Walimu walioshushwa vyeo na kusimamishwa kazi kisa Wimbo wa "Honey" warejeshwa kazini

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120
Walimu wawili wakuu wa Shule za Msingi Mlimani na Tunduma TC zilizopo Halmashauri ya Mji Tunduma Mkoani Songwe ambao walivuliwa vyeo kutokana na video iliyosambaa mitandaoni ikionesha Wanafunzi wakicheza wimbo wa Msanii Zuchu wa Honey, wamerejeshwa kwenye nafasi zao.

Akiongea na @AyoTV_ kwa njia ya simu leo Jumanne November 07, 2023, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji Tunduma, Philemon Magesa amethibitisha kuwa Walimu hao wamerejeshwa “Ni kweli taarifa hizo ni sahihi Walimu hao wamerejeshwa vyeo vyao"

Alipoulizwa sababu za kurejeshwa vyeo Walimu hao, Mkurugenzi huyo amesema “Walimu hao walivuliwa vyeo kutokana na maelekezo ya Waziri wa Elimu na wamerejeshwa kutokana na maelekezo wa Waziri wa Elimu"

Jana November 6, 2023 akiwa Bungeni, Spika wa Bunge laJamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt, Tulia Ackson aliishauri Serikali kuwarejesha kazini Walimu hao.
 
Ule wimbo wa nyege nyegezi ulipigwa ban nchini, kule uganda mheshimiwa aliserebuka nao ulipopigwa kuwaburudisha. Sawa walimu wamerudishwa kazini, kimsingi wao hawakuwa na hatia kwa sababu hawakujua ma dj wa wale watoa misaada shuleni kama wataupiga huo wimbo wa honey.

Ila watanzania tunapenda kusikiliza midundo tu ya nyimbo bila kujali maneno yanasemaje. Kuna nyimbo ni matusi matupu mwanzo mwisho tunasikiliza tu.

Zingine ni za kiingereza kama zile za wasanii wa nje unakuta shetani anatukuzwa, ushoga, ukahaba, usagaji, ulevi, ugomvi watu tunasikiliza midundo tu lugha hatuijui.

Iwe funzo siku nyingine watoa misaada au wale wale wanaorekodi vipindi vya watoto/wanafunzi wajiridhishe na nyimbo za kuwapigia watoto kama zina maadili mabaya au la ndio wapige
 
Walimu wawili wakuu wa Shule za Msingi Mlimani na Tunduma TC zilizopo Halmashauri ya Mji Tunduma Mkoani Songwe ambao walivuliwa vyeo kutokana na video iliyosambaa mitandaoni ikionesha Wanafunzi wakicheza wimbo wa Msanii Zuchu wa Honey, wamerejeshwa kwenye nafasi zao.

Akiongea na @AyoTV_ kwa njia ya simu leo Jumanne November 07, 2023, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji Tunduma, Philemon Magesa amethibitisha kuwa Walimu hao wamerejeshwa “Ni kweli taarifa hizo ni sahihi Walimu hao wamerejeshwa vyeo vyao"

Alipoulizwa sababu za kurejeshwa vyeo Walimu hao, Mkurugenzi huyo amesema “Walimu hao walivuliwa vyeo kutokana na maelekezo ya Waziri wa Elimu na wamerejeshwa kutokana na maelekezo wa Waziri wa Elimu"

Jana November 6, 2023 akiwa Bungeni, Spika wa Bunge laJamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt, Tulia Ackson aliishauri Serikali kuwarejesha kazini Walimu hao.
Jana November 6, 2023 akiwa Bungeni, Spika wa Bunge laJamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt, Tulia Ackson aliishauri Serikali kuwarejesha kazini Walimu hao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jana November 6, 2023 akiwa Bungeni, Spika wa Bunge laJamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt, Tulia Ackson aliishauri Serikali kuwarejesha kazini Walimu hao.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuwarejesha kazini au kwenye nafasi zao? Maana hawakutolewa kazini, hapa nawaza kama kuna mwalimu hapo shuleni alifurahia waziwazi kwa bosi wake kushushwa cheo sijua sasahivi atakuwa kwenye hali gani
 
Ifike muda kuwe na utaratibu maalum, na si kutegemea akili za mmoja kufanya kadri ya anavyoona ni sahihi, kisa tu ni kiongozi, hii itasaidia mana sheria na utaratibu utapunguza uonevu.
 
Walimu wawili wakuu wa Shule za Msingi Mlimani na Tunduma TC zilizopo Halmashauri ya Mji Tunduma Mkoani Songwe ambao walivuliwa vyeo kutokana na video iliyosambaa mitandaoni ikionesha Wanafunzi wakicheza wimbo wa Msanii Zuchu wa Honey, wamerejeshwa kwenye nafasi zao.

Akiongea na @AyoTV_ kwa njia ya simu leo Jumanne November 07, 2023, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji Tunduma, Philemon Magesa amethibitisha kuwa Walimu hao wamerejeshwa “Ni kweli taarifa hizo ni sahihi Walimu hao wamerejeshwa vyeo vyao"

Alipoulizwa sababu za kurejeshwa vyeo Walimu hao, Mkurugenzi huyo amesema “Walimu hao walivuliwa vyeo kutokana na maelekezo ya Waziri wa Elimu na wamerejeshwa kutokana na maelekezo wa Waziri wa Elimu"

Jana November 6, 2023 akiwa Bungeni, Spika wa Bunge laJamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt, Tulia Ackson aliishauri Serikali kuwarejesha kazini Walimu hao.
mkenda ana mihemko kama bao la kwanza.
 
Pale profesa anapoogopa honey wa watu kuitiwa shuleni! 😀😀😀
 
Back
Top Bottom