Walimu wa secondary kwenda msingi serikali inakwepa nini

Walimu wa secondary kwenda msingi serikali inakwepa nini

Oxpower

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2012
Posts
2,181
Reaction score
3,115
Naamini wote sisi ni wazima

Jana nmeona tangazo linatembea lihusulo uhamisho wa walimu wa secondary wa sanaa kwenda kufundisha shule ya msingi kwa lengo la kufidia upungufu wa walimu uliopo shule za msingi.

Nmejikuta napata maswali
Je ni kwamba serikali haina pesa ya kuajiri walimu wengine au inaongeza ufanisi katika kazi na ni kwa namna gani sasa?
Mtaani kuna walimu tokea 2015, je hawa hatima yao ni nini?

Kiufanisi litakuaje hili?

Je hawa walimu wataokwenda shule za msingi wataweza kuendana na kasi ya huko
 
Naamini wote sisi ni wazima

Jana nmeona tangazo linatembea lihusulo uhamisho wa walimu wa secondary wa sanaa kwenda kufundisha shule ya msingi kwa lengo la kufidia upungufu wa walimu uliopo shule za msingi.

Nmejikuta napata maswali
Je ni kwamba serikali haina pesa ya kuajiri walimu wengine au inaongeza ufanisi katika kazi na ni kwa namna gani sasa .
Mtaani kuna walimu tokea2015 je hawa hatima yao ni nini?

Kiufanisi litakuaje hili?

Je hawa walimu wataokwenda shule za msingi wataweza kuendana na kasi ya huko
Wanaosubiri ajira watasubir sana.
Au hakuna tena
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Unapopunguza watu kwenda sehemu nyingne jiulize huko Unakopunguza wanafunzi wanapungua au wanaongezeka. Tiba sahihi ni kuwekeza kwe elimu ili iwe bora na sio short cut
 
Walimu wa cheti nadhani wataoewa muda wa kujiendeleza baada ya hapo kwa atakaekuwa bado watamterminate ...nadhani wanataka kufuta cheti...pia serikali iko hoi kulipa mishahara hawana namna...hamjiulizi wafanyakazi wa vyeti feki walivyotolewa kwa jinsi wanavyopenda kick wasinge ajiri kweli idadi ile ile?
 
Hapa kuna shida, elimu yetu itazidi kudidimia Zaidi. Mafunzo ya mwalimu wa primary ni tofauti na sekondari anashughulika na adolescent.

Pia kupunguza walimu wa sekondari kwa kigezo kwamba wamezidi sio hoja ya kuwaambia watz wenye akili timamu. Idadi ya wanafunzi waliopo mashuleni ndio inaonesha uhutaji wa walimu na wala sio idadi ya vipindi ambavyo mwalimu anafundisha.

Unakuta shule ina wanafunzi mia tano wa kidato cha kwanza, wamewekwa kwenye vyumba vinne, hapo inachukuliwa mwalimu anafundisha madarasa manne wakati yalitakiwa yawe kumi au zaidi kutokana na idadi ya wanafunzi na ratio ya kila wanafunzi 40 kwenye darasa
 
Ila nakumbuka kabla huu mpango haujaanza waliufanyia kwanza majaribio arusha naona wakaona unafaa sasa wameamua kuufanyia kazi kabisa,sema mim hofu yangu wamepunguza walimu sec kwahyo hawajaokoa kitu hapo
 
Kwa nchi zinazoelewa umuhimu Wa elimu,hawawez kumchukua mwalimu Wa sekondar kumpeleka Shule ya msingi,sababu njia za ufundishaji wa Shule za msing na sekondar ni tofauti,content ya msing na sekondar ni tofauti,na kuna tofauti ya kiuzoefu pia.sasa sijajua wamezingatia vigezo gan?
Mwongo mkubwa, ukienda nchi za watu chekechea anafundishwa na degree holder siyo certificate, primary hadi secondary pia ni degree holder na PhD,
 
Mwongo mkubwa, ukienda nchi za watu chekechea anafundishwa na degree holder siyo certificate, primary hadi secondary pia ni degree holder na PhD,
Mkuu kama we sio mwalimu naomba ukae kimya, hao unaowasemea wana degree sijui PhD wanakuwa wamespecialize kufundisha shule za misingi ila sio kama huku ambako hao wanaoamishwa wamespecialize kufundisha sekondari.
 
Mwongo mkubwa, ukienda nchi za watu chekechea anafundishwa na degree holder siyo certificate, primary hadi secondary pia ni degree holder na PhD,
Tatizo hujaelewa,hapo Uganda tu,wanatoa degree in primary education.huyo mtu mwenye degree anatakiwa asome mambo ya Shule ya msingi,sio asome mambo ya sekondar harafu umpeleke akafundishe Shule ya msingi.sasa,niambie chuo gan Tanzania wanatoa degree ambayo inadili na elimu ya Shule ya msingi.usikurupuke tu kubisha.

Sent from my TECNO H6 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom