Waliochota Pesa ESCROW Stanbic hawa hapa

Waliochota Pesa ESCROW Stanbic hawa hapa

ccm ya sasa hakuna mwadilifu tena
 
Tatizo si magezeti ya kibongo, ila tatizo ni mfumo wa kulindana na katiba ya sasa inayolinda watawala wasinyoshewe kidolge kwa lolote, Mtajwa mmojawapo kama ni mke wa Kigogo wa Juu pale Ikulu ujue analindwa na katiba ya sasa hivyo vigumu kwa mazingira ya kibongo kumwanika hadharani. Ingwa jina laeleweka maana vigogo wa Juu wanaoishi Ikulu si idadi ya kuhesabu bali ni familia moja, vinginevyo wengingine wanaingia kikazi na kutoka si makazi yao na wengine ni watumishi tu.

Umeandika ngazi za juu na sio anaishi ikulu!!!!
 
Hili gazeti la Raia Mwema nalo limekuwa kama lile la Majira, wameshindwa nini kumtaja huyo kigogo wa Ikulu wakati alishstajwa siku nyingi anaitwa Rashid Gurumo, huu ndio Uandishi Pasipo Elimu (UPE)
 
Mi naona bora wenye acess ya kuiba waendelee kuiba,kwa maana watafichwa fichwa kuanzia kwenye vyombo vya usalama mpaka media
Thats the bottom line.
Kama unaweza kuchota usionekane so be it, CHOTA!!!
Thats the noral of escrow!
 
Hawakuwa na ulazima wa kuandika hiyo habari kama bado TAKUKURU wanafanya kazi yao...Nilitegemea waliposema majina haya hapa,wasingesita kuyataja. ...salima. ..salama nk. ...

Huyo mke wa kigogo ataharibu uchunguzi, wengine hawaharibu....!
 
Ukimya wa Ikulu ambao Katibu Mkuu alivyokingia kifua sakata hilo kuna dalili za Ikulu kuhusika. Umeona waliokaribu na Ikulu walivyonywea/

Mie nadhani gazeti liko sawa kabisa. Gazeti la uchunguzi haliandiki habari zake straight kwani zingine zinaweza kukiuka maadili ya kiuandishi. Hapa tunafahamishwa kuwa wapo wazito wanahusika na wajibu wa kuwataja moja kwa moja ni wa vyombo vya kisheria vyenye uwezo wa kuwashtaki mahakamani.
Hata hivyo habari hiyo inatosha kujulisha wananchi kuwa Ikulu ni Pango la wanyang'anyi na wahusika wameshindwa kujisafisha.
 
Jambo la maana.nikubadirisha serikali.bila hivyo wataendelea kuiba siku hadi siku.tarifa zitatoka hazitasaidia.
 
Si utaje majina yote kama unayajua?

Mke wa kigogo hana jina?

Wapi majina ya mawaziri nk?

Ndugu bongo tatizo unafiki mwingi. Mtu anasema waliochota fedha kupitia Stanbic hawa hapa, then anaseme jina tunalo kakini tunalihifadhi huo ndiyo unafiki unaosababisha nchi iendelee kutafunwa tu.

Kwa mwendo huo acha waitafune nchi tu hadi tutakapoacha unafiki.
 
Hii sredi ishakuwepo hapa na zaidi ni hewa tu haina lolote...

Yap niliona ina kama week hivi.
~Kiboko alikuwa kubenea angewataja wote waliokula mlungula kupitia Stanbic pamoja na miamala yao yote waliyofanya bring back our mwana.halisi
 
Mie nadhani gazeti liko sawa kabisa. Gazeti la uchunguzi haliandiki habari zake straight kwani zingine zinaweza kukiuka maadili ya kiuandishi. Hapa tunafahamishwa kuwa wapo wazito wanahusika na wajibu wa kuwataja moja kwa moja ni wa vyombo vya kisheria vyenye uwezo wa kuwashtaki mahakamani.
Hata hivyo habari hiyo inatosha kujulisha wananchi kuwa Ikulu ni Pango la wanyang'anyi na wahusika wameshindwa kujisafisha.

This needed a paper??!!!
 
Soma habari uielewe, kwamba ili kutoharibu upelelezi unaoendelea na TAKUKURU majina yamehifadhiwa. Lakini kuambiwa mke wa kigogo wa juu pale Ikulu aliondoka na gunia la pesa nini zaidi unataka? Kama ni Darisalama? Salmina? Salamania? Sadakiasa? Au Marejesho?

Salama
 
Nikiskia habari za ikulu kuhusishwa na ufisadi nakumbuka jinsi sugu alivyodhulumiwa mradi WA marelia kwa kutumia hii hii ikulu ...ikulu yetu now inatumiwa na majambazi kufanikisha mambo yao
 
Hii scandal itakuwa inagusa watu wakubwa sana, kwa nini kila mtu anapata kigugumizi kwenye hizi transactions(miamala) iliyofanyika benki ya Stanbic!? Sina imani na uchunguzi unaofanywa na hayo yanayoitwa "vyombo vya usalama" na kina Taasisi ya Kuchukua na Kula Rushwa(TAKUKURU) maana watafunika tu haya mambo ili kuwalinda wakubwa wao wa kazi
 
asingeandika majina haya hapa, je ungenunua gazeti, iloyotumika ni lugha ya kibiashara zaidi, japokua huu pia ni ufisadi tena mkubwa sana, jiulize ni watu wangapi walinunua gazeti hili akitegemea majina na details zimekuwa mention,

mwandishi amejitaidi kujinasua kwenye mtego wake baada ya kukuambia majina tunayahifadhi kwa sababu ya uchunguzi, pengine wajinga ndio waliwao
 
Back
Top Bottom