Waliojenga mwaka 2021 tunaomba uzoefu wenu

August tena...hio kama ingekua yangu nahamia
Boss hapo navuta nguvu niweke wiring ndo nifunge bod na vigae also aluminium za madirisha.
Unaweza ona kazi bado boss wangu
IMG-20211030-WA0016.jpg
 
1.KIWANJA
Hakikisha unachagua kiwanja kizuri in terms of landscape na accessibility! Chaguzi sahihi ya kiwanja upunguza gharama za ujenzi so kuwa makini mwanzo kabsa wakt unanunua kiwanja.
2.RAMANI
Watu wengi upenda kuchukua ramani(copy n paste) na kuanza ujenzi bila ya kufanya uchunguzi wa ramani husika kutokana na uwezo wake au mahitaji yake! Hakikisha kama sio mtaalamu mtafute hata mtaalamu mkae muitafsiri ramani na kujadiliana juu ya ramani zima iendane na mahali unapojenga!
3.KONA
Make sure unapunguza nyumba yako kuwa na kona nyingi zisizo na ulazima kwan kona nyingi uongeza kuta, idadi ya bati na mbao za kenchi, na kufanya gharama za nyumba kupanda.
4.MABADILIKO NJIANI
Hakikisha kbla ya kuanza ujenzi ushajua nyumba yako itakuaje na ukubaliane nayo! Epuka kufanya changes midway(kubadilisha wakati ushaanza)
5. FUNDI
Hakikisha unapata fundi mzuri wa kufanya kazi yako na unapochagua fund factor yako isiwe bei tu, usimpe fundi kaz eti kisa ana bei ndogo go extra mile (kwenye engineering tunaamin kuna mahusiano makubwa kati ya cost n safety hvo vitu ni direct proportional)
Pia jitahidi fundi wako atoke maeneo ya unapofanyia ujenzi kuliko kumtoa mbali
6. KUKODI BADALA YA KUNUNUA
Makes sure baadhi ya vitu ambavyo unaweza kuvpata kwa kukodi unafnya hvyo instead ya kuvinunua mfano Mbao za formwork, mapipa ya maji, formwork za nguzo, sahani kwa ajili ya madirisha, mirunda etc
7.UWEPO SITE MUDA MWINGI
Hata kama ujui abc za ujenzi hakikisha wakat wa ujenzi unatenga muda mwingi wa ww mwnyewe kuwepo site na kuobserve kila kitu kama unaweza kupata hyo nafasi.
8.KUTOJENGA KWA AWAMU NYINGI
Ni kwel ujenzi gharama sana lakni hakikisha ukianza ujenzi usijenge kwa awamu nying sana kama una kipato kidgo bas nunua hata material kwanza then ukianza at least ujenge kwa awamu nne (msingi,boma,kupaua,finishing) kujenga kwa muda mrefu au ile ukipata laki unaita fundi ni gharama zaidi.
9.BAJETI
Hakikisha kabla ujaanza unajua bajeti aghalau ya makadirio ya nyumba yako mpka kukamilika na kama una uwezo huo! So ili ujenzi usikusumbue zaidi hakikisha unajenga nyumba ya kipato chako.
10.LAYOUT
Hapa namaanisha mpangilio wa vyumba, hakikisha unaweka vyumba vinavyofanana sehemu moja, nakupa mfano vyoo (master na public),jiko,dining kwa sababu lazima viwe connected na mfumo wa maji taka ni vzr uviweke kwenye sehemu moja au karbu hi itakupunguzia cost wakat wa plumbing kuliko kuviweka mbali mbali.
Kwa maneno rahis vyumba vyenye tabia za kufanana vikae karibu.
11.MATERIAL
Uchaguzi sahihi wa material za kujengea! Mfano ni vizur kujengea ile kokoto nyeusi ambayo haina vumbi( utumia saruji kidgo zaidi kutengeneza zege zuri kuliko ile kokoto nyekundu), mchanga(ukitaka kujua mchanga mzuri uchukue mkononi then ingiza mkono wako ndani ya ndoo kama mchanga ujaondoka wote kiganjani kwako au aujakuwa tope basi ni mzuri) Maji ya chumvi sio mazuri kujengea etc

So hizo ni baadhi ya tips na wengne naamini watashare tupate kujifunza zaidi
Hii imekaa vizuri mkuu. Umesema so vyema kujengea maji ya chumvi. Sisi wakazi wa Dom kwa kiasi kikubwa tuna maji ya chumvi. Unashaurije?
 
Ndio nmejenga na shimo la choo tena kwa tofali zile za round nmenunua moja 1200 na ni included kwenye hyo hyo 10m.

Hongera sana mkuu. Naomba kuuliza, tofali za kulala kabla ya mkanda wa chini ( za msingi zilikua nnchi ngpapi na ziliteketetea ngapi?

Mkanda na linter zote umetumia nondo tatu au nne?

Naona kama umefanikiwa sana kupata vitu bei rahisi.

Ardhi yetu mfinyanzi 10 iliteketea kwenye msingi tu, ikijumuisha kifusi cha kuweka sawa.
 
Hongera sana mkuu. Naomba kuuliza, tofali za kulala kabla ya mkanda wa chini ( za msingi zilikua nnchi ngpapi na ziliteketetea ngapi?

Mkanda na linter zote umetumia nondo tatu au nne?

Naona kama umefanikiwa sana kupata vitu bei rahisi.

Ardhi yetu mfinyanzi 10 iliteketea kwenye msingi tu, ikijumuisha kifusi cha kuweka sawa.

Tofal za msingi kama 1300 za inch 5, nmetumia nondo tatu tatu juu za 12mm na chini za 10mm kwenye nguzo za barazani ndio nmeweka nondo nne nne!
 
Hongera sana mkuu. Naomba kuuliza, tofali za kulala kabla ya mkanda wa chini ( za msingi zilikua nnchi ngpapi na ziliteketetea ngapi?

Mkanda na linter zote umetumia nondo tatu au nne?

Naona kama umefanikiwa sana kupata vitu bei rahisi.

Ardhi yetu mfinyanzi 10 iliteketea kwenye msingi tu, ikijumuisha kifusi cha kuweka sawa.
Ni kweli kabisa, mimi pia msingi na rinta pamoja na kifusi tu ilishakatika zaidi ya m7, sijui jamaa ametumia mbinu gani kufika hapo kwa m10? daahh
 
Back
Top Bottom