kama uabandika maharage unakuta nyama basi hapo pazuri
Hawaniwezi! Si rahisi kama unavyofikiria!
walimu wa shule ya msingi Shigala wilaya ya Busega mkoani Simiyu wamejikuta wamelala nje wa nyumba zao kutokana na vitendo vya kishirikina! Walimu hao wameeleza kuwa mara kadhaa wamekuwa wakikutwa na vituko kadhaa! '' unaweza ukala ugali na maharage au mrenda lkn tukiamka asbh tunakuta mifupa ya nyama mezani'''
mara kadhaa unaweza kuwa unapika maharage na upo hapo hapo jikoni wakati umefunikia na yanachemka ukifunua baada ya muda furani uangalie kama yameiva unakuta yamegeuka kuwa nyama!
Kama hiyo haitoshi mwalimu analala peke yake usiku lkn akiamka anajikuta ameingiliwa kimwili(anajikuta alikuwa kwenye ngono usiku). Walimu wamegoma kufundisha wanasubir hatima yao.
Wadau kama ni wewe ndo yanakukuta ungefanyaje?
ndio mambo ya Busega.
Kuna taarifa pia zilizodhibitiswa na polisi leo hii kuwa katika mji mdogo wa Nyamikoma km chache kutoka Shigala majira ya saa sita mchana wanawake wawili wamechomwa moto kwa tuhuma kuwa ni washirikina na inasemekana waume zao walikimbia na walikuwa wanafahamika hivyo ikatokea tafarani na kufanya wanaume wote kukimbilia waliokua na wasiwasi vijiji vya jirani vya Mwaburugu, Lamadi na Mwasamba hadi muda huu. Mimi ni mwl pia katika eneo hili hila watu kutoka Kaskazini hatuna amani kupangwa ndani ya maeneo haya.
Acha uoga dogo,piga kazi wewe unalialia unadhani JF ni Gaka wa kukuhamisha.
Acha uoga dogo,piga kazi wewe unalialia unadhani JF ni Gaka wa kukuhamisha.
Mtu anaamua kukuletea nyama basi anakupenda sana lakini hili la kuingiliwa na kulala nje hapo sjui labuda Simiyu yetu atusaidie!!
Nenda kalale bila nguo utapata source! !!leta source pls!
Wachawi wa kileo hao! Yaani anakula vitu alafu anakuachia nyama!
Wajaribu kuchoma mahindi, wanaweza kuta wamewekewa mkuu wa meza, japo wachawi wa kizamani wanaiogopa hii kitu