Walimu wa shule za msingi wanatakiwa waajiriwe wenye degree na sio waliofeli form 4 kama ilivyo sasa

Walimu wa shule za msingi wanatakiwa waajiriwe wenye degree na sio waliofeli form 4 kama ilivyo sasa

Dennis Robert Shughuru

JF-Expert Member
Joined
May 30, 2024
Posts
4,124
Reaction score
6,141
Zipo changamoto nyingi katika elimu yetu ya shule za msingi za serikali ambapo watoto wengi wa maskini na kipato cha chini ndo wanaposoma zinachangamoto ya uhaba wa ualimu, wanafunzi kukaa chini, kutokua na maabara n.k

Ila changamoto nayotaka kuongelea kwenye huu uzi ni swala zima la kiwango cha elimu cha walimu wa shule za msingi

MIMI NIKIWA RAIS NTAFANYA MABORESHO MAKUBWA SANA SHULE ZA MSINGI KAMA YAFUATAYO
  1. Kuongeza wigo wa masomo ya kingereza
  2. Kusoma programming language tokea primary
  3. Kusoma graphics
  4. Kusoma words, excel na PowerPoint
  5. Kufundishwa kuifanyia maintanance computer
Kwa hayo mabadiliko ni wazi hata degree za ualimu zinazotolewa haziko compatible na mabadiliko ya hali ya dunia yaani haziendani na hali ya sasa ya dunia ni wazi kunahitajika mabadiliko yaani sio tu degree bali hata aina ya degree hizo zinatakiwa kuendana na hali ya sasa

Nchi kama Finland, Singapore ili uwe mwalimu ni shuhuli pevu ndo maana wanatoa elimu bora sana hata sisi Tanzania tunaweza kama tukiamua sio fair ukiongea na mtoto wa shule za serikali ni kama anaenda kukua na sio kuelimika

 
Kufundisha ni kipawa ndugu zangu na moyo,watu weng wapo kufundisha TU kwa sababu ya maisha au marks alizopatq.
 
Huwezi fundishwa na mtu aliyefeli ilihali watoto wengine wanafundishwa na watoto waliofaulu ndani ya nchi hiyo hiyo sio sawa
Ngugu acha kudharau elimu za watu,walimu wa shule za msing hawajafel hata kdg,km umesoma shule za kata zaman kdg kuanzia 2005 kupata three TU ulikuwa shida sana
 
Huo ni ubinafsi uliochangamana na ujinga. Hao wenye degree unafikir ndio watafanya watoto wafaulu? Ualimu ni mbinu na njia za ufundishaji. Walimu wengi wa Diploma na Certificates ni walimu wazuri sana kuliko hata hao graduates....!!
 
kufundisha nikipawa na ndomana wanapitia mafunzo na unaweza kuwa na digirii ila usiweze kufundisha...walimu wa upe wamefanikiwa kuzalisha ,walimu,madaktari,wanajeshi ,manesi,mawaziri ,wabunge,maprofesa.n.k .wakati walimu hao wamemaliza la4 elim ya mkoloni na darasa la saba.kufundisha ni talent sio elimu
 
Huo ni ubinafsi uliochangamana na ujinga. Hao wenye degree unafikir ndio watafanya watoto wafaulu? Ualimu ni mbinu na njia za ufundishaji. Walimu wengi wa Diploma na Certificates ni walimu wazuri sana kuliko hata hao graduates....!!
Mtu aliyefeli hawezi kuwa mwalimu
 
Back
Top Bottom