Waliomalima VETA basic driving wanacheleweshewa vyeti vyao.

Waliomalima VETA basic driving wanacheleweshewa vyeti vyao.

Monomer

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2023
Posts
683
Reaction score
1,263
Naombeni hii post mods mnisaidie kuiweka kwenye kero.Dira ya maendeleo 2025-2050 inasema elimu na ujuzi kwa maendeleo ya taifa na katika hilo waziri mkuu aliepita alishauri na kusistiza sana watu waende veta wakachukue juzi mbalimbali.

Katika hao walioitikia huo ushauri Kuna wengine wamechukua driving kwa malengo mbali mbali.Cha ajabu ni kwamba Vyeti vyao ambavyo vinawatambulisha kwamba wamehudhuria na kufuzu mafunzo ya awali ya udereva katika chuo kinachotambulika na serikali hatimae waweze kuvitumia kukata lessen wanacheleweshewa.

VETA TANGA Kuna intake kama 5 zote zinasubiria vyeti waalimu wenyewe hawajui vinatoka lini,wao wanakwambia kazi Yao ni kufundisha tu kama unataka maelezo zaidi onana na uongozi wa juu uulize.

Sasa naomba kuiuliza veta makao makuu ni nini kinapelekea ucheleweshaji huu wa vyeti ukizingatia kwamba ili uruhusiwe kukata lessen ni lazima uwe na lessen hai ya awali ya kujifunzia ambayo nayo Ina expire baada ya miezi 3.

Kwa sababu walimu muda mwingine wanakwambia changhamoto haziko chuoni bali ziko veta makao makuu kwamba anaehitajika kuvisign hivyo vyeti ni mtu mmoja ambae nae anamajukumu mengi.Kwa hivyo ili kurahisha utendaji kazi Mimi naomba utaratibu urejelewe upya vyeti viwe vinapatikana kwa urahisi eneo husika.Ila tu uwekwe mfumo mpya wa kuzuia kugushi.
 
Mimi naona ni veta na veta veta mkoa wa kagera ndani ya mwezi mmoja unapata cheti.

Hakuna malimbikizo ya intake
Alafu leseni ipi ina expire baada ya miezi mitatu?
 
Mimi naona ni veta na veta veta mkoa wa kagera ndani ya mwezi mmoja unapata cheti.

Hakuna malimbikizo ya intake
Alafu leseni ipi ina expire baada ya miezi mitatu?
Lessen ya learner(ile unayokata mwanzo pale unapokua umeanza mafunzo kwa vitendo)
 
Back
Top Bottom