter of time!
 
Ilikuwa hivi-Kuanzia mwaka 2012 baada ya kuwa waziri wa fedha Dr.Mgimwa alianza kuandamwa na kufuatwa na mabepari hao ili wajadiriane kuhusu pesa za escrow account lakini kwa uzalendo wake alikataa katakata pesa hizo kutoka na kulipwa huyo Singasinga na Washirika wake.

= wajadiliane
 
Back
Top Bottom