Walinzi wa Mlimani City wafanya mgomo wa kudai walipwe mishahara yao

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049


Nipo hapa Mlimani City ndani ya Jiji la Chalamila (Dar es Salaam), taarifa ikufikie kuwa vijana wa security yaani wale walinzi wanaovaa yale mashati maupe wameandaa maandamanonmadogo ya mgomo wa ndani ya jengo hilo, wanadai hawajalipwa mshahara, imekuwa kero, hiyo maandamano yasiyo rasmi yametokea jioni hii ya leo tarehe 6 Septemba 2023.

Jamani mabosi wa Mmlimani City tunajua mna mahela mengi tuhuko benki, hawa vijana wanafanya kazi kubwa, wanalinda vitu vingi vya thamani.

Mnashindwa kuwalipa mishahara kwa sababu gani? Tatizo Tanzania tumezoa kila kitu mpaka watu wafanye fujo kama hivi.

Hawa vijana wasaidiwe wasisumbue watu, hiyo security company inaitwa AS GUARD
 
View attachment 2741321

Nipo hapa Mlimani City ndani ya Jiji la Chalamila (Dar es Salaam), taarifa ikufikie kuwa vijana wa security yaani wale walinzi wanaovaa yale mashati maupe wameandaa maandamanonmadogo ya mgomo wa ndani ya jengo hilo, wanadai hawajalipwa mshahara, imekuwa kero, hiyo maandamano yasiyo rasmi yametokea jioni hii ya leo tarehe 6 Septemba 2023.

Jamani mabosi wa Mmlimani City tunajua mna mahela mengi tuhuko benki, hawa vijana wanafanya kazi kubwa, wanalinda vitu vingi vya thamani.

Mnashindwa kuwalipa mishahara kwa sababu gani? Tatizo Tanzania tumezoa kila kitu mpaka watu wafanye fujo kama hivi.

Hawa vijana wasaidiwe wasisumbue watu, hiyo security company inaitwa AS GUARD
Kwa wenye kutaka kuelewa, hiki k8nachoendelea ni mule mule kuonesha kuwa eneo la usimamizi na utawala maeneo mengi ya umma hayazingatii weledi, utu, tija wala haki.

Makundi madogo madogo kama hayo wanapofikia hali ya kuchoshwa na usumbufu wa kikundi kidogo cha watu ni picha kubwa ya nini kinakuja kujiri kwenye sekta zingine kubwa.

Unaweza kukuta Mlimani City wameilipa kampuni hela zao zote, lakini wenye kampuni hawwjawalipa mishahara wafanyakazi. Na kwa sababu kampuni imesajiliwa polisi na mmiliki ni polisi mstaafu.... basi kilio hicho ni kigumu kusikizwa na kifuatacho hao wote wanatimuliwa kazi..
 
Na kwa sababu kampuni imesajiliwa polisi na mmiliki ni polisi mstaafu.... basi kilio hicho ni kigumu kusikizwa na kifuatacho hao wote wanatimuliwa kazi..
NAKAZIA kuna watu ajira zao zipo mashakani hapo hasa wale frontliners wanaodai haki zao. Ndio nature ya private sectors nyingi za hapa nchini.

Ukionyesha misimamo ya kudai haki zako unaonekana adui.
 
Back
Top Bottom